Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,322
- 33,126
Wakala wa Barabara nchini (Tanroads), imesema italingoa bango la kampuni ya matangazo ya A1 Outdoor, lililojengwa katika hifadhi ya barabara kwenye eneo la Tazara.
Tanroads imesema kuwa italiondoa bango hilo endapo kampuni hiyo, itashindwa kuliondoa kama ilivyoagizwa na wakala hao.
Miezi kadhaa iliyopita, Tanroads ilisitisha mpango wa kuweka bango katika barabara zake nchini hadi itakapotoa muongozo mpya kwa wafanyabiashara wa matangazo hayo.
Agizo hilo, limeonekana kupuuzwa na kampuni ya A1 Outdoor baada ya kuamua kuweka bango kubwa katika eneo linalodaiwa kuwa ni hifadhi ya makutano ya barabara za Mandela na Nyerere kwenye eneo la Tazara jijini Dsm.
Meneja wa Tanroads mkoa wa Dar es Salaam, James Nyabakari alisema waliiandikia kampuni hiyo, isitishe ujenzi na kungoa bango hilo kwa kuwa liko kwenye hifadhi ya barabara, lakini imegoma kutekeleza agizo hilo.
"Yule jamaa baada ya kumuandikia barua alikataa kusitisha ujenzi na akajibu kuwa eneo hilo si la hifadhi ya barabara ya Mandela, bali ni la bustani ya Shirika la Reli kati ya Tanzania na Zambia (Tazara).
"Sisi tuna uhakika eneo lile ni la hifadhi ya barabara na tulikwenda mbali zaidi tukamjibu na kumtumia nakala ya mchoro wa ramani ya barabara, ikionyesha mipaka ya hifadhi zake, lakini inaonekana hajaridhika, " alisema Nyabakari.
Nyabakari alisema taarifa kuhusiana na tatizo hilo, wamezipeleka makao makuu ya Tanroads, ili kupata ushauri zaidi wa kisheria kabla ya kuanza kuchukua hatua zaidi.
Alifafanua wamekuwa wakijibizana baina yao na A1 Outdoor kwa njia ya barua kuhusu bango hilo, lakini kampuni hiyo, lakini haijawa tayari kutii agizo la Tanroads.
"Akizidi kukaidi sisi tutalingoa halafu kama yeye hajaridhika ataenda mahakamani kwa sababu sisi tuna kanuni na sheria ambazo zinatuongoza katika kazi zetu," alisema.
Nyabakari alisema awali A1 Outdoor haikuomba ruhusa ya kujenga bango hilo na kwamba walishtukia na kwamba baadaye walishangaa kuona bango hilo, likiwa tayari limejengwa.
Bango laigombanisha serikali na Kampuni!
Tanroads imesema kuwa italiondoa bango hilo endapo kampuni hiyo, itashindwa kuliondoa kama ilivyoagizwa na wakala hao.
Miezi kadhaa iliyopita, Tanroads ilisitisha mpango wa kuweka bango katika barabara zake nchini hadi itakapotoa muongozo mpya kwa wafanyabiashara wa matangazo hayo.
Agizo hilo, limeonekana kupuuzwa na kampuni ya A1 Outdoor baada ya kuamua kuweka bango kubwa katika eneo linalodaiwa kuwa ni hifadhi ya makutano ya barabara za Mandela na Nyerere kwenye eneo la Tazara jijini Dsm.
Meneja wa Tanroads mkoa wa Dar es Salaam, James Nyabakari alisema waliiandikia kampuni hiyo, isitishe ujenzi na kungoa bango hilo kwa kuwa liko kwenye hifadhi ya barabara, lakini imegoma kutekeleza agizo hilo.
"Yule jamaa baada ya kumuandikia barua alikataa kusitisha ujenzi na akajibu kuwa eneo hilo si la hifadhi ya barabara ya Mandela, bali ni la bustani ya Shirika la Reli kati ya Tanzania na Zambia (Tazara).
"Sisi tuna uhakika eneo lile ni la hifadhi ya barabara na tulikwenda mbali zaidi tukamjibu na kumtumia nakala ya mchoro wa ramani ya barabara, ikionyesha mipaka ya hifadhi zake, lakini inaonekana hajaridhika, " alisema Nyabakari.
Nyabakari alisema taarifa kuhusiana na tatizo hilo, wamezipeleka makao makuu ya Tanroads, ili kupata ushauri zaidi wa kisheria kabla ya kuanza kuchukua hatua zaidi.
Alifafanua wamekuwa wakijibizana baina yao na A1 Outdoor kwa njia ya barua kuhusu bango hilo, lakini kampuni hiyo, lakini haijawa tayari kutii agizo la Tanroads.
"Akizidi kukaidi sisi tutalingoa halafu kama yeye hajaridhika ataenda mahakamani kwa sababu sisi tuna kanuni na sheria ambazo zinatuongoza katika kazi zetu," alisema.
Nyabakari alisema awali A1 Outdoor haikuomba ruhusa ya kujenga bango hilo na kwamba walishtukia na kwamba baadaye walishangaa kuona bango hilo, likiwa tayari limejengwa.
Bango laigombanisha serikali na Kampuni!