Babu wa Loliondo afungiwa kwa muda kutoa huduma...

Babu amekwambia anatibu kwa dawa ya mti aliooteshwa pamoja na maombi. Sasa unaweza kuyapima maombi kwa kisayansi!

Alafu amesha sema hiyo dawa ukichemsha mwenyewe haitibu, yeye akitoka hapo kwenda kuwapelekea kwingine haitibu, mgonjwa asipoenda na kuipokea hapo yeye mwenyewe na kupewa na mikono ya babu haitibu so hiyo science itapima kitu gani hapo? But kiroho tunaweza ipima kwamba imani itakufanya wewe unyanyue mguu wako uende kule, unyenyekevu utakufanya wewe ukubali kuacha nyumba yako nzuri na magari na chakula huku ukiweka elimu yako pembeni umfuate babu asiye na jina wala elimu kwenye nyumba yake hiyo ndogo ya matope akakupe dawa inayoponya kwa neno alilopewa kwenye ndoto (Mungu mjanja maana alijua watamhonga babu awape upendeleo wachache wenye uwezo kwanza), but babu ni mtii huyu haongezi wala hapunguzi alichoambiwa (another character of a child of God)...so whats the healing power in that 'MUTI'...the word ofcourse which was given to babu by His God; who then is this God this is a spiritual question...Ukishahakikishiwa ndani ya dhamira yako na ukaipima kwa neno la Mungu tulilopewa (Biblia) ukaona halijapungua then umekiri uponyaji wahuyo mtoa ndoto and according to Babu ni Yesu maana yeye ni mchungaji...Kama kweli imo ndani yake basi ni neno ndilo linaponya hapo huo mti ni media ya kupitisha huo uponyaji kwani Mungu pia anajua cultural setting ya watanzania ni rahisi kuamini mti shamba/physical matter kuliko neno lakuambiwa...Hii ni based na analysis yangu mwenyewe na wala si ukristo nilionao lisije likatukanwa jina la Bwana yesu kwaajili yangu...

Then neno linasema kwa matendo yao mtawajua...kama kweli babu hapokei hata senti tano then yuko biblically correct kwamba umepewa bure na utoe bure..hapo anawaacha wenye dini kwa mbali sana...Tena neno la Mungu linasema God is not respector of person kila mwenye roho iliyotayari hupokea this is proved to both..babu aliyetamani kutibu hayo magonjwa (according to what is said in JF) na wale wote wanaoenda kunywa dawa ya babu huku wakiweka dini zao pembeni na kupokea uponyaji; this is also biblically proved kwamba Bwana Mungu wa majeshi ameleta wokovu kwa wote kwa myunani kwanza na kwa mataifa pia, again babu ni mtii hapunguzi wala haongezi neo sisi je tumeambiwa kila mwenye kulitaja jina la bwana na aache uovu je is this what we do?...niajabu sana wenye dini wameingia kwenye mtego wa kupeleka habari njema kwa wateja wao tu na kuiacha dunia ikiwaya waya kama machele...God promised if you wont take this good news to all nations then I will raise stones to do it on your behalf...so watumishi wajiulize mbona ukimwi bado unatesa dunia wakati wao wamebeba anointing kwenye makanisa huku watu wakiendelea kupukutika? Je yesu alikuwa mwongo aliposema mtapokea nguvu nanyi mtakuwa mashahidi wangu Galilea, Samaria na kwa mataifa yote? Ushuhuda wetu uko wapi? Je ni kipi hatukifanyi sawa? Babu is a challenge to the gospel we are preaching!
 
Ndugu yangu amerudi leo kutoka kwa Babu kupata dawa, amenipa hali halisi kuwa Babu yupo kwa ajili moja tu kusaidia watu na hapati hata senti tano. Ni kuwa mpaka sasa ana wasaidizi sita ambao wote ni wachungaji wanaomsaidia kutoa dawa na kwa siku anahudumia magari yapatayo elfu moja. Na mchanganuo wake kwa kila Tsh 500 inayotolewa ni kuwa; Tsh 300 inakwenda kwenye huduma za kanisa yote kama ilivyo bila kupungua hata senti na Tsh 200 wanachukua hawa wasaidizi wake sita kwa kazi ngumu wanayoifanya. Hivyo yeye hapati hata mbuni. :-(

Kwa hakika huyu ametumwa na Mungu aisee kuja kusaidia watu wa kila aina. Tajiri na maskini.
Mungu ampe maisha marefu na huo uwezo aliopewa uendelee kufanya kazi.
 
Sasa masharti hayo yamekushinda nini? Mbona basic kabisa. Unataka waipime vipi dawa yako kama hautawaambia inaponya nini na dosage yake ni nini? Uko serious kweli mkuu??

Soma tena thread yangu member!
Wao wangekua wastaarabu wangekubali wapokee unga.
Lakini hawakukubali.
Huoni ndio kuibiwa jua la saa sita!.
Hapo hata ukipewa maelekezo haitokusaidia ukikumbuka wao ndio wapo hapo jikoni.
Kesho unasikia Dr fulani amefanya utafiti na amegundua dawa fulani.
Sijui umetaka niwe-serious vipi?
 
Naamini kuna ukweli shemeji yangu alimpeleka mkuu wake wa kazi ambaye amelemaa mkono (wakati wapo njiani kurudi A -town Kibosile alisikika alishangaa kuwa mkono unapata nguvu) awali kwakuwa naye (shemeji) alikuwa na vidonda vya tumbo kwa siku nyingi ikabidi aunge foleni, toka apate hiyo dawa hajasikia tena hali ya kusumbuliwa na vidonda vya tumbo hivyo watu wasidharau wenye matatizo waende, inaonyesha huyu mzee amechaguliwa na mungu atumike sio kama hao tuliozoea
 
It is True, I have the evidence.
...Sawa mkuu nina dada yangu ana saratani ya titi niko kwenye maandalizi ya kumpeleka huko ingawa issue ya usafiri inaelekea kunipotezea stimu. Bei zinazotajwa ili mtu kufika huko nayo ni changamoto!!
 
Huyu Mzee Mungu ambariki, kazi yake inaonyesha alivyo mtiifu kwa Mungu.....
Wanaomlaani, Mwenyezi Mungu awaadhibu....
 
Hii ni sawa, lakini kama serikali inabidi/ni muhimu ijiridhishe pia kwamba dawa hiyo licha ya kuponya kama inavyodaiwa haina madhara mengine makubwa kwa mtumiaji (sasa na baadae). kumbuka ni maelfu ya watu wanapatiwa tiba hii na wengine wanatolewa mahospitalini kwenda huko kwa ajili ya tiba, sasa kama ina madhara ni watu wengi wataathirika na serikali ina jukumu la kulinda afya na maisha ya watu wake.

Very good SMU!! This is the thing, we are not critically thinking. We are so used to easy things just because we are desperate. The only thing that's bringing this hyper about this guy in Loliondo is DESPERATION that's why we just don't think! I totally agree with the government to investigate this dawa scientifically to make sure it will not bring any effects to people, especially HIV patients whom their drugs are NOT even good at the moment. We all know kwamba some ARV's zinaleta side effects kwa wagonjwa, so why allowing them to take another drug which we don't even know what it is?? Is it because we believe in GOD? How many people have already come in the name of GOD and then we found out they were actually lying?? Just think hard, if this dawa has bad effects how many people will be affected?
 
kuna sample ya huo mti hapo kwa babu.....wapime huo
...Preta sidhani kama huyo mzee ni mjinga kiasi hicho ni kweli huo mti upo hapo kijijini na hata kwenye maeneo mengi nchini lakini yaelekea kuna vitu vingine anavyochanganya kiasi kwamba si rahisi yeye kutoa hiyo siri. Wakichuma tu hayo majani na kupima wanaweza kukuta mambo tofauti na matarajio yao kiasi wakaishia kumpiga stop babu kuwa ananywesha watu sumu maana password zingine hawajui....
 
<font face="Comic Sans MS"><font size="4"><font color="purple">ni kawaida ya nuru na giza kushindana.....bahati mbaya kwa giza maana halitaishinda nuru kamwe
ndugu yangu nani kakwambia kwa babu wa loliondo ni mwanga? Ndiyo maana mungu anasema ''watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa'' na kweli tutaangamia. yule babu ni Ibilisi at work,ukweli utajifunua na mungu wetu atajitukuza. tunatumia jina la mungu vibaya sana sasahivi!
 
Kufuatia ujumbe uliotumwa na wizara ya afya na ustawi wa jamii kwenda Loliondo kwenda kuangalia uhalali wa matibabu yanayo tolewa na babu inasemekana babu hakuwa tayari kuruhusu wataalam hao kuipima dawa yake. ndugu wanajamii je hiyo imekaaje?
Zile za shee yahaya pale mwembetea zimepimwa?
 
Yule babu wa Loliondo aliyepata umaarufu kwa muda mfupi kutokana na dawa yake kutibu magongwa sugu amefungiwa kuendelea ma kutoa dawa kwa wagonjwa na wizara ya afya,wizara imesema inataka kuifanyia utafiti dawa hiyo pia wamemsauli mchungaji huyo mstaafu kuisajili dawa yake mamlaka ya chakula na dawa(TFDA). Source.Channel ten habari ya saa 7 mchana.
 
Hata wakina kibwetere serikali iliwaacha kwa mantiki ya uhuru wa kuabudu, haijasemwa inapimwa azuie isipokuwa je ikitokea baada ya miezi 6 wale wote waliokunywa hiyo dawa wakaanza kupata madhara makubwa si ninyi mtaigeukia na kuilaumu serikali ilikuwa wapi?
shame on you
 
Sasa wateja wote walioko kule watasubiri hadi ifanyiwe utafiti???
 
ulichosema ni sahihi kabisa mkuu, wajitolee kuwapima bure wagonjwa wote walioitumia dawa na kupata uthibisho kutoka hospitali walizokuwa wanahudhuria matibabu kwamba ni kweli walikuwa na magonjwa hayo na kwa sasa hawaumwi tena baada ya kuitumia dawa wa babu

Kupima ufanisi wa kitu kuna njia nyngi: mfano, ufanisi wa mkandarasi unaweza kupimwa kwa kupima ubora wa jengo au barabara aliyojenga na si kukagua vyeti vyake au zana alizotumia. Nawashauri wapime wagonjwa kama wamepona au la.
 
Back
Top Bottom