Lekanjobe Kubinika
JF-Expert Member
- Dec 6, 2006
- 3,020
- 577
Mimi ni mmoja wa watu wanaodharau wanamuziki wa bongofleva hasa pale wanapomkatikia kiuno Mkwere hasa kwenye matukio ya uchaguzi. Naona mambo yanaanza kubadilika. Alianza Sugu na Mkoloni. Safari hii Selemani Msindi, narudia tena SULEMAN amenukuliwa akisema yafuatayo dhidi ya Kikwete:
Anajenga makundi ya chuki na uhasama katika kila sekta kuanzia kwenye chama chake, serikali yake na sasa kwenye sanaa na haswa mziki wetu ambao ndio amekuwa akijinadi kuusaidia kumbe katika hii awamu yake ndio mziki umepotea mwelekeo. Sasa kama anasema studio aliwapa waliomuomba mbona mimi na watu wengine wenye misimamo tulikuwepo siku ile alipoahidi studio hatujui lolote na hatujaonyeshwa hiyo studio?" [/SIZE][/FONT][/I]
Source: BONGO STAR LINK
"Ah, huyu JK kwa tamko lake hili kuhusu studio aliyowapa THT na Ruge anaonyesha jinsi gani asivyo kiongozi makini na kwa mtazamo halisi anaonyesha ni jinsi gani hakustahili kuwa mkuu wa nchi.
Masikini Sele! Anakumbuka shuka wakati ndio kumekucha? Pole sana. Mliyemsifia ndiye huyo ndugu yangu. Anajua hana kipindi kingine baada ya hapa na kwa hivyo anaonyesha makucha yake kweupeeee! Mwanaume anapotafuta mchumba humchunguza sana anayemuwania pasipo muwaniwa mwenyewe kujua kama anachambuliwa. Lakini akishajionyesha na kuchunguzwa yeye ndipo huficha makucha yake yasionwe. Ngoja muanze kuishi pamoja, kila kucha na urefu wake utalijua! Kwa sababu hata konda huwajali abiria walioko nje ya bus lake na sio walioko ndani ya bus tayari. Ukibisha omba msaada kushushwa kona ilee! Utaambulia matusi na dharau "Hii sio baiskeli bwana, sishushi pale" Lakini akimwona abiria anakuja kwenye kona utasikia konda anaita "Kichwa babu punguza mwendo; Ukakwenda? Mpe mchuma juu kwa juu"