Asilimia 90 ya watanzania tumeshagundua kwamba hawa viongozi wamehongwa kwa ajili ya bandari

Rushwa ni kitu kibaya sana na ndo kitu kinachoumiza hii nchi. Rushwa haifai hata kidogo.
Kwa kweli rushwa haifai. Si unaona baada ya kuwa Mbowe, NSHALLA, Lissu, Mwabukusi na Kitima wamepewa rushwa si waliharibu mjadala wa bandari na kuanza kuongelea uzanzibar wa rais na waziri Mbarawa na Uarabu wa akina DP WORLD mpaka watu wakahamia kwenye hayo mambo na hoja ya msingi ikaachwa? Rushwa ina madhara makubwa sana.
 
Habari zenu wanaJF wenzangu,

Ndugu zangu,,, hapa nchini kwetu ukiwa mtu makini, mwenyekujitambua, mwenye uwezo wa kudhibiti mihemko, mwenye mawazo na akili iliyohuru bila kukontroliwa na mtu mungine ambae ataitumia akili yako kwa faida yake na familia yake huku akikuacha wewe ukidhalilika, ukiwa mwenye kutafakari kwa kina juu ya mstakabali wa nchi na future za wananchi, hakika utaweza kuona madudu mengi yaliojificha nyuma ya migongo ya viongozi wenye njaa. Kuona huko kunaweza kufanikiwa kupitia historia zao, maneno yao, na vitendo vyao.

Fikiria kiongozi mkubwa wa chama cha siasa anafika Kariakoo, badala ya kuwaeleza watu sera za chama chake, badala ya kuwaeleza watu namna watakavyofaidika, au taifa litakavyosonga mbele kimaendeleo na huduma bora kwa wananchi kutokana na sera hizo endapo chama chake au chao kitafanikiwa kushika dola.

Yeye anakuja na upepo wa bandari kwa kuwaeleza watu maneno mawili matatu ya kuuponda mkataba wa bandari bila kuonesha sehemu anayodai kuwa haifai, baada ya hapo anaanza kuomba michango na baadae akishachangiwa chake anatokomea anapokujua yeye kununua nyama, mchele, mafuta na mahitaji mengine ya lazima huku waliomchangia wengi wao wakienda kula dagaa na ugali usiku ule.

Sasa mtu mwenye akili unajiuliza kama mtu ana njaa hadi anaamua kuwakamua wale anaodai kwamba anawasaidia, je atashindwa kupokea hongo atakayohongwa na kundi lenye lengo la kumtumia kupush ajenda zao mbele.

Kama anachukua hadi elfu ya masikini muuza pilipili wa Kariakoo atawezaje kukataa milioni 1 au 2 ya wale wapitisha madawa ya kulevya bandarini, wezi wa vifaa vya magari na mizigo mbali mbali bandarini, wakwepa kodi na ushuru wa bandarini?

Jibu utapata kwamba jamaa amehongwa ili awapambanie waliomuhonga, na hizo za Kariakoo anazitumia kununua mahitaji yake ya siku. Ndio maana tunasema hawa viongozi wanapambana kwa sababu ya njaa zao na wakishapata chao wanatokomea kula na familia zao. Mnaosubiri kupata maendeleo kupitia viongozi hawa, hamna tofauti na mtu anaesubiri nazi ianguke kutoka juu ya mkungu.
Tatizo kubwa la afrika na la miaka mingi ni wananchi wa kawaida kabisa kuwaamini wanasiasa na kuwapa kila chembe ya uelewa wao.

Wanawaamini kwa kutumia uzoefu wao walioupata kwa wachache kati yao na kudhani kwamba wanasiasa wote wana hulka moja ya ukweli mioyoni mwao.

Mpaka siku wakija kugundua kwamba wametapeliwa tayari wameshaumizwa. Suala la bandari haswa hiyo mikataba ni danganya toto ya wanasiasa, huwa wanavisoma vifungu viwili vitatu bila ya kuusoma mkataba mzima wenye vifungu 30.

Na hii ni janja ya hao hao wapigaji wa bandarini, kuwatumia watu wenye ushawishi na heshima miongoni mwetu ili eti tukizipinga hoja za hao wanazuoni ionekane kama vile ni dhambi ya mauti kwa nafasi zao mbele ya jamii!.

Hii ni vita nzito ya kiuchumi, wale wenye kuelewa nini anakuja kufanya DPW pale bandarini na katika uchumi kwa ujumla na tusikae kimya tukaacha upotoshaji wenye lengo la kuwalinda wapigaji ukaendelea kuheshimiwa na kukubalika.
 
Kwa kweli rushwa haifai. Si unaona baada ya kuwa Mbowe, NSHALLA, Lissu, Mwabukusi na Kitima wamepewa rushwa si waliharibu mjadala wa bandari na kuanza kuongelea uzanzibar wa rais na waziri Mbarawa na Uarabu wa akina DP WORLD mpaka watu wakahamia kwenye hayo mambo na hoja ya msingi ikaachwa? Rushwa ina madhara makubwa sana.
Tumeshawashtukia hivyo kushindwa kwa hoja zao ni suala la muda tu.
 
wewe ndo unaakili au umeshikiwa
2008 Enyi misukule yetu tunawambieni Lowasa ni fisadi sasa andamaneni ili ajiuzulu, misukule mkaandamana kweli hadi Lowasa akajiuzulu.

2015 Lowasa akamwaga pesa...
Lowasa ni msafi na kamwe hakuwahi kuwa fisadi. Kwahiyo misukule yetu tunawaamrisha mumchague ili awe raisi wetu, na kweli siku ya kupiga kura ukamchagua Lowasa.

Sasa mpaka hapo unaweza kuona ni jinsi gani ulivyoshikiwa akili na wanasiasa uchwara. Unakubali vipi wanasiasa uchwara wakifanye kichwa chako ni chaka la kudanganyia na bado unaendelea kuwaona ni wakombozi kwako!!
 
Kwa kweli rushwa haifai. Si unaona baada ya kuwa Mbowe, NSHALLA, Lissu, Mwabukusi na Kitima wamepewa rushwa si waliharibu mjadala wa bandari na kuanza kuongelea uzanzibar wa rais na waziri Mbarawa na Uarabu wa akina DP WORLD mpaka watu wakahamia kwenye hayo mambo na hoja ya msingi ikaachwa? Rushwa ina madhara makubwa sana.
Bora Mbowe na lisu wanajulikana wazi kuwa ni wanasiasa uchwara wanaoishi kwa njia za uongo uongo, rushwa nk.

Sasa Mwabukusi na wenzake si wanajiaibisha tu bure na hadhi yao inashuka.
 
Tatizo kubwa la afrika na la miaka mingi ni wananchi wa kawaida kabisa kuwaamini wanasiasa na kuwapa kila chembe ya uelewa wao.

Wanawaamini kwa kutumia uzoefu wao walioupata kwa wachache kati yao na kudhani kwamba wanasiasa wote wana hulka moja ya ukweli mioyoni mwao.

Mpaka siku wakija kugundua kwamba wametapeliwa tayari wameshaumizwa. Suala la bandari haswa hiyo mikataba ni danganya toto ya wanasiasa, huwa wanavisoma vifungu viwili vitatu bila ya kuusoma mkataba mzima wenye vifungu 30.

Na hii ni janja ya hao hao wapigaji wa bandarini, kuwatumia watu wenye ushawishi na heshima miongoni mwetu ili eti tukizipinga hoja za hao wanazuoni ionekane kama vile ni dhambi ya mauti kwa nafasi zao mbele ya jamii!.

Hii ni vita nzito ya kiuchumi, wale wenye kuelewa nini anakuja kufanya DPW pale bandarini na katika uchumi kwa ujumla na tusikae kimya tukaacha upotoshaji wenye lengo la kuwalinda wapigaji ukaendelea kuheshimiwa na kukubalika.
Natamani wanaodanganywa na wanasiasa ili kuupinga mkataba wangepita hapa ili wajifunze kitu kupitia comment yako yenye hekima.
 
Huyo Mwabukusi ni mtu wa hovyo sana ndomana kadharauliwa na kila mwenye akili
WaTanganyika sio wajinga kama mnavyodhania! Waarabu wameshtuka hawataki tena kuja kupora Bandari zetu na sasa wanataka warudishiwe $$$ zao walizowahonga Samia na genge lake!!
Huo ndio mtihani alionao Samia kwani fedha walizohongwa wamezogawagawa kwa machawa wao hivyo hawajui watazirudishaje!
Ndio maana wanahangaika kuzunguka nchi nzima kuwarubuni wananchi ili hali waarabu wameshtuka wanataka warudishiwe hela zao!
 
WaTanganyika sio wajinga kama mnavyodhania! Waarabu wameshtuka hawataki tena kuja kupora Bandari zetu na sasa wanataka warudishiwe $$$ zao walizowahonga Samia na genge lake!!
Huo ndio mtihani alionao Samia kwani fedha walizohongwa wamezogawagawa kwa machawa wao hivyo hawajui watazirudishaje!
Ndio maana wanahangaika kuzunguka nchi nzima kuwarubuni wananchi ili hali waarabu wameshtuka wanataka warudishiwe hela zao!
Endelea kujitekenya na kuruka mwenyewe, wenye akili tunasubiri dp world waje kuanza kazi na wale wote waliokuwa wanatumia bandari yetu kupitishia madawa ya kulevya na kuja kuharibu nguvu kazi ya vijana wa kitanzania sasa watafute biashara zingine za halali wafanye.

Pia wale waliokuwa wanapitisha mizigo bandarini bila kulipa ushuru na kodi sasa kwisha habari zao. Wamejaribu kuwatumia wanasiasa uchwara na mawakili njaa wakifikiri labda serikali itawasikiliza. Kwa bahati serikali haina muda wa kuwasikiliza na wananchi ndo kabisa hatutaki kusikia porojo zao.

Wao waendelee kula hela za wakwepa kodi wa bandari ila wasifikiri kwamba serikali itaacha kuendelea na mipango yake na ukizingatia raisi Samia akiamua jambo huwa habadilishi. I hope unakumbuka swala la Loliondo ambapo Wakenya walitumia mamluki wao humu ila raisi hakurudi nyuma, operation ikaendelea kama kawa.
 
Back
Top Bottom