Bangi mbaya:

X-PASTER

JF-Expert Member
Feb 12, 2007
11,610
1,810
kuna maeneo fulani mkoani morogoro kama unaelekea Kinole, kuna daraja jembamba ambalo linaruhusu kupita gari moja tu kwa wakati mmoja.
Sasa siku moja kulikua na gari mbili zinatokea pande mbili tofauti na zote zinataka kukatiza daraja lile, na kila mmoja ana haraka sana. Si unajuwa tena mabasi ya abiria kwa kukimbilia abiria.
Sasa wakawa wapigiana honi kila mmoja anampigia mwenzake ili apite yeye kwanza, na kila mmoja hataki kumpisha mwenzake.

Mmoja wao akaamua kuzima gari moto, basi yule wa pili nae pia akazima gari moto. Wakaka hapo kama lisaa limoja hivi.

Mmoja kati ya wale madereva akaamua kutoa Biblia na kuanza kusoma gazeti.
Yule mwengine akaamua kushuka ndani ya gari kisha akaenda kwa yule dereve mwenye kusoma Biblia akamwambia "Mjomba! Ukimaliza kusoma hiyo Biblia nipe na mie nisome"
 
Back
Top Bottom