Je ni kweli Africa Inahitaji Miradi Kama Hii ya BRT ya Umeme kama huu wa Senegal?

ChoiceVariable

JF-Expert Member
May 23, 2017
43,063
49,749
Nimeona Senegal wanazindua mradi wa Barabara za BRT ambazo zinatumia Umeme.

Yaani kama hiyo BRT ya Dar ila iwe ni mfumo wa kuchaji/Umeme badala ya diesel.

Kwangu binafsi naona hii ni miradi ya kipigaji na isiyosaidia watu maskini kuongeza kipato Chao badala yake ni upigaji wa wakubwa.

Miradi ya hivi inapendwa sana na watu wasio na akili ila wajinga hudhani Wana akili.

Kwangu Mimi Ili Kiongozi awe wa maana lazima nione anachukua initiative ambazo zitamsaidia maskini wa Kijijini kuepukana na umaskini wake mfano kubadili Kilimo chake kiwe Chenye Tija,kubadili Ufugaji wake uwe wenye Tija,kubadili machinga awe muuzaji mkubwa nk nk.

Lakini haya mamiradi ya kujenga Jenga ni mamiradi ya watu wasio na akili ambao kila layman anaweza.

Ndio maana namsifj Samia Kwa kujitumbukiza kwenye BBT Kwa sababu unaona Kuna logic na Kuna nia ya kuondoa Vijana wanaozurula huko na Kuwavutia kwenye Kilimo.

Swali.

Ni kweli Africa Inahitaji BRT ya Umeme kwamba ndio itaondoa Umaskini Kwa watu?
Screenshot_20240102-160347.jpg
 
Kupanga ni kuchagua Senegal wako Sawa kufanya hivyo maana kwao ni tija,kwetu sisi sio tija.Na kuweka mambo Sawa kila nchi ina mahitaji yake na vipaombele vyake hivyo basi Mimi sioni haja ya wewe kuona watu ni wajinga.
 
Haswaaa
Umeweka wazi bila kupindisha
Masikini hahitaji haya, kuna mambo ya kuiga kwa manufaa ya wananchi wengi ila wao viongozi wanatafuta njia za kuiba tu hakuna lingine
 
Haswaaa
Umeweka wazi bila kupindisha
Masikini hahitaji haya, kuna mambo ya kuiga kwa manufaa ya wananchi wengi ila wao viongozi wanatafuta njia za kuiba tu hakuna lingine
Maviongozi yasiyo na akili yanakilimbia mamiradi makubwa ya ujenzi Ili wapige pesa na kutafuta sifa Kwa wajinga but has nothing to do with reducing or getting away with their poverty.

Ndio maana Nchi kama Ethiopia pamoja na reli za umeme ila Wananchi wanakimbia hakuna maisha.
 
Kupanga ni kuchagua Senegal wako Sawa kufanya hivyo maana kwao ni tija,kwetu sisi sio tija.Na kuweka mambo Sawa kila nchi ina mahitaji yake na vipaombele vyake hivyo basi Mimi sioni haja ya wewe kuona watu ni wajinga.
Afrika yote inafanana,Tija ipi Kwa maskini wa Senegal? Huko wanakoandamnaa kila siku maisha magumu ndio Kuna Tija?
 
Ukiokoa mda wa watu wa mjini kupotea njiani umeokoa pesa nyingi zitakazoenda kutumika huko vijijini.
Umeme unaokoa matumizi ya uagizaji mafuta nje na uokoa pesa za kigeni
 
Maviongozi yasiyo na akili yanakilimbia mamiradi makubwa ya ujenzi Ili wapige pesa na kutafuta sifa Kwa wajinga but has nothing to do with reducing or getting away with their poverty.

Ndio maana Nchi kama Ethiopia pamoja na reli za umeme ila Wananchi wanakimbia hakuna maisha.

..kama ujenzi wa mji mkuu dodoma.
 
..kama ujenzi wa mji mkuu dodoma.
Tungeweka tuu ratiba ya ujenzi Kwa phases badala ya kukurupuka na iwe kwenye sheria ,Kwa sababu takribani Trilioni 5 zimelala pale ambazo kiuchumi opportunity cost yake ni kubwa sana.

The likes of Sgr kwenda huko badala ya kwenda Zambia/DRC
 
Nimeona Senegal wanazindua mradi wa Barabara za BRT ambazo zinatumia Umeme.

Yaani kama hiyo BRT ya Dar ila iwe ni mfumo wa kuchaji/Umeme badala ya diesel.

Kwangu binafsi naona hii ni miradi ya kipigaji na isiyosaidia watu maskini kuongeza kipato Chao badala yake ni upigaji wa wakubwa.

Miradi ya hivi inapendwa sana na watu wasio na akili ila wajinga hudhani Wana akili.

Kwangu Mimi Ili Kiongozi awe wa maana lazima nione anachukua initiative ambazo zitamsaidia maskini wa Kijijini kuepukana na umaskini wake mfano kubadili Kilimo chake kiwe Chenye Tija,kubadili Ufugaji wake uwe wenye Tija,kubadili machinga awe muuzaji mkubwa nk nk.

Lakini haya mamiradi ya kujenga Jenga ni mamiradi ya watu wasio na akili ambao kila layman anaweza.

Ndio maana namsifj Samia Kwa kujitumbukiza kwenye BBT Kwa sababu unaona Kuna logic na Kuna nia ya kuondoa Vijana wanaozurula huko na Kuwavutia kwenye Kilimo.

Swali.

Ni kweli Africa Inahitaji BRT ya Umeme kwamba ndio itaondoa Umaskini Kwa watu?
View attachment 2860125
Ujinga bora tram za umeme
 
Diesel ni gharama kuliko umeme. Ndio wanahitaji ili kusave hela in future.
1. Senegal umeme ni uhakika haukatiki mara kwa mara.
2. Umeme ni nafuu kuliko diesel na hawaimport umeme kama wanavyoimport diesel.
3. Usafiri wa uma wa Senegal ni hovyo mabasi mabaya sana. So mradi huu ni sahii kupandisha hadhi ya public transport.
 
Ni kama Bongo treni ya umeme.

Inakula matrilion ya pesa .

Magu namkubali ila swala la kujenga reli mpya ndefu halikuwa na ulazima.

Angeboresha zile zile reli za zamani. Treni za kizamani mbona zinabeba mizigo na abiria fresh kabisa.

Hizo trilioni za kujenga reli..zingejenga kiwanda kikubwa cha kusapoti agliculture zetu for export
 
Maviongozi yasiyo na akili yanakilimbia mamiradi makubwa ya ujenzi Ili wapige pesa na kutafuta sifa Kwa wajinga but has nothing to do with reducing or getting away with their poverty.

Ndio maana Nchi kama Ethiopia pamoja na reli za umeme ila Wananchi wanakimbia hakuna maisha.
Kwanza hao wa Ethiopia ndio wabaya zaidi mkuu
Yaani wananchi wanaikimbia nchi yao kwa mguu huku wanapigwa risasi za mgongo na ndugu zao wanajeshi
Leo inawafanya watu wazikimbie nchi zao kwa tamaa za wachache ila ipo siku hawa hawa watakuja kubadilika na kuwa na hofu ya Mungu haswa na kukataa viongozi majizi na yasiyokuwa na huruma kwa wenzao
Miradi ya upigaji halafu haiishi hebu tuone SGR mpaka July hiyo ahadi
Ila kwq kuwa waafrika huwa wanaogopa ila hawana haya wala Soni, utaona wanavyomaliza kwa haraka hata kabla ya July ili tu kumridhisha Wa juu
Ila umasikini utakuwa palepale
 
Nimeona Senegal wanazindua mradi wa Barabara za BRT ambazo zinatumia Umeme.

Yaani kama hiyo BRT ya Dar ila iwe ni mfumo wa kuchaji/Umeme badala ya diesel.

Kwangu binafsi naona hii ni miradi ya kipigaji na isiyosaidia watu maskini kuongeza kipato Chao badala yake ni upigaji wa wakubwa.

Miradi ya hivi inapendwa sana na watu wasio na akili ila wajinga hudhani Wana akili.

Kwangu Mimi Ili Kiongozi awe wa maana lazima nione anachukua initiative ambazo zitamsaidia maskini wa Kijijini kuepukana na umaskini wake mfano kubadili Kilimo chake kiwe Chenye Tija,kubadili Ufugaji wake uwe wenye Tija,kubadili machinga awe muuzaji mkubwa nk nk.

Lakini haya mamiradi ya kujenga Jenga ni mamiradi ya watu wasio na akili ambao kila layman anaweza.

Ndio maana namsifj Samia Kwa kujitumbukiza kwenye BBT Kwa sababu unaona Kuna logic na Kuna nia ya kuondoa Vijana wanaozurula huko na Kuwavutia kwenye Kilimo.

Swali.

Ni kweli Africa Inahitaji BRT ya Umeme kwamba ndio itaondoa Umaskini Kwa watu?
View attachment 2860125
Ungekuwa unajua hesabu ungejua wana akili kuliko sisi, gharama ya kuendesha basi linalotumia umeme iko chini kuliko mafuta, ulaya walianza zaidi ya miaka 100 iliyopita.
 
Back
Top Bottom