Babu wa Loliondo afungiwa kwa muda kutoa huduma...

Wawachukue wagonjwa wa ukimwi, kisukari na kifua kikuu kama "sample" wawapeleke na baada ya kunywa wawapeleke maabara kupima kama bado wanasumbuliwa na magonjwa yao. Hili halihitaji PHD kulithibisha, kupima dawa ni kutaka kuiba formular ya Babu bila idhini yake.

hawa walitaka per diems tu, wameshapata wachape rapa.
 
Fedha za nini?, nawashangaa hawa viongozi wa nyumba za ibada wanajirimbikizia mali utadhani wataishi milele, shame to kakobe et al.
 
Fedha za nini?, nawashangaa hawa viongozi wa nyumba za ibada wanajirimbikizia mali utadhani wataishi milele, shame to kakobe et al.

hivi zile dhahabu Kakobe aliwavua waumini alizipeleka wapi?
 
Anajitengenea ka barick kake, mambo yakiwa si mambo anaanza kuchimba!!
BTW mzima wewe?

mimi nimekumiss hivyo halafu wewe hujui......njoo basi unisindikize kwa babu naenda ijumaa
 
Kupima ufanisi wa kitu kuna njia nyngi: mfano, ufanisi wa mkandarasi unaweza kupimwa kwa kupima ubora wa jengo au barabara aliyojenga na si kukagua vyeti vyake au zana alizotumia. Nawashauri wapime wagonjwa kama wamepona au la.

Mkuu kuchukua wagonjwa eg wa HIV na kuwatumia kwenye majaribio kama wameponywa na hiyo dawa ni kinyume na medical ethics,utakuwa unaingilia haki ya privacy sharti hiyo dawa ipatikane ifanyiwe majaribio kwanza,hapo imekaaje?
 
mimi nimekumiss hivyo halafu wewe hujui......njoo basi unisindikize kwa babu naenda ijumaa
Likewise Preta, Ngoja nifanye michakato nije nije twende kwa babu!! Namuombea babu aendelee kudumu!
Yaeda wazima lakini?
 
Uko sahihi wapime wagonjwa kama wamepona kweli au la. Lakini wasiishie hapo tu, kama hiyo dawa inaponya kweli ni vizuri sampuli zikachukuliwa kufanyiwa uchunguzi wa kina, kwa muda mrefu wanasayansi wamekuwa wakihangaika kupata dawa za magonjwa haya sugu. Yawezekana kuna kemikali fulani ambazo zinapatikana katika mmea huo ambazo zinaleta tiba, Dunia inahitaji matumaini na matumaini hayo yakichimbukia Tanzania hatutakaa tusahaulike katika historia ya dunia, Vilevile watu watamtukuza Mungu kwa kazi zake kama ni kweli ameoteshwa na Mungu.
Nikweli Babu anasema ni dawa ya kiimani na inamasharti, lakini kama binadamu na jumuiya ya wanasayansi kwa ujumla hatuna budi kujaribu kuchunguza tujue kulikoni.
:amen:
 
1. Hakuna hata kiongozi mmoja hapa Tanzania kwa sasa mwenye uwezo wa Kwenda kinyume na matakwa ya mamia ya wanachi wenye nia ya kutumia tiba ya Babu...Ajari aone!!!

2. Viongozi wengi jumlisha na hao waliotumwa .... wanaihitaji hiyo tiba na hawana ujasiri hata ya kuihoji.

3. Viongozi na wansayansi wengi tayari wemeshaitumia dawa ..hivyo hivyo ilivyo ..bila kuihakiki wala porojo nyingine..

4. Ni kweli huduma ya Tiba kwa magonjwa sugu ..iko ukingoni...kila mtu jumlisha viongozi na wataifiti wanasanyansi...wamechanganjikiwa tu... Kilichopo kitatumika ..hadi kiji regulate chenyewe..!
 
Ina maana babu hajatoa hata namba ya account tuchangie huduma! Anyway tenda wema nenda zako usitizame nyuma. Anachofanya babu ndiyo utumishi wa kweli yeye hayuko kibiashara na hii inadhihirisha babu kweli katumwa na Mungu kuokoa watu. Zidumu harakati za babu. Vipi mustakabali wa akina ndodi??
 
huyu babu kweli kaamua kuokoe bila ht kujali atapata nn... Mungu azidi kumbariki na kumpa maisha marefu......
 
Wale jamaa wa wizara waliotumwa lazima watakuwa walibeba dondoo zao za kiukiritimba zaidi. Kwanza wangemchunguza kama amejiunga na CHAWATIATA ambacho kinakubalika pale wizarani, kama anacho kibali cha serikali kuendesha shughuli zake, kama madawa anayotumia yamepitia TBS, kama Kituo cha tiba asilia Muhimbili wameruhusu aendelee, kama bodi ya madawa ya taifa imeridhia mazingira ya tiba kutumika, kama mabwana afya wameruhusu, kama analipa kodi kwa serikali, kama anatoa risiti kwa pesa anayopokea, kama kuna ukaguzi wa mahesabu na ripoti wangetaka kuiona, .....

Kadhalika, katika hao waliokwenda kule, najua ni lazima wakuu wa vitengo vinavyoshughulikia tiba mbadala wangekuwamo, ambao kusema kweli wapo kikazi zaidi kwa maana ya policies za wizara kwenye makaratasi lakini hawana msaada wowote kuendeleza tiba mbadala, maana shughuli zao zaidi ni kuzunguka mikoani na kupata perdiem na hawana lolote wanaloweza kujivunia tangu kitengo kianze enzi za Prof wa Mifupa wa Rorya ambaye ndiye pioneer wa kitengo hicho. Hawasikii ushauri na wana viburi ajabu. AAmefanya vizuri Ambilikile kuwatolea nje jamaa hao, maana waganga wengi sasa hivi wanawakwepa watu hao kwa ulaliaji.

Watu kibao wametamka bayana kwamba walikuwa wanaumwa na sasa wamepona kwa dawa hiyo, sasa wanachunguza mganga au dawa? Kwa nini wasifanye utafiti mwepesi kabisa kwa kupeleka dondoo kwa wanaohudhuria wanaumwa nini na tangu lini na sasa wanayo maoni gani juu ya magonjwa yao baada ya kutibiwa? Huhitaji kuingia darasani kutafuta ukweli huo. Kama mzee wa watu angekuwa anatengeneza vidonge wangetafiti kwenye maabara kisayansi ya sasa. Lakini dawa ya mzee huyo inapoteza nguvu ukienda mbali naye, tena huwezi hata kumchukulia nduguyo nyumbani ila anaitoa yeye mwenyewe kwa mkono wa kushoto na maombi kwa Mungu. Waende kwa Askofu Laizer wa Arusha akawaambie uzoefu wake yeye mwenyewe na tiba hiyo kama hawaamini nkwamba watu wa kawaida watakuwa wakweli. Na yule Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Kilimanjaro tuliyemwona kwenye picha akichukua dawa kwa nini hawamwamini? Wanatengeneza mazingira ya ulaji hawa, hawana lolote.
 
Hawa naona wamekosa kazi! Wameiba hela ya vyandarua, halafu MUNGU katuletea uponyaji wa MAGONJWA SIGU nako wanataka kuchokonoa. Na wakijaribu kumgusa babu lazima waumwe kisukari kisichopona hao
 
kuna sample ya huo mti hapo kwa babu.....wapime huo

Hii ndiyo sawa...wachukue mti wapeleke maabara..wafanye wanavyojua wao,au chukua mgonjwa mmoja mnayemfahamu alikuwa anasumbiliwa na maradhi hayo ambayo Babu anatoa tiba....Lazima wapo wengi tuuu...na Historia zao na mafaili yao yapo...wacheck vipi bado wanaumwa au laa?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom