Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,173
Nimevipima vyama vya upinzani kwenye mizania yangu ya upembuzi yakinifu na kubaini bila ya mashaka yoyote yale bado havipo tayari kimfumo kutupatia Raisi bora na hizi ndizo nondo zangu zilizonifikisha hapo..:-
a) Vyama vyote vya upinzani vimeiga mfumo mbovu wa kidemokrasia wa ccm na vinaendeshwa kibabe-kibabe mno na huku wenzao wa ccm kuanzia 2010 walianza kujivua gamba la udikteta pale waliporuhusu wabunge wake wachaguliwe na wananchi moja kwa moja...ingawaje bado wana safari ndefu kwenye hili lakini lazima niwapongeze ccm kwa angalau kujaribu....rushwa na kuingiliwa na ngazi za juu katika maoni ya wananchi ni changamoto ambazo ccm itabidi waendelee kuzitafutia muarobaini wake.
Kwenye hili vyama vya upinzani wapo nyuma na tumeona hata chadema bila ya kupitisha kura ya maoni kwa wapigakura wa Arusha wakitumia kauli za kidikteta kukejeli kura za wanachama wao Arusha pale kamati kuu yao ilipotengua madiwani wakaidi wa Arusha...well, chadema worshippers...that was not democracy at all...it was dictatorship.........face it now before it is too late.....Only the truth will set you free
b) Vyama vyote vya siasa vyenye wabunge Bungeni vimekumbwa na dhoruba kali la wizi na ubadhirifu wa ruzuku ya hazina na hakuna uthibiti wa aina yoyote ile!!!!!
Kwa mtazamo wangu kama wapinzani wameshindwa hata kusimamia kidogo ambacho tumewapa ni kwa upuuzi upi utushawishi kuwakabidhi nchi yote?
Njaa ya viongozi wa upinzani ni kali kulikoni ya viongozi wa ccm ambao pamoja na bandubandu kweli humaliza gogo lakini ccm hawana uchu wa kututafuna kama upinzani walionao.....ccm vibosile wake wamekwisha shiba njaa siyo kali sana kwa kipimo cha malinganisho.................lol
c) Mchakato wa katiba mpya umenifungua macho hila na upofu wa wapinzani ambao waliipinga tume kwa vile wao hawajaweka mrija wao ndani yake na kunyonya Hazina baada ya CCM kuwaingiza kingi - au niseme mkenge? - hakuna anayehoji uhalali wa Tume ya kukusanya maoni.
Wote wanaimba wimbo wa CCM wa ya kuwa tume tajwa haina uwalakini na sasa wamehamia kwenye mabunge mawili ambako wanaona mirija yao ni michache na kwa hiyo wanatafuta namna ya kuiongeza.
Hii siyo demokrasia hata chembe bali ni ubinafsi tu...period. Mwanamageuzi wa kweli atadai haki hata kama yeye ni mwathirika wa hayo mageuzi siyo yule ambaye hujigeuza mpiga filimbi ya Hamelini pale anapoona masilahi yake yamepigwa na tufani kali sana...anachofanya ni kulinda tonge lake la ugali lisidondokee pabaya tu....lol hao kweli ni wababaishaji tu hawatufai kabisa.........
USHAURI:
Hivyo chama chochote kile cha siasa ambacho kitashirikisha wanachama wake katika kuteua viongozi watakaopeperusha bendera za vyama vyao katika ngazi zote ikiwemo ya URAISI, UBUNGE, UDIWANI hadi UENYEKITI WA KITONGOJI kina nafasi njema ya kutupatia viongozi bora...na kutumia utaratibu huohuo katika kuwavua madaraka itakuwa imepiga hatua katika demokrasia shirikishi.
Have your say too...unaridhika na demokrasia ndani ya vyama vya siasa hasa hivi vya upinzani hata sasa kuviamini kutupatia Raisi na viongozi wengineo bora bila ya kutushirikisha grassroots?
a) Vyama vyote vya upinzani vimeiga mfumo mbovu wa kidemokrasia wa ccm na vinaendeshwa kibabe-kibabe mno na huku wenzao wa ccm kuanzia 2010 walianza kujivua gamba la udikteta pale waliporuhusu wabunge wake wachaguliwe na wananchi moja kwa moja...ingawaje bado wana safari ndefu kwenye hili lakini lazima niwapongeze ccm kwa angalau kujaribu....rushwa na kuingiliwa na ngazi za juu katika maoni ya wananchi ni changamoto ambazo ccm itabidi waendelee kuzitafutia muarobaini wake.
Kwenye hili vyama vya upinzani wapo nyuma na tumeona hata chadema bila ya kupitisha kura ya maoni kwa wapigakura wa Arusha wakitumia kauli za kidikteta kukejeli kura za wanachama wao Arusha pale kamati kuu yao ilipotengua madiwani wakaidi wa Arusha...well, chadema worshippers...that was not democracy at all...it was dictatorship.........face it now before it is too late.....Only the truth will set you free
b) Vyama vyote vya siasa vyenye wabunge Bungeni vimekumbwa na dhoruba kali la wizi na ubadhirifu wa ruzuku ya hazina na hakuna uthibiti wa aina yoyote ile!!!!!
Kwa mtazamo wangu kama wapinzani wameshindwa hata kusimamia kidogo ambacho tumewapa ni kwa upuuzi upi utushawishi kuwakabidhi nchi yote?
Njaa ya viongozi wa upinzani ni kali kulikoni ya viongozi wa ccm ambao pamoja na bandubandu kweli humaliza gogo lakini ccm hawana uchu wa kututafuna kama upinzani walionao.....ccm vibosile wake wamekwisha shiba njaa siyo kali sana kwa kipimo cha malinganisho.................lol
c) Mchakato wa katiba mpya umenifungua macho hila na upofu wa wapinzani ambao waliipinga tume kwa vile wao hawajaweka mrija wao ndani yake na kunyonya Hazina baada ya CCM kuwaingiza kingi - au niseme mkenge? - hakuna anayehoji uhalali wa Tume ya kukusanya maoni.
Wote wanaimba wimbo wa CCM wa ya kuwa tume tajwa haina uwalakini na sasa wamehamia kwenye mabunge mawili ambako wanaona mirija yao ni michache na kwa hiyo wanatafuta namna ya kuiongeza.
Hii siyo demokrasia hata chembe bali ni ubinafsi tu...period. Mwanamageuzi wa kweli atadai haki hata kama yeye ni mwathirika wa hayo mageuzi siyo yule ambaye hujigeuza mpiga filimbi ya Hamelini pale anapoona masilahi yake yamepigwa na tufani kali sana...anachofanya ni kulinda tonge lake la ugali lisidondokee pabaya tu....lol hao kweli ni wababaishaji tu hawatufai kabisa.........
USHAURI:
Hivyo chama chochote kile cha siasa ambacho kitashirikisha wanachama wake katika kuteua viongozi watakaopeperusha bendera za vyama vyao katika ngazi zote ikiwemo ya URAISI, UBUNGE, UDIWANI hadi UENYEKITI WA KITONGOJI kina nafasi njema ya kutupatia viongozi bora...na kutumia utaratibu huohuo katika kuwavua madaraka itakuwa imepiga hatua katika demokrasia shirikishi.
Have your say too...unaridhika na demokrasia ndani ya vyama vya siasa hasa hivi vya upinzani hata sasa kuviamini kutupatia Raisi na viongozi wengineo bora bila ya kutushirikisha grassroots?