Elections 2010 Baada ya hatihati, Chadema yapendekeza wagombea viti maalum

Mtu wa Pwani

JF-Expert Member
Dec 26, 2006
4,184
671
viti maalum Chadema vyazidi kupasua kichwa Send to a friend Saturday, 25 September 2010 22:38 0diggsdigg

_dk%20wilbord%20slaa.jpg
Mgombea Urais kwa tiketi ya Chadema,Dk Wilbrod Slaa

Fredy Azzah na Frederick Katulanda, Mwanza
MKUTANO Chadema, uliotishwa kuwateua wabunge wa viti maalumu, uliingia dosari baada ya kumalizika bila mwafaka kutokana na kuibuka makundi mawili yanayopingana.
Mkutano huo ulishindwa kumaliza ajenda zake baada ya makundi hayo kushindwa kufikia njia sahihi ya kuwapata wabunge wa viti maalumu vya wanawake.
Vyanzo vya habari kutoka ndani ya mkutano huo, vililidokeza gazeti hili kuwa makundi mawili yanayovutana yaliibuka kwenye kikao hicho na kukifanya kipoteze mwelekeo.

Makundi hayo yalidaiwa kuegemea vigogo wawili wazito ndani ya chama hicho, jambo ambalo liliipasua pia meza kuu na kuiweka katika mazingira magumu katika kuokoa jahazi.

Ingawa watu wanaodhani kuwa katika makundi hayo hawakutaka kuzungumza, habari zilidokeza kuwa mmoja wa viongozi wa juu wa Chadema (jina tunalo), alitaka elimu kiwe kigezo cha kuwapata wabunge hao wateule.

“Yeye anakazania kigezo cha elimu kitumike katika kuwapata wabunge,na anafanya hivyo kwa sababu kuna watu wake anaotaka waingie,” kilisema chanzo kimoja na kufafanua:

“Watu wengi wanataka utumike mfumo utakao wezesha kupata uwakilishi kutoka katika mikoa yote ili ile dhana ya kuwa Chadema viongozi wake wanatoka Kaskazini ifutike,”.
Chanzo kingine kutoka ndani ya mkutano huo kilisema, baadhi ya wajumbe walipinga njia ya kupiga kura kutafuta wabunge hao kutokana na kile kilichoelezwa kuwa kinaweza kurudisha makundi yaliyokuwa tayari yamevunjwa.
“Wanasema yatarudi yale makundi ya kina-Zitto na Mbowe kwa hiyo hawataki hiyo njia ya kupiga kura, kwa hiyo ngoma imelala mpaka kesho tena,” kilisema chanzo kingine.
Habari zimeeleza kuwa vingezo vingine vya kuwapata wabunge hao ambavyo viliibua makundi katika mkutano huo ni kuangalia uzoefu na juhudi za mtu katika kujitoa kukitumikia chama.

Baadhi ya wajumbe waliokuwa katika mkutano huo ambao pia ni wagombea wa kinyanganyiro hicho walisema, kuna watu ambao wameshaandaliwa ili kutimiza vigezo hivyo.
“Wameshawaandaa watu wao katika hizi siku za karibuni wamekuwa wakiwapitisha pitisha mbele ili waonekane ni watu muhimu na wanaojitolea katika kukihudumia chama,” kilisema chanzo kingine.

Chanzo kiningine kilidai: “Kwa mfano kama tukishinda katika uchaguzi huu, ni baraza gani la mawaziri tutaunda la watu wasiyo na elimu, lazima tuhakikishe tunajenga watu watakaoweza kuiendesha hii nchi kwa siku za baadaye” .
Kaimu Katibu Mkuu wa Chadema , John Mnyika alikataa kuzungumzia kilichojadiliwa katika mkutano huo kwa madia kwamba leo ataizungumza na vyombo vya habari.

Hata hivyo, baadhi ya vigogo waliotoka meza kuu walioombwa kutotajwa gazetini walisema wameamua kuahirisha kikao hicho ili leo wajipange upya kupata mwafaka.
“Tumelaza ngoma mpaka kesho. Imeundwa timu maalumu ya ku-rank (kupanga) majina. Hakuna kura. Mzozo ulikuwa hapo wakati mjumbe kutoka Shinyanga alipinga vikali akitaka kura.”

Hata hivyo, habari zilizolifikia gazeti hili zinaelezwa kwamba timu hiyo iliundwa na kuanza kuyapitia majina hayo ili kunusuru chama hicho ambacho kimeonekana kutoa upinzani mkali kwa CCM katika uchaguzi wa mwaka huu.

Hii ni mara ya pili kufanyika kwa mkutano wa viongozi wa Chadema kujadili kupata wagombea wa wabunge viti maalumu baada ya kile cha kwanza kuvunjika kutokana na wajumbe kushindwa kuelewana.

Wakati hayo yakiendelea makao makuu ya chama hicho jijini Dar es Salaam, mgombea ubunge wa chama hicho jimbo la Nyamagana Ezekiel Wenje, ameonja adha ya mkono wa dola baada ya kutiwa mbaroni na polisi na kuohojiwa kwa saa kadhaa.

Habari zimeeleza kuwa mgombea huyo wa ubunge ambaye hivi karibuni alinusurika kuenguliwa baada ya kuwekewa pingamizi na mgombea ubunge wa CCM, Lawrence Masha, alikamatwa juzi jioni wakati akizungumza na wananchi katika mtaa wa Kamanga jirani na Ikulu ndogo jijini Mwanza.

Wenje ambaye akiwa ameongozana na wapambe wake kumi, alikuwa akipita katika mitaa mbalimbali ya kati kati ya Jiji la Mwanza akitokea mitaa ya Sokoni.

Lakini alipokuwa amefika mitaani maarufu ya Makoroboi, alijikuta akianza kuzungukwa na watu wengi ambao walimfuata uku wakipiga miruzi na wengine kutoa maneno ya kejeli dhidi ya CCM.

Matembezi hayo yalianza majira ya saa 9:30 alasiri na kuhitimishwa na jeshi la polisi majira ya saa 11:17 baada ya maofisa hao wa polisi kumfuata na kumweka chini ya ulinzi.

“Kutoka hapa nilipo ni umbali wa mita 100 sasa sidhani kama inafaa kwenda kwa gari. Nitatembea hadi hapo kituoni.” Wenje aliwaeleza polisi hao ambao walitaka apande kwenye gari lao.

Wakati anaelekea kituoni kundi kubwa la watu liliendelea kumfuata jambo ambalo liliwafanya polisi hao kumbeba Wenje na kumwingiza kwenye gari lao kisha kuwaamuru wapambe hao kurudi.

“Kumkamata na kumweka katika gari ni matumizi ya nguvu, lakini hajaonyesha kukaidi na anakwenda vizuri kituoni. Hawa wafuasi wake watarudi tu,” alieleza mmoja wa mapambe hao.

Baada ya kumfikisha kituo cha polisi cha kati, mvutano mwingine uliibuka walipotaka kumweka ndani.

Lakini baadaye walikubaliana atoe maelezo ya kwanini alifanya mkutano nje ya utaratibu na ratiba za kampeni za uchaguzi.

Wenje aliliambia gazeti hili baada ya kuachiwa Wenje alisema: “Nilipofika kituoni walikuwa wakibishana (polisi). Wengine walidai wakiniweka ndani watazua vurugu na wengine wakidai kuwa hakuna sababu ya msingi ya kuniweka ndani kisheria, baadaye waakaniachia huru".

Kaimu Kamanda wa jeshi la polisi Nonosius Komba alipoulizwa kuhusu suala hilo alisema hana taarifa za kukamatwa kwa mgombea huyo.



source mwananchi
 
kwenye chama makini lazima mambo kama haya yatokee na sio uchakachuaji kwama tulivyoona kwa wenzetu haya ni yakawaida saaaana yata pita na tutasonga mbele tukiwa wamoja
 
kwenye chama makini lazima mambo kama haya yatokee na sio uchakachuaji kwama tulivyoona kwa wenzetu haya ni yakawaida saaaana yata pita na tutasonga mbele tukiwa wamoja

Kwenye chama makini ufisadi lazima uwepo. Ndiyo maana yule Mwenyekiti kakopa mamillioni NSSF halafu hataki kuyarudisha. :becky:
 
Kwenye chama makini ufisadi lazima uwepo. Ndiyo maana yule Mwenyekiti kakopa mamillioni NSSF halafu hataki kuyarudisha. :becky:
Tangu lini kukopa ikawa ufisadi?Kwani hao waliokopwa- ambao unadai wamefisadiwa- hawana debt collectors au taratibu za kukusanya madeni?Hebu nikudadisi ndugu yangu mwenye busara za kichwa panzi,nani fisadi kati ya mtu aliyekopa kisha mkopeshaji akazembea kudai deni husika AU mkopeshaji anayekopesha fedha zisizo zake,bila idhini ya wenye fedha hizo,hafuatilii madeni,na siku wenye fedha wanapokuja kuchukua mafao yao wazungushwa kana kwamba wanaomba mikopo,na kibaya zaidi malipo yenyewe hayaendani na michango yako?

Dont tell us hapo ulipo huna deni hata moja unless nawe ni fisadi.Tunaowaita mafisadi hawasaini mikataba na umma kuwa watarejesha fedha wanazoazima (Fisadi Kikwete alijaribu mbinu hiyo na kuwazuga Watanzania kuwa mafisadi wamepewa muda warejeshe walichoiba).Na ufisadi ni pale mwenye mali anapozembea kufuatilia chake hata kama ana uwezo wa kufanya hivyo.Tuna takukuru,polisi,usalama wa mafisadi...ooops,I meant usalama wa taifa,nk lakini hadi leo kagoda imebaki muujiza na mafisadi wa EPA bado wanatesa.
 
Chadema waelewe mshika mawili mmoja humponyoka wanachotakiwa hivi sasa ni kupata ushindi wa uchaguzi mkuu baada ya hapo watajua wanagombea viti vingapi maalumu. nguvu nyingi ikipotea kwenye viti maalumu italeta migawanyiko isiyo ya lazima wakati hata mzoga bado haujauliwa na kuwekwa mezani
 
KUDADEKI
mwenyekiti ni mfanyabiashara makini sana,
Amekopa NSSF ili akiletewa Zengwe la kibiashara na uongozi uliopo madarakani hasara itakuwa kwa nssf then itakuwa kwa wananchi then itabakfire kwa uongozi uliomletea zengwe,si kama hakuweza kukopa sehemu nyingine,na isitoshe mbona kuwa Quality Plaza wao walikopa wapi? :))
Kwenye chama makini ufisadi lazima uwepo. Ndiyo maana yule Mwenyekiti kakopa mamillioni NSSF halafu hataki kuyarudisha. :becky:
 
viti maalum Chadema vyazidi kupasua kichwa Send to a friend Saturday, 25 September 2010 22:38 0diggsdigg

_dk%20wilbord%20slaa.jpg
Mgombea Urais kwa tiketi ya Chadema,Dk Wilbrod Slaa

Fredy Azzah na Frederick Katulanda, Mwanza
MKUTANO Chadema, uliotishwa kuwateua wabunge wa viti maalumu, uliingia dosari baada ya kumalizika bila mwafaka kutokana na kuibuka makundi mawili yanayopingana.
Mkutano huo ulishindwa kumaliza ajenda zake baada ya makundi hayo kushindwa kufikia njia sahihi ya kuwapata wabunge wa viti maalumu vya wanawake.
Vyanzo vya habari kutoka ndani ya mkutano huo, vililidokeza gazeti hili kuwa makundi mawili yanayovutana yaliibuka kwenye kikao hicho na kukifanya kipoteze mwelekeo.

Makundi hayo yalidaiwa kuegemea vigogo wawili wazito ndani ya chama hicho, jambo ambalo liliipasua pia meza kuu na kuiweka katika mazingira magumu katika kuokoa jahazi.

Ingawa watu wanaodhani kuwa katika makundi hayo hawakutaka kuzungumza, habari zilidokeza kuwa mmoja wa viongozi wa juu wa Chadema (jina tunalo), alitaka elimu kiwe kigezo cha kuwapata wabunge hao wateule.

“Yeye anakazania kigezo cha elimu kitumike katika kuwapata wabunge,na anafanya hivyo kwa sababu kuna watu wake anaotaka waingie,” kilisema chanzo kimoja na kufafanua:

“Watu wengi wanataka utumike mfumo utakao wezesha kupata uwakilishi kutoka katika mikoa yote ili ile dhana ya kuwa Chadema viongozi wake wanatoka Kaskazini ifutike,”.
Chanzo kingine kutoka ndani ya mkutano huo kilisema, baadhi ya wajumbe walipinga njia ya kupiga kura kutafuta wabunge hao kutokana na kile kilichoelezwa kuwa kinaweza kurudisha makundi yaliyokuwa tayari yamevunjwa.
“Wanasema yatarudi yale makundi ya kina-Zitto na Mbowe kwa hiyo hawataki hiyo njia ya kupiga kura, kwa hiyo ngoma imelala mpaka kesho tena,” kilisema chanzo kingine.
Habari zimeeleza kuwa vingezo vingine vya kuwapata wabunge hao ambavyo viliibua makundi katika mkutano huo ni kuangalia uzoefu na juhudi za mtu katika kujitoa kukitumikia chama.

Baadhi ya wajumbe waliokuwa katika mkutano huo ambao pia ni wagombea wa kinyanganyiro hicho walisema, kuna watu ambao wameshaandaliwa ili kutimiza vigezo hivyo.
“Wameshawaandaa watu wao katika hizi siku za karibuni wamekuwa wakiwapitisha pitisha mbele ili waonekane ni watu muhimu na wanaojitolea katika kukihudumia chama,” kilisema chanzo kingine.

Chanzo kiningine kilidai: “Kwa mfano kama tukishinda katika uchaguzi huu, ni baraza gani la mawaziri tutaunda la watu wasiyo na elimu, lazima tuhakikishe tunajenga watu watakaoweza kuiendesha hii nchi kwa siku za baadaye” .
Kaimu Katibu Mkuu wa Chadema , John Mnyika alikataa kuzungumzia kilichojadiliwa katika mkutano huo kwa madia kwamba leo ataizungumza na vyombo vya habari.

Hata hivyo, baadhi ya vigogo waliotoka meza kuu walioombwa kutotajwa gazetini walisema wameamua kuahirisha kikao hicho ili leo wajipange upya kupata mwafaka.
“Tumelaza ngoma mpaka kesho. Imeundwa timu maalumu ya ku-rank (kupanga) majina. Hakuna kura. Mzozo ulikuwa hapo wakati mjumbe kutoka Shinyanga alipinga vikali akitaka kura.”

Hata hivyo, habari zilizolifikia gazeti hili zinaelezwa kwamba timu hiyo iliundwa na kuanza kuyapitia majina hayo ili kunusuru chama hicho ambacho kimeonekana kutoa upinzani mkali kwa CCM katika uchaguzi wa mwaka huu.

Hii ni mara ya pili kufanyika kwa mkutano wa viongozi wa Chadema kujadili kupata wagombea wa wabunge viti maalumu baada ya kile cha kwanza kuvunjika kutokana na wajumbe kushindwa kuelewana.

Wakati hayo yakiendelea makao makuu ya chama hicho jijini Dar es Salaam, mgombea ubunge wa chama hicho jimbo la Nyamagana Ezekiel Wenje, ameonja adha ya mkono wa dola baada ya kutiwa mbaroni na polisi na kuohojiwa kwa saa kadhaa.

Habari zimeeleza kuwa mgombea huyo wa ubunge ambaye hivi karibuni alinusurika kuenguliwa baada ya kuwekewa pingamizi na mgombea ubunge wa CCM, Lawrence Masha, alikamatwa juzi jioni wakati akizungumza na wananchi katika mtaa wa Kamanga jirani na Ikulu ndogo jijini Mwanza.

Wenje ambaye akiwa ameongozana na wapambe wake kumi, alikuwa akipita katika mitaa mbalimbali ya kati kati ya Jiji la Mwanza akitokea mitaa ya Sokoni.

Lakini alipokuwa amefika mitaani maarufu ya Makoroboi, alijikuta akianza kuzungukwa na watu wengi ambao walimfuata uku wakipiga miruzi na wengine kutoa maneno ya kejeli dhidi ya CCM.

Matembezi hayo yalianza majira ya saa 9:30 alasiri na kuhitimishwa na jeshi la polisi majira ya saa 11:17 baada ya maofisa hao wa polisi kumfuata na kumweka chini ya ulinzi.

“Kutoka hapa nilipo ni umbali wa mita 100 sasa sidhani kama inafaa kwenda kwa gari. Nitatembea hadi hapo kituoni.” Wenje aliwaeleza polisi hao ambao walitaka apande kwenye gari lao.

Wakati anaelekea kituoni kundi kubwa la watu liliendelea kumfuata jambo ambalo liliwafanya polisi hao kumbeba Wenje na kumwingiza kwenye gari lao kisha kuwaamuru wapambe hao kurudi.

“Kumkamata na kumweka katika gari ni matumizi ya nguvu, lakini hajaonyesha kukaidi na anakwenda vizuri kituoni. Hawa wafuasi wake watarudi tu,” alieleza mmoja wa mapambe hao.

Baada ya kumfikisha kituo cha polisi cha kati, mvutano mwingine uliibuka walipotaka kumweka ndani.

Lakini baadaye walikubaliana atoe maelezo ya kwanini alifanya mkutano nje ya utaratibu na ratiba za kampeni za uchaguzi.

Wenje aliliambia gazeti hili baada ya kuachiwa Wenje alisema: “Nilipofika kituoni walikuwa wakibishana (polisi). Wengine walidai wakiniweka ndani watazua vurugu na wengine wakidai kuwa hakuna sababu ya msingi ya kuniweka ndani kisheria, baadaye waakaniachia huru".

Kaimu Kamanda wa jeshi la polisi Nonosius Komba alipoulizwa kuhusu suala hilo alisema hana taarifa za kukamatwa kwa mgombea huyo.



source mwananchi

Umekwenda Msikitini leo?
 
Ni kweli kabisa

tena hili lilileta mgogohata pale mkutanoni pta

hawakua makini


lakini siku zote viti maalum ni balaa, tumesahau mama kahama alivyodhalilishwa na sofia?
 
HTML:
[[FONT=Comic Sans MS][SIZE=4][COLOR=blue]Wengine walidai wakiniweka ndani watazua vurugu na wengine wakidai kuwa hakuna sababu ya msingi ya kuniweka ndani kisheria, baadaye waakaniachia huru[/COLOR][/SIZE][/FONT]".
/HTML]
[/QUOTE]kidogo kidogo POLICE wanaanza kujitambua, mwanzo wa ukungu kuondoka machoni mwao kuwa wao si waajiliwa wa ccm , bali ni watumishi wa UMMA, dalili ya kuanza kutofautiana juu ya maswala ya msingi ni dalili njema juu ya haki ya msingi ya Ushiriki wa mapolisi katika kuing'oa ccm manyoya madarakani.
 
Kwenye chama makini ufisadi lazima uwepo. Ndiyo maana yule Mwenyekiti kakopa mamillioni NSSF halafu hataki kuyarudisha. :becky:

Hapo kama ungekuwa karibu umeshaklula za macho ambazo hazina idadi, unawagusa wasotaka kuguswa hata kama wanagusika kaka.Watakwambia deni halifungi.
 
hili nalo linawasumbua

hawa mahtuti hawaji tena juu na baada ya uchaguzi na chama wanavunja hawa
 
Hatimaye Chadema imepitisha majina ya wabunge 105 wa viti maalumu huku ikiwaacha
wanachama wake 42 walioshindwa kukidhi vigezo vya chama hicho.

Majina ya wabunge hao hayakuwekwa hadharani na badala yake yatapelekwa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kabla ya Septemba 30 mwaka huu.

Uteuzi wa majina hayo ulifanywa na mshauri kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Dk. Mkumbo Kitila, ambaye ni mwanachama wa chama hicho na kuthibitishwa na Kamati Kuu katika kikao chake cha Septemba 25 na 26 jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na waandishi wa habari leo, Katibu Mkuu wa Chadema ambaye pia mgombea urais, Dk. Willibrod Slaa, alisema baada ya matokeo ya wabunge hao ya Julai kufutwa kutokana na mizengwe, Baraza Kuu lilikasimu madaraka kwa Kamati Kuu kufanya uteuzi huo.

“Kamati Kuu ikaunda Kamati Ndogo ambayo ilimtumia mshauri kufanya uteuzi huo akizingatia vigezo vya elimu, uzoefu wa uongozi kisiasa, uzoefu wa uongozi nje ya siasa; ugombea jimboni mwaka huu; mchango katika operesheni za chama na kampeni zinazoendelea na umri ndani ya chama,” alisema Slaa.

Katika vigezo hivyo, aliyeongoza alipata asilimia 94 na wa mwisho 16 ambapo moja ya sababu za kutumika utaratibu huo ambao Dk. Slaa aliuita wa kisayansi, ni kuondoa uswahiba, wagombea kutoka kanda moja na urafiki.

“Tumeondoa dhana ya mtu kuchagua ‘girlfriend (rafiki wa kike)’ wake, na majina haya hatutayatoa hadharani, kwani wengine waliopitishwa wanagombea majimboni,
hivyo kunaweza kuwachanganya wapiga kura,”
alifafanua.

Dk. Kitila alisema katika uandaaji wa vigezo, waliangalia suala la umahiri wa mgombea na kwambambunge atakuwa anawakilisha nchi na kupanua wigo wa ushiriki wa wanawake.

Katika Bunge lililopita, wabunge wa Chadema walikuwa 11 wakiwamo wa majimbo na viti
maalumu na mwaka huu imesimamisha wabunge wa majimbo 185.
 
Back
Top Bottom