GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,848
- 109,557
1. Kikosi cha jana dhidi ya Senegal alikipinga Yeye au alisaidiwa na akina Karia pamoja na Mwakyembe?
2. Ni kwanini ana Chuki sana na Wachezaji Nyota wanaotoka Klabu ya Simba Sports Club?
3. Kwanini alimpanga Beki David Mwantika ambaye alimuita kutoka Tanzania, hakuwa na Mazoezi ya pamoja na Wenzake, wala match Fitness na akampanga huku akimpanga Benchi Mchezaji Kiraka Erasto Nyoni?
4. Anaweza kunipa sababu ya Yeye kupenda kuwatumia Wachezaji kama Himid Mao na Mudathiri Yahaya katika Kiungo cha Ukabaji huku akimuacha na Kumchukia kabisa Natural Defensive Midfielder na ambaye yupo katika Kiwango cha juu Tanzania nzima kwa miaka kadhaa sasa Jonas Gerald Mkude?
5. Je zile Rafu za Kipumbavu ( Kiduduna ) walizokuwa wakizicheza akina David Mwantika, Faisal Salum na Himid Mao Yeye ndiye aliwatuma hivyo walikuwa wakitekeleza Maelekezo yake?
6. Je mpaka hivi sasa Kichwani mwake ana Kikosi chake cha Kwanza kiasi kwamba hata nikimuamsha tu Usiku wa Manane atanitajia bila matatizo yoyote?
7. Je baada ya Beki wake Aggrey Morris Kuumia alipaswa amuite Beki Abdi Banda ambaye alikuwa nae huko huko Kambini Misri au alipaswa amuite Beki David Mwantika ambaye hapo mwanzoni hakumjumuisha katika Kikosi chake kile cha Wachezaji 33 alioondoka nao?
8. Ni kwanini anawapenda sana Wachezaji Thomas Ulimwengu na Himid Mao kiasi kwamba hata kama wakiwa hawako katika Form au Majeruhi lakini Yeye ni lazima tu atawaita na kwenda nao popote pale ambapo Taifa Stars itaweka Kambi yake?
9. Je kati ya Thomas Ulimwengu na Rashid Mandawa ni Mchezaji gani ambaye Kiuhalisia na jinsi Mechi ilivyokuwa Jana alitakiwa ndiyo amuingize ili aweze kuleta Uhai au Mabadiliko katika Timu?
10. Kama tukiamua Kuangalia Mchezaji ambaye amepata Uzoefu wa Michuano mikubwa mikubwa ya Kimataifa je Kwake Yeye kati ya Mohammed Hussein Tshabalala kutoka Simba SC na Gadiel Michael kutoka Yanga SC ni nani angefaa na pengine hata Kumuanzisha katika Mechi ya Jana?
11. Tanzania tunajivunia sana Wachezaji wanaocheza Ligi Kubwa tena za Ulaya kama Samatta anayecheza KRC Genk ya Ubelgiji na Yousuf anayecheza Blackpool ya Uingereza ni kwanini ameamua tu Kumtumia Samatta na Wachezaji wengine wa Kulipwa ila wanacheza Klabu za hapa hapa barani Afrika zisizo na Mafanikio akina Msuva, Himid na Ulimwengu na akimuacha Yousuf benchini?
Mwisho kabisa akishanijibu haya Maswali yangu Kumi na Moja ( 11 ) naomba anisaidie pia kuniambia ni lini atatuachia Timu yetu ya Taifa Stars ili waje Makocha wenye Kuujua Mpira kuliko Yeye, wasio na Chuki wala Visasi kwa Wachezaji kabla Mimi na Wenzangu wenye Uchungu na Hasira kali dhidi yake hatujaamua Kumvizia pale Uwanjani JNIA akirudi na Timu kisha tumpopoe na Mawe na aione Tanzania hii Chungu Kwake!
Msisahau kumwambia kuwa mwana JamiiForums Mimi An Eagle a.k.a BRAINIAC namsalimia ila simkubali kabisa na aondoke tu.
2. Ni kwanini ana Chuki sana na Wachezaji Nyota wanaotoka Klabu ya Simba Sports Club?
3. Kwanini alimpanga Beki David Mwantika ambaye alimuita kutoka Tanzania, hakuwa na Mazoezi ya pamoja na Wenzake, wala match Fitness na akampanga huku akimpanga Benchi Mchezaji Kiraka Erasto Nyoni?
4. Anaweza kunipa sababu ya Yeye kupenda kuwatumia Wachezaji kama Himid Mao na Mudathiri Yahaya katika Kiungo cha Ukabaji huku akimuacha na Kumchukia kabisa Natural Defensive Midfielder na ambaye yupo katika Kiwango cha juu Tanzania nzima kwa miaka kadhaa sasa Jonas Gerald Mkude?
5. Je zile Rafu za Kipumbavu ( Kiduduna ) walizokuwa wakizicheza akina David Mwantika, Faisal Salum na Himid Mao Yeye ndiye aliwatuma hivyo walikuwa wakitekeleza Maelekezo yake?
6. Je mpaka hivi sasa Kichwani mwake ana Kikosi chake cha Kwanza kiasi kwamba hata nikimuamsha tu Usiku wa Manane atanitajia bila matatizo yoyote?
7. Je baada ya Beki wake Aggrey Morris Kuumia alipaswa amuite Beki Abdi Banda ambaye alikuwa nae huko huko Kambini Misri au alipaswa amuite Beki David Mwantika ambaye hapo mwanzoni hakumjumuisha katika Kikosi chake kile cha Wachezaji 33 alioondoka nao?
8. Ni kwanini anawapenda sana Wachezaji Thomas Ulimwengu na Himid Mao kiasi kwamba hata kama wakiwa hawako katika Form au Majeruhi lakini Yeye ni lazima tu atawaita na kwenda nao popote pale ambapo Taifa Stars itaweka Kambi yake?
9. Je kati ya Thomas Ulimwengu na Rashid Mandawa ni Mchezaji gani ambaye Kiuhalisia na jinsi Mechi ilivyokuwa Jana alitakiwa ndiyo amuingize ili aweze kuleta Uhai au Mabadiliko katika Timu?
10. Kama tukiamua Kuangalia Mchezaji ambaye amepata Uzoefu wa Michuano mikubwa mikubwa ya Kimataifa je Kwake Yeye kati ya Mohammed Hussein Tshabalala kutoka Simba SC na Gadiel Michael kutoka Yanga SC ni nani angefaa na pengine hata Kumuanzisha katika Mechi ya Jana?
11. Tanzania tunajivunia sana Wachezaji wanaocheza Ligi Kubwa tena za Ulaya kama Samatta anayecheza KRC Genk ya Ubelgiji na Yousuf anayecheza Blackpool ya Uingereza ni kwanini ameamua tu Kumtumia Samatta na Wachezaji wengine wa Kulipwa ila wanacheza Klabu za hapa hapa barani Afrika zisizo na Mafanikio akina Msuva, Himid na Ulimwengu na akimuacha Yousuf benchini?
Mwisho kabisa akishanijibu haya Maswali yangu Kumi na Moja ( 11 ) naomba anisaidie pia kuniambia ni lini atatuachia Timu yetu ya Taifa Stars ili waje Makocha wenye Kuujua Mpira kuliko Yeye, wasio na Chuki wala Visasi kwa Wachezaji kabla Mimi na Wenzangu wenye Uchungu na Hasira kali dhidi yake hatujaamua Kumvizia pale Uwanjani JNIA akirudi na Timu kisha tumpopoe na Mawe na aione Tanzania hii Chungu Kwake!
Msisahau kumwambia kuwa mwana JamiiForums Mimi An Eagle a.k.a BRAINIAC namsalimia ila simkubali kabisa na aondoke tu.