mcubic
JF-Expert Member
- Mar 3, 2011
- 10,310
- 6,544
SERIKALI ya Rais John Magufuli imekosolewa kwamba haijafanya lolote linaloitambulisha kama serikali ya kimageuzi na badala yake imeboresha tu mambo yaliyokuwepo.
Katika mazungumzo na Raia Mwema yaliyofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita, Kiongozi wa chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, alisema ingawa kuna mazuri aliyoyaona kwa Magufuli, hajamuona kama kiongozi anayeweza kuleta mageuzi kwa Watanzania.
Alisema alikuwa anataraji kuwa Magufuli angekuwa kiongozi atakayeweza kubadili mfumo wa nchi yetu katika maeneo muhimu lakini hadi sasa alichoona ni kubana matumizi, kufukuza watumishi na kuongeza juhudi za kukusanya mapato, lakini bila ya kufanya mabadiliko ya vyombo husika kimkakati.
Akimnukuu mwandishi Archie Brown kwenye kitabu chake cha Myth of a Strong Leader, Zitto alisema kiongozi anayeweza kuleta mageuzi kwenye nchi ni yule ambaye “atafanya mabadiliko katika mifumo yote ya kisiasa na kiuchumi ili kuboresha maisha ya watu wake”.
“ Watumishi wa umma takribani 150 wamesimamishwa au kufukuzwa kazi katika kipindi cha siku hizi 100 za Magufuli. Aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Edward Hosea, ameondolewa, kama ilivyokuwa kwa Kamishina Mkuu wa TRA, Rished Bade. Lakini, nini kimebedilishwa kwenye taasisi hizo? Takukuru imepewa meno gani? Hayo ndiyo mambo ya kujiuliza,” alisema.
Hata hivyo, Zitto alisema siku 100 ni chache kumhukumu kiongozi ambaye amepewa miaka mitano ya kutawala, ingawa zinaweza kuonyesha picha ya aina gani ya kiongozi ambaye taifa linaweza kuwa naye katika kipindi hicho.
Kwa upande wake, mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Kitila Mkumbo, alisema baada ya siku 100 za Magufuli, bado anasubiri kuona dira, falsafa na mwelekeo wa kiongozi huyo. Alisema kipimo cha siku 100 kinachowekwa kwa marais wapya, kilianza kutumika nchini Marekani kutokana na mafanikio ya Rais Franklin Delano Roosevelt aliyeapishwa Machi 4, mwaka 1933 na ndani ya siku 100 alikuwa amepitisha sheria mpya 15 zilizosaidia kufufua uchumi wa Marekani.
“Katika hali isiyo ya kawaida, Rais Roosevelt alifanikiwa kushawishi Bunge kupitisha miswaada ya sheria 15 katika kipindi cha siku 100. Mwanahistoria mashuhuri James McGregor anaamini kwamba hadi leo hakuna Rais aliyevunja rekodi ya Rais Roosevelt ya kushawishi Bunge la Marekani kupitisha miswaada mingi kiasi hicho katika kipindi cha muda mfupi.
“Kufuatia kupitishwa kwa miswaada hiyo Serikali ya Roosevelt ilileta mageuzi makubwa ya kiuchumi yaliyosababisha ajira nyingi, na huo ndio ukawa mwanzo wa ukuu wa kiuchumi wa Taifa la Marekani tunaouona leo. “Kwa tathmini yangu ya siku 100 madarakani, Rais Magufuli amejipambanua vizuri kama kiongozi atakayepambana na kero za kijamii kama vile rushwa na ufisadi. Hata hivyo, Rais bado hajijipambanua katika maeneo mengine matatu muhimu ya kiuongozi, ambayo ni falsafa, dira, na ulinzi wa tunu za kitaifa.
Najua wapo watakaosema dira na falsafa ya Rais ni ‘Hapa kazi tu na kutumbua majipu’. Hapana. “Hizi sio dira wala falsafa. Hivi ni vibwagizo tu vya kisiasa! Nikimtakia kila la heri katika utawala wake, naendelea kuitafuta dira ya Rais Magufuli,” ameandika Kitila katika andishi lake lililochapwa kwenye gazeti hili.
Chanzo: Raia Mwema
Katika mazungumzo na Raia Mwema yaliyofanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki iliyopita, Kiongozi wa chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, alisema ingawa kuna mazuri aliyoyaona kwa Magufuli, hajamuona kama kiongozi anayeweza kuleta mageuzi kwa Watanzania.
Alisema alikuwa anataraji kuwa Magufuli angekuwa kiongozi atakayeweza kubadili mfumo wa nchi yetu katika maeneo muhimu lakini hadi sasa alichoona ni kubana matumizi, kufukuza watumishi na kuongeza juhudi za kukusanya mapato, lakini bila ya kufanya mabadiliko ya vyombo husika kimkakati.
Akimnukuu mwandishi Archie Brown kwenye kitabu chake cha Myth of a Strong Leader, Zitto alisema kiongozi anayeweza kuleta mageuzi kwenye nchi ni yule ambaye “atafanya mabadiliko katika mifumo yote ya kisiasa na kiuchumi ili kuboresha maisha ya watu wake”.
“ Watumishi wa umma takribani 150 wamesimamishwa au kufukuzwa kazi katika kipindi cha siku hizi 100 za Magufuli. Aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru, Edward Hosea, ameondolewa, kama ilivyokuwa kwa Kamishina Mkuu wa TRA, Rished Bade. Lakini, nini kimebedilishwa kwenye taasisi hizo? Takukuru imepewa meno gani? Hayo ndiyo mambo ya kujiuliza,” alisema.
Hata hivyo, Zitto alisema siku 100 ni chache kumhukumu kiongozi ambaye amepewa miaka mitano ya kutawala, ingawa zinaweza kuonyesha picha ya aina gani ya kiongozi ambaye taifa linaweza kuwa naye katika kipindi hicho.
Kwa upande wake, mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Profesa Kitila Mkumbo, alisema baada ya siku 100 za Magufuli, bado anasubiri kuona dira, falsafa na mwelekeo wa kiongozi huyo. Alisema kipimo cha siku 100 kinachowekwa kwa marais wapya, kilianza kutumika nchini Marekani kutokana na mafanikio ya Rais Franklin Delano Roosevelt aliyeapishwa Machi 4, mwaka 1933 na ndani ya siku 100 alikuwa amepitisha sheria mpya 15 zilizosaidia kufufua uchumi wa Marekani.
“Katika hali isiyo ya kawaida, Rais Roosevelt alifanikiwa kushawishi Bunge kupitisha miswaada ya sheria 15 katika kipindi cha siku 100. Mwanahistoria mashuhuri James McGregor anaamini kwamba hadi leo hakuna Rais aliyevunja rekodi ya Rais Roosevelt ya kushawishi Bunge la Marekani kupitisha miswaada mingi kiasi hicho katika kipindi cha muda mfupi.
“Kufuatia kupitishwa kwa miswaada hiyo Serikali ya Roosevelt ilileta mageuzi makubwa ya kiuchumi yaliyosababisha ajira nyingi, na huo ndio ukawa mwanzo wa ukuu wa kiuchumi wa Taifa la Marekani tunaouona leo. “Kwa tathmini yangu ya siku 100 madarakani, Rais Magufuli amejipambanua vizuri kama kiongozi atakayepambana na kero za kijamii kama vile rushwa na ufisadi. Hata hivyo, Rais bado hajijipambanua katika maeneo mengine matatu muhimu ya kiuongozi, ambayo ni falsafa, dira, na ulinzi wa tunu za kitaifa.
Najua wapo watakaosema dira na falsafa ya Rais ni ‘Hapa kazi tu na kutumbua majipu’. Hapana. “Hizi sio dira wala falsafa. Hivi ni vibwagizo tu vya kisiasa! Nikimtakia kila la heri katika utawala wake, naendelea kuitafuta dira ya Rais Magufuli,” ameandika Kitila katika andishi lake lililochapwa kwenye gazeti hili.
Chanzo: Raia Mwema