Personal Plea Kwa Rais Magufuli: Kama ameweza kuwasamehe wabakaji, wauaji, mafisadi, wahujumu, anaweza pia kumsamehe Eric Kabendera, amzike mama yake

Pascal Mayalla

Platinum Member
Sep 22, 2008
50,503
113,616
Wanabodi
Tangu kukamatwa kwa Mwandishi wa habari za kiuchunguzi Eric Kabendera, na kukamatwa kule kukahushishwa na makala zake, na kwa vile ni mimi niliyekuwa natafsiri makala za majarida ya nje na kuzileta humu jf, hivyo nikatuhumiwa kuwa ni makala za jf ndio zimemchongea Eric Kabendera kukamatwa, sijawahi kujibu chochote kwasababu Eric Kabendera hajakamatwa kwa ajili ya makala zake au kazi ya kalamu yake , bali ameshitakiwa kwa makosa mengine na sio makosa ya kiuandishi.

Lakini leo baada ya kupokea taarifa hii
Mama mzazi wa mwandishi Erick Kabendera, Verdiana Mjwahuzi amefariki dunia leo Jumanne Desemba 31, 2019. Mtu wa karibu na familia amethibitisha

View attachment 1308015
Shocked!.
Kama ni kweli Eric Kabendera anashikiliwa kwa sababu ya kalamu yake hivyo hayo mengine yote ni kisingizio tuu, na yeye ndiye alikuwa tegemeo la mama yake na mama yake amefariki baada ya kukosa huduma na usongo wa mawazo wa kukamatwa kwa mwanaye, na hatimaye huyu mama amekufa, then usually karma ya kifo, hulipizwa kwa kifo!. Hivyo karma ya kifo cha huyu mama, isipokuwa reversed, then itakuwa ni janga kubwa au italeta majanga makubwa na haina mfano, na inaweza kula kichwa au vichwa vya wahusika regardless hao wahusika ni kina nani!.

Naandika kwa kutuma ombi kwa rais Magufuli, kama akiingiwa na huruma na kifo cha huyu mama, na kama akiamua kumsamehe Eric Kabendera na kumwachia huru, anaweza ku reverse the impending karma, hii itapunguza tuu makali ya karma ya kifo cha huyu mama, ambaye kabla ya kifo chake, alimlilia Magufuli.


Kilio kama hiki cha huyu mama kumlilia mwanae na kumuombea msamaha, is not a small thing, kama kuna watu wa karibu na JPM wanaojua karma ni nini, wamfikishie kilio hiki, maana if anything happens to huyu mama kutokana na kukamatwa kwa mwanae, the consequences would be bad kwasababu karma haijui nani ni nani, au labda huyu ni rais, when karma hits back, it just hits!.

Kama rais Magufuli ameweza kuwasamehe watu waliokutwa na hatia ya kubaka na kuthibitishwa na mahakama na wakahukumiwa vifungo na akawasamehe, kuna watu waliokutwa na hatia ya kuua, wakathibitishwa na mahakama wakahukumiwa vifungo lakini rais Magufuli akawasamehe, atashindwaje kumsamehe Kabendera?.

Kama rais Magufuli ameweza kuwasamehe watuhumiwa wa ufisadi, uhujumu na utakatishaji fedha, na sasa hivi tunavyo zungumza tuko nao huru huku mitaani, then rais Magufuli, ikimwingia huruma kuhusu Eric Kabendera, Rais Magufuli akiamua, anaweza!.

Mimi na Eric Kabendera
Nimetokea kumfahamu Eric Kabendera miaka mingi nyuma kama mmoja wa waandishi mahiri kabisa kutokea hapa nyumbani Tanzania.

Ili mtu kuwa mwandishi mahiri, sio suala tuu la kujua kusoma na kuandika, bali unahitaji kuwa na brain yenye intelligence fulani ambayo kiukweli hapa Tanzania tuna waandishi wachache wenye intelligence ya kiwango cha Eric Kabendera, na mimi niko very proud kusema kuwa niliingia fani ya uandishi baada ya kupasi vizuri masomo yangu shule ya sekondari ya Tambaza na Ilboru, ndipo nikasomea uandishi wa habari na hata baada ya kuwa mwandishi wa habari bado nilijiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kusomea sheria LL.B na kuhitimu with honours, wale wanaijua sheria ya UDSM halafu ukasikia mtu ametoka with honours, mtaelewa, lengo sio kutambia honours ya sheria, bali kuwajulisha kuwa kuna watu tumeamua kuwa waandishi wa habari sio kwasababu ni vilaza bali kwa upenzi wa fani hii, hivyo Eric Kabendera ni miongoni mwa waandishi vichwa vya ukweli.

Kuna siku mimi nilikuwa moderator wa panel ya mjadala kuhusu "freedom of expression in Tanzania ya sasa"

On the 12th of July 2017 at Serena, JamiiForums in collaboration with The Collaboration on International ICT Policy in East and Southern Africa (CIPESA) hosted a stakeholder’s event with the theme ‘Engagement on Intermediary Liability and Data Protection’.

The conference was assessing the roles of the intermediaries and how they could effectively protect the customer’s valuable data (intermediaries such as Mobile Companies, JamiiForums, ISP etc). This session was hosted by Pacal Mayalla of a panel consisting of Erick Kabendera, Irene Kiwia, Carol Ndosi and Jebra Kambole.

View attachment 1172992
From Left, Erick Kabendera, Irene Kiwia, Paschal Mayalla, Adv. Jebra Kambole and Carol Ndosi

#FreeErickKabendera #ErickKabendera #FreedomOf Expression
Kuna maneno mazito sana Eric Kabendera aliyaongea kuhusu Freedom of expression,

2131026_A68707B3-962E-4066-8A0E-2D1515E73FBB.jpeg

Kwenye picha hapo, mimi ndio moderator wa huo mjadala wa Kwanza Kulia ni Eric Kabendera.

Tuhuma za Kumchongea Eric Kabendera
Kwanza naomba kukiri kuwa ni kweli mimi ndiye nilikuwa naleta makala za majarida mbalimbali ya nje yanasema nini kuhusu Tanzania humu jf. Wakati naleta makala hizo, kwanza sikuwahi kufahamu waandishi wake, wala hadi sasa ninapoandika hapo sina uhakika waandishi wa makala hizo ni kina nani, hivyo hakuna any direct linkage ya makala zangu na kukamatwa kwa Eric Kabendera, hivyo nawaomba sana wazushaji wa humu msinizushie. Ila kama ni kweli Erick amekamatwa kwa sababu ya kazi ya kalamu yake, na kama mimi nisinge tafsiri kwa Kiswahili, viongozi wetu vilaza wa kizungu wasinge jua, then na mimi I have my karma payback to pay, for my role.

Msamaha kwa Eric Kabendera, ninao muombea hapa, is purely on Humanitarian Grounds and not on criminal liabilities.
Nimejitokeza kumuombea Eric Kabendera asamehewe on Humanitarian grounds kufuatia kilio cha Mama yake kumuombea msamaha mwanae, hadi huyu mama amekufa na kinyongo, hivyo nimeguswa na kuumizwa na kilichomtokea Eric Kabendera kama mwandishi mwenzangu hivyo ombi hili kwa rais Magufuli ni kumsamehe tuu kama alivyo wasamehe hao wengine.

Why Kabendera and What's So Special About Him.
Kama nilivyoeleza hapo juu mimi nimesoma sheria hivyo nafahamu taratibu zote za mashitaka ya kijinai, mamlaka ya rais ni yapi kisheria na mwenye mamlaka ya kufanya kitu ni DPP, lakini maombi haya nayatuma kwa rais Magufuli kwa sababu fulani.
Japo kuna mahabusu wengi na mashitaka mengi ila issue ya Eric Kabendera tangu kukanatwa kwake, taarifa za polisi kujikanganya mara ahojiwe kuhusu uraia na kisha ndipo yakaibuka hayo mashitaka kunaleta mashaka fulani kwa sisi waandishi critical kwa sababu ambazo naomba nisiziseme hapa ila naamini kwa wajuzi wa hizi mambo wanazielewa na wana nielewa.

Hoja za Kisheria za Eric Kabendera Kuruhusiwa Kumzika Mama Yake

MAHAKAMA YAOMBWA KABENDERA KUMUAGA MAMAKE

HOJA SITA ZA UPANDE WA UTETEZI KWANINI KABENDERA APEWE RUHUSA KUSHIRIKI MAZIKO YA MAMA YAKE

Jopo la mawakili wa Mwandishi wa habari wa kujitegemea Erick Kabendera, wakiongozwa na Wakili Jebra Kambole wamewasilisha hoja sita mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Kisutu Janet Mtega kwa mshitakiwa kupatiwa ruhusa chini ya ulinzi ili aweze kushiriki Katika maziko au kutoa heshima za mwisho kwa mama yake aliyefariki hivi karibuni.

1. Kutoa heshima za mwisho ni haki ya msingi ya binadamu. Wakili ameeleza kuwa Kabendera ana haki ya kuwa na kuheshimu familia pamoja na haki ya faragha hivyo kuna umuhimu kwa Kabendera kushiriki Katika kutoa heshima za mwisho kwa mama yake.

2. Erick Kabendera anatakiwa adhaniwe kuwa hajatenda kosa mpaka pale mahakama itakapothibitisha kuwa ametenda kosa na kumzuia kushiriki mazishi itakuwa ni adhabu ya Kinyama kwa Kabendera.

3. Tangu Mshitakiwa amekamatwa hajaonesha nia ya kutoroka au kutaka kufanya vurugu hivyo hakuna uwezekano wa mtuhumiwa kutoroka Kama atapatiwa ruhusa

4. Mashitaka anayokabiliwa nayo mshitakiwa hayahusiani na uvunjifu wa amani hivyo Mahakama itilie maanani ombi Hilo

5. Kama Mahakama ilitoa amri aende mahabusu hivyo Mahakama Ina uwezo wa kuamua ombi hilo kwani kama mshitakiwa pia aliweza kupelekwa mahakamani haitashindikana kumpeleka kanisani kumuaga mama yake.

6. Ruhusa ya Kabendera kuhudhuria mazishi Jamhuri haiwezi kuathirika
Namalizia kwa kusisitiza karma is real na haina mswalie Mtume.
Natoa Pole sana Eric Kabendera
Mungu akufariji na Mungu akupiganie
Na kumuomba rais wetu Magufuli aguswe na madhila anayopitia huyu mwandishi wa habari mwenzetu Eric Kabendera.

Nawatakia Mwaka Mpya Mwema.

Paskali.
Rejea.
Kwa faida kwa wasio nijua, hii sio mara yangu ya kwanza kumuombea msamaha mhalifu au mahamubusu, nimewaombea msamaha wengi kwenye nyuzi hizi
Kifo Cha Kanumba: Ni Uzembe Tuu? Sio Lulu!

Political Capitalization: Kufuatia Kupendwa na Wengi na Kumhurumia, Jee Tumuombee Msamaha wa Rais, ili Aachiwe Huru?.

Hukumu ya Lulu Gerezani Imesaidia Wengi, Imesaidia Mengi!, Babu Seya Nje, TV Hadi Magerezani, Mazuri Mengi Zaidi Yaja!.

Mhe.Kaimu Jaji Mkuu, Prof. Ibrahim Juma, Naomba Usiruhusu Udhalilishaji Huu Ndani ya Mahakama Zetu!.
 
Ila kila mtu ataonja mauti.

Hii haina tofauti na mgonjwa anahitaji chakula na hapo hapo unakila chakula hicho na yeye anakufa.
so sad.

Hata akifanya hivyo ni aibu, aache hivyo hivyo.

Ni sawa na mtu anaumwa hapewi dawa wala matibabu, ila akifa ndiyo matarumbeta, makamera , maturubahi nk.
 
Kaka Paskali vipi? Unasema unamfahamu vizuri mwandishi Kabendera kama mwadishi wa habari halafu unaongelea kwa kirefu wasifu wako mpaka kufikia kuwa mwandishi wa habari huku ukiacha kuelezea kiundani wasifu wa Kabendera kama mwandishi wa habari.
 
Back
Top Bottom