Sakata la Bandari: Sioni uwezekano wa Raisi Samia kupata asilimia 30 ya kura zote, na CCM kupata wabunge zaidi ya 100 mwaka 2025

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,018
144,377
Sakata la Bandari na kashifa nyingine zinaziendelea kuibuliwa kama hii ya kuwapa Waarabu hifadhi za misitu yetu na nyinginezo kama ya Ngorongo, zinakwenda kuimalliza vibaya CCM pamoja na mgombea wao wa uraisi ambae bila shaka atakuwa ni Mama Samia kwenye uchaguzi mkuu ujao wa 2025.

Kashifa hizi, mithili ya dhoruba kali baharini, zimekuja kuzamisha mtumbwi ambao teyari ulikuwa umetoboka na sasa unajaa maji(unazama).

Mama alikuwa teyari hakubaliki sana, na badala ya kufanya mambo ambayo yangemsaidia kukubalika, amefanya kinyume chake kupata hizi kashifa zinazoendelea kuibuliwa na wanasiasa wa upinzani, wanaharakati na watu wa makundi mengine katika jamiii mfano viongozi wa dini.

Ukiacha hayo, wafuasi wa Mwendazake ndani ya chama chake nao ni tatizo kwake. Hivyo, baadhi ya kura za wana-CCM, Mama atakwenda kugawan na wapinzani jambo litalokwenda kumuweka katika hali mbaya zaidi.

Sio Samia tu kama mgombea uraisi atakaeathirika(naamini atagombea), bali hata wagombea ubunge wa CCM nao wataathirika kwa kuridhia ule mkataba mbovu wa bandari.

Kama ambayo kashifa za wizi na ufisadi wakati wa Kikwete zilivyoigharimu CCM kwenye chaguzi za 2010 na 2015, ndivyo ambavyo kashifa hizi zinazoendelea zitakwenda kuigharimu vibaya zaidi CCM katika uchaguzi mkuu ujao wa mwaka 2025.

Hali ikiendelea hivi, itakuwa ni vigumu sana kwa Mama Samia kupata asilimia 30 ya kura zote na CCM kupata wabunge zaidi ya 100 kote bara na visiwani.

Najua hatuna tume huru ya uchaguzi na wala CCM hawatakubali tuwe na tume huru, lakini huo ndio utakuwa uhalisia katika uchaguzi ujao(makaratasi yatawapa uhalisia hata kama watatangaza tofauti).

Walioko hatarini zaidi ni wagombe ubunge ambao sometimes huwa ni vigumu kupindua matokeo labda kama Mama afanya kama alivyofanya Mwendake kuwa ni lazima watangazwe washindi ingawa hii inahitaji roho ngumu na elements za ukatili mambo ambayo Mama yanaweza kumshinda.

Time will tell.
 
Sakata la Bandari na kashifa nyingine zinaziendelea kuibuliwa kama hii ya kuwapa Waarabu hifadhi za misitu yetu na nyinginezo kama ya Ngorongo, zinakwenda kuimalliza vibaya CCM pamoja na mgombea...
Kwa wapiga kura hawa wa bongo na kwa katiba hii!?

Sana sana Mama atacama ushauri wa JK kuwapa wapinzani viti kadhaa bungeni tofauti na Mwendazake aliyekusudia kuua kabisa upinzani akafa yeye
 
Usikariri 😄😄
Fanya simple research huko mtaani uone namna hii kashifa ya bandari inavyomgharimu Mama.

Sasa hivi hata wale ambao mwanzoni walikuwa wanaona huu mkataba sio tatizo, wengi wao sasa hivi wamebadilka na wanakiri huu mkataba sio kabisa.

Binafsi kuna staff mwenzangu mwanzoni alikuwa upende wa wale waliokuwa wanaunga mkono huu mkataba, ila juzi alikuwa anaongea tofauti kabisa na ni baada ya kuendelea kusikua na kuona yanayoendelea kuhusu hii kashifa.
 
Sakata la Bandari na kashifa nyingine zinaziendelea kuibuliwa kama hii ya kuwapa Waarabu hifadhi za misitu yetu na nyinginezo kama ya Ngorongo, zinakwenda kuimalliza vibaya CCM pamoja na mgombea wao wa uraisi ambae bila shaka atakuwa ni Mama Samia kwenye uchaguzi mkuu ujao wa 2025...
2010 CCM nusura izame japo hakukuwa na kashfa nzito kama hii. Imeenda hiyo
 
Hivi wenzetu bado mna imani na chaguzi zetu? Kwa katiba na tume hii ya uchaguzi, ni ngumu sana wagombea wa kutotangazwa washindi bila kujali kura halali zinasemaje. Tutafute njia nyingine ya kuondokana na CCM, lakini sio kupoteza muda na hizo chaguzi za kishenzi.
 
Hivi wenzetu bado mna imani na chaguzi zetu? Kwa katiba na tume hii ya uchaguzi, ni ngumu sana wagombea wa kutotangazwa washindi bila kujali kura halali zinasemaje. Tutafute njia nyingine ya kuondokana na CCM, lakini sio kupoteza muda na hizo chaguzi za kishenzi.
Soma vizuri uelewe nilichosema. Watabadili matokeo lakini uhalisia wa kura utawapa majibu labda maboksi ya kura nayo yavurugwe kama walivyofanya 2020.
 
Soma vizuri uelewe nilichosema. Watabadili matokeo lakini uhalisia wa kura utawapa majibu labda maboksi ya kura nayo yavurugwe.
Uhalisia wa kura mara zote wanaujua ndio maana wanaendelea kupora chaguzi, na wala hawajali matokeo ya kweli. Machafuko ama mapinduzi ya kijeshi pekee ndio yatawatisha na ndio yatarejesha heshima ya box la kura.
 
Sakata la Bandari na kashifa nyingine zinaziendelea kuibuliwa kama hii ya kuwapa Waarabu hifadhi za misitu yetu na nyinginezo kama ya Ngorongo, zinakwenda kuimalliza vibaya CCM pamoja na mgombea wao wa uraisi ambae bila shaka atakuwa ni Mama Samia kwenye uchaguzi mkuu ujao wa 2025...
Watamtoa huyo, hatogombea, ndo mpango wao.
 
Back
Top Bottom