Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,903
- 945
MHE. ENG. AISHA ULENGE, Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Tanga Akizungumza katika Mkutano wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Geneva Uswissi.
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Tanga, Mhandisi Mwanaisha Ulenge ameshiriki katika Mkutano wa 148 wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU) unaofanyika jijini Geneva Switzerland.
Katika Mkutano huo, Mhandisi Ulenge ameshiriki pia mikutano ya Umoja wa nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara (SADC) na Jukwaa la Afrika vikao ambavyo vimeangazia mambo ya dharura yanayohitajika kujadiliwa katika Mkutano wa Dunia unaojadili Diplomasia ya Bunge kupelekea kujenga Amani na Maelewano.
Pia, Mhandisi Ulenge ameshiriki katika majukwaa ya wabunge Wanawake na vijana ambapo amepata nafasi ya kuchangia mada za Mkutano huo kuhusu mifumo ya usalama na Amani.