Frank Wanjiru
JF-Expert Member
- Apr 12, 2012
- 21,838
- 38,729
Edward Ngoyai Lowasa ameondoka. Yuko mahali salama pasipo na mgao wa umeme wala usanii wa treni za umeme. Amepumzika baada ya kazi ngumu. Anapokufa mtu mzito kama Lowassa, kuna makundi matatu hujitokeza;
1. Wanaolia
2. Wanaofurahia
3. Wasiojua kama walie au wafurahie.
Makundi yote matatu tunayo katika kifo cha Edward Lowasa. Mimi sijui nipo kundi gani lakini niseme mambo manne ninayokumbuka:
1. Dola yetu ina mihimili mitatu: Bunge, serikali na mahakama. Lakini Lowassa alisababisha kuzaliwa kwa mihimili mitatu ndani ya mhimili wa bunge:
2. Alikuwa mtetezi asiye na mtetezi. Alikitetea chama chake, kikamtelekeza. Alimtetea Rais wake akamsaliti. Aliitetea nchi lakini nchi ikawatetea watesi wake.
3. Aliwapenda Wamasai, lakini Watesi wake wakamchonganisha na Wamasai. Wakahoji umasai wake na kudai Lowassa ni Mmeru. Lakini upendo wake kwa Wamasai ukawa na nguvu kuliko fitina za watesi wake. Akiwa hai na akiwa maiti Edward amebaki kuwa Mmasai.
4. Alisalitiwa na wengi aliowasaidia. Baada ya kumtumia kwa maslahi yao na kumtelekeza alibaki na Regina. Tujifunze kujali familia zetu. Mwisho wa yote, mzigo unabebwa na familia. Mambo ya “Pengo halitazibika” ni ulaghai mtupu. Kufa uone watakavyoziba pengo hata kabla ya mazishi.
LOWASSA KATIKA UBINADAMU WAKE:
A. Aliwaamini watu kuliko walivyomuamini.
B. Aliuchukia umaskini kwa vitendo. Watesi wake wakatumia hoja hii kumchonganisha na wananchi maskini. Wakasahau kuwa hata maskini wanauchukia umaskini wao na wanatamani kutoka.
C. Aliamini uzalendo si umaskini. Unaweza kuwa tajiri na ukawa mzalendo.
D. Alitumikia vyama 2 vikubwa. Vikamchafua na kumsafisha. Vikambeza na kumtukuza. Ameondoka akiwa mshindi kwa vyama vyote viwili.
E. Ameishi duniani miaka 70. Lakini Historia yake ni ndefu kuliko miaka yake. Ni mfupi wa umri lakini mrefu wa historia. Nenda Edward. Pole kwa Mama Regina, Watoto na wajukuu.!
1. Wanaolia
2. Wanaofurahia
3. Wasiojua kama walie au wafurahie.
Makundi yote matatu tunayo katika kifo cha Edward Lowasa. Mimi sijui nipo kundi gani lakini niseme mambo manne ninayokumbuka:
1. Dola yetu ina mihimili mitatu: Bunge, serikali na mahakama. Lakini Lowassa alisababisha kuzaliwa kwa mihimili mitatu ndani ya mhimili wa bunge:
- Wa kwanza ni Spika Samwel Sitta
- Wa pili ni Wabunge mitume wakiongozwa na Mwakyembe
- Mhimili wa 3 ulikua Edward Lowasa mwenyewe.
2. Alikuwa mtetezi asiye na mtetezi. Alikitetea chama chake, kikamtelekeza. Alimtetea Rais wake akamsaliti. Aliitetea nchi lakini nchi ikawatetea watesi wake.
3. Aliwapenda Wamasai, lakini Watesi wake wakamchonganisha na Wamasai. Wakahoji umasai wake na kudai Lowassa ni Mmeru. Lakini upendo wake kwa Wamasai ukawa na nguvu kuliko fitina za watesi wake. Akiwa hai na akiwa maiti Edward amebaki kuwa Mmasai.
4. Alisalitiwa na wengi aliowasaidia. Baada ya kumtumia kwa maslahi yao na kumtelekeza alibaki na Regina. Tujifunze kujali familia zetu. Mwisho wa yote, mzigo unabebwa na familia. Mambo ya “Pengo halitazibika” ni ulaghai mtupu. Kufa uone watakavyoziba pengo hata kabla ya mazishi.
LOWASSA KATIKA UBINADAMU WAKE:
A. Aliwaamini watu kuliko walivyomuamini.
B. Aliuchukia umaskini kwa vitendo. Watesi wake wakatumia hoja hii kumchonganisha na wananchi maskini. Wakasahau kuwa hata maskini wanauchukia umaskini wao na wanatamani kutoka.
C. Aliamini uzalendo si umaskini. Unaweza kuwa tajiri na ukawa mzalendo.
D. Alitumikia vyama 2 vikubwa. Vikamchafua na kumsafisha. Vikambeza na kumtukuza. Ameondoka akiwa mshindi kwa vyama vyote viwili.
E. Ameishi duniani miaka 70. Lakini Historia yake ni ndefu kuliko miaka yake. Ni mfupi wa umri lakini mrefu wa historia. Nenda Edward. Pole kwa Mama Regina, Watoto na wajukuu.!