Wananchi wa Goba wakarabati barabara wenyewe, Serikali za Mtaa washawishi bango litolewe

The Sheriff

JF-Expert Member
Oct 10, 2019
617
1,800
Barabara-kwa-watu-wa-Goba.jpg

Hii ni picha ya bango la mradi wa ujenzi na ukarabati wa kilomita mbili (2) Goba kwa Awadhi ambayo imesambaa kwa kwenye mitandao ya kijamii.

Mradi huu ni wa ukarabati na ujenzi wa mitaro ambapo unatokana na nguvu za wakazi wa eneo hilo.

FB_IMG_1710938422294.jpg

Inaelezwa wakazi hao wamekubaliana kujenga mitaro kwa kutumia zege na makadirio ya bajeti ni Shilingi milioni 40 kutoka kwa wakazi 95 ambao wameahidi kuchangia. Hadi sasa, zaidi ya Shilingi milioni 16 zimekusanywa, na ujenzi umeshaanza.

Sema tofauti na mabango mengine ambayo mara nyingi yamekuwa na ujumbe uliozoeleka kwamba UKIMWI unaua, bango hili limehitimishwa na ujumbe wa “Tuchange wote kujenga barabara yetu”.

Pia inasemekana kuwa mjadala huo umewaibua viongozi wa mtaa ambao waliwashawishi wananchi kuliondoa bango hili bila mafaniko. Wananchi wanasema kuwa endapo watalitoa, basi viongozi waitishe mkutano kuelezea barabara hiyo itatengenezwa lini.

Uamuzi wa wananchi wa Goba wa kujikomboa kwa kujenga barabara yao wenyewe ni ishara ya ujasiri na kujitolea katika kuleta mabadiliko katika jamii yao. Hii ni hatua ya kipekee ambayo inaonyesha nguvu ya umoja na dhamira ya kuboresha maeneo yetu.

Je, mtaani kwenu mnachukua hatua gani kama barabara inazingua?
 

Hii ni picha ya bango la mradi wa ujenzi na ukarabati wa kilomita mbili (2) Goba kwa Awadhi ambayo imesambaa kwa kwenye mitandao ya kijamii.

Mradi huu ni wa ukarabati na ujenzi wa mitaro ambapo unatokana na nguvu za wakazi wa eneo hilo.

Inaelezwa wakazi hao wamekubaliana kujenga mitaro kwa kutumia zege na akadirio ya bajeti ni Shilingi milioni 40 kutoka kwa wakazi 95 ambao wameahidi kuchangia. Hadi sasa, zaidi ya Shilingi milioni 16 zimekusanywa, na ujenzi umeshaanza.

Sema tofauti na mabango mengine ambayo mara nyingi yamekuwa na ujumbe uliozoeleka kwamba UKIMWI unaua, bango hili limehitimishwa na ujumbe wa “Tuchange wote kujenga barabara yetu”.

Pia inasemekana kua mjadala huo umewaibua viongozi wa mtaa ambao waliwashawishi wananchi kuliondoa bango hili bila mafaniko. Wananchi wanasema kuwa endapo watalitoa, basi viongozi waitishe mkutano kuelezea barabara hiyo itatengenezwa lini.

Uamuzi wa wananchi wa Goba wa kujikomboa kwa kujenga barabara yao wenyewe ni ishara ya ujasiri na kujitolea katika kuleta mabadiliko katika jamii yao. Hii ni hatua ya kipekee ambayo inaonyesha nguvu ya umoja na dhamira ya kuboresha maeneo yetu.

Je, mtaani kwenu mnachukua hatua gani kama barabara inazingua?
Hii nayo ni aina ya maandamano... Good move
 
Ni upumbavu kuchanga pesa wakati serikali imekopa pesa kwa ajili hiyo hiyo.

Ujamja ni kusimama kidete na kuhoji pesa zilizotilewa na WB Kwa ajili ya kujenga miundo mbinu ya Nini la Dar?
Watu wamechoka, miundombinu ya Ubungo ni mibovu, viongozi wa mtaa wakienda Serikalini wanaambiwa pesa hamna, unataka watu wazidi kuharibu magari yao na kutumia gharama kubwa ya usafiri wakati wanaweza kujichanga kutengeneza njia yao?

Serikali kwa namna moja au nyingine imefeli, acha watu wajiletee maendeleo yao.
 
Ni upumbavu kuchanga pesa wakati serikali imekopa pesa kwa ajili hiyo hiyo.

Ujamja ni kusimama kidete na kuhoji pesa zilizotilewa na WB Kwa ajili ya kujenga miundo mbinu ya Nini la Dar?
Wako sahihi kabisa kama wewe unashindwa kuingia kwako na barabara inakuwa maji taka kila siku utaanza kutegemea serikali hii feki si utasubiria mpaka ufe? Waungwe mkono.
 
Waswahili huwa hamna tabia ya kujenga nchi wenyewe bali kila kitu mnasubiri Serikali. Hawa wa Goba wameona miradi haiendi au wamesubiri sana na labda hela zimeishapigwa.

Hongera kwao hata mimi kuna siku niliona Mashimo mbele ya nyumba na halmashauri hawana Habari
Niliyafukia kwa hela zangu.

Kuna wakati kujitolea kwa faida ya wengi ni vizuri wala sio kosa kisa tu eti ni kazi ya serikali. Kwa hiyo mpaka watu wafe?

Tena mjufunze kuwa na Charities nyingi. Kuna nchi matajiri lakini wana Charities tunazochangia kwa kupata maendeleo au hata utafiti wa madawa

Big up kwao
 
Ni upumbavu kuchanga pesa wakati Serikali imekopa pesa kwa ajili hiyo hiyo.

Ujanja ni kusimama kidete na kuhoji pesa zilizotolewa na WB Kwa ajili ya kujenga miundombinu ya nini la Dar?
Sioni sababu ya kuita kitendo chao kuwa ni upumbavu kwa sababu wewe hujui maafa na shida wanazozipata wakati barabara hiyo ikizidi kuwa mbovu. Neno upumbavu si zuri kumwita mwenzako.
 
Watu wamechoka, miundombinu ya Ubungo ni mibovu, viongozi wa mtaa wakienda Serikalini wanaambiwa pesa hamna, unataka watu wazidi kuharibu magari yao na kutumia gharama kubwa ya usafiri wakati wanaweza kujichanga kutengeneza njia yao?

Serikali kwa namna moja au nyingine imefeli, acha watu wajiletee maendeleo yao.
Ikiwezekana wajenge na bandari yao. Tumechoka kupigwa pale bandari ya magogoni.
 
Back
Top Bottom