Kipeperushi
Senior Member
- Aug 17, 2011
- 167
- 33
Hivi karibuni, takribani miezi mitatu au zaidi, nimekuwa nikipokea e-mail kwa nyakati tofauti toka kwa watu mbalimbali ambao baadae nilikuja kugundua kwamba hawakuwa na maelezo ya ukweli kwangu. Kwa kifupi watu hawa ni wadada, (ingawa sidhani kama kweli watu hawa huwa ni wadada au la..!). Katika maelezo yao, ambayo mara nyingi huambatanishwa na picha za wasichana (kwa madai kwamba ndio picha za wahusika), watu hawa wamekuwa wakidai kwamba eti wamevutiwa na mimi baada ya kutembelea Profile yangu kwenye Facebook na Netlog kwa hiyo wanaomba niwajibu kwenye yahoo mail ili tuendelee kufanya mawasiliano ya kirafiki kupitia yahoo.
E mail mbili za kwanza (ambazo zilitofautiana kama siku tatu hivi) nilizijibu positively ingawa hizi za mtu wa pili zilianza kunipa doubt, kwani zilinionyesha wazi kwamba zilikuwa ni copy za zile za yule mtu wa kwanza (isipokuwa zilikuwa zimefanyiwa editing kidogo). Wote walikuwa wakidai kuwa ni raia wa Rwanda ambao walijikuta wanalazimika kuishi kwenye Refugee Camps zilizopo mjini Dakar Senegal baada ya kukimbia vita nchini Rwanda.
Baada ya kuwasiliana nao kwa mara kadhaa na kupata story juu ya maisha yao huko Senegal, niliamua kutafuta ukweli kuhusu hii kitu inayoitwa REFUGEE CAMP IN DAKAR SENEGAL. Nilipokwenda kwenye Google niligundua hapakuwa na story yoyote ya ukweli kutoka kwa wadada hao ila tu hii ilikuwa ni tricks za INTERNET SCAMMERS.
Baada ya kugudua upuuzi huo niliamua kuwachana. Kimsingi niliwatukana kinoma na nikawaambia kuwa wakiendelea kunifuatilia watapoteza muda wao bure. Sasa wana jamii, kinachoendelea ni kwamba hizi e mail zinakuja kama mvua sasa hivi. Swali langu ni kwamba hawa watu hawataniletea Virus wabaya kwenye computer yangu? Maana naona wako so tricky na wananifuatilia sana. Nifanye nini ili kuwa avoid? Siwezi kubadili e mail address yangu kwa sasa.
E mail mbili za kwanza (ambazo zilitofautiana kama siku tatu hivi) nilizijibu positively ingawa hizi za mtu wa pili zilianza kunipa doubt, kwani zilinionyesha wazi kwamba zilikuwa ni copy za zile za yule mtu wa kwanza (isipokuwa zilikuwa zimefanyiwa editing kidogo). Wote walikuwa wakidai kuwa ni raia wa Rwanda ambao walijikuta wanalazimika kuishi kwenye Refugee Camps zilizopo mjini Dakar Senegal baada ya kukimbia vita nchini Rwanda.
Baada ya kuwasiliana nao kwa mara kadhaa na kupata story juu ya maisha yao huko Senegal, niliamua kutafuta ukweli kuhusu hii kitu inayoitwa REFUGEE CAMP IN DAKAR SENEGAL. Nilipokwenda kwenye Google niligundua hapakuwa na story yoyote ya ukweli kutoka kwa wadada hao ila tu hii ilikuwa ni tricks za INTERNET SCAMMERS.
Baada ya kugudua upuuzi huo niliamua kuwachana. Kimsingi niliwatukana kinoma na nikawaambia kuwa wakiendelea kunifuatilia watapoteza muda wao bure. Sasa wana jamii, kinachoendelea ni kwamba hizi e mail zinakuja kama mvua sasa hivi. Swali langu ni kwamba hawa watu hawataniletea Virus wabaya kwenye computer yangu? Maana naona wako so tricky na wananifuatilia sana. Nifanye nini ili kuwa avoid? Siwezi kubadili e mail address yangu kwa sasa.