WAZUNGU WANAPOSEMA "LIFE BEGINS AT 40" WANA MAANA IPI?
_________________________________,
Wazungu wanapenda sana kusema kuwa "Life begins at 40" . Msemo huu huwa una maana kwamba mstakabali wa maisha ya binadamu mara nyingi unatafsirika pindi anapofikisha umri wa miaka 40 na kuendelea.
Leo nataka nikupe dondoo kamili za maisha ikiwa haujafikisha umri huo ama umefikisha.
1. Kwa umri huo ni muhimu uwe na familia kwa maana ya mke/mume na watoto ikiwa Mungu amekujalia.
(sio umri wa kutafuta mchumba huu)
2. Katika umri huo, hakikisha una kazi maalumu yenye kipato cha uhakika (hata kama ni kidogo) iwe ni kilimo,
biashara, ajira n.k
(sio umri wa kuanza kusaka kazi)
3. Kwenye umri wa miaka 40 punguza sana kusoma ili utumie muda mwingi kusomesha watoto na ndugu zako.
(sio lazima uongeze elimu)
4. Katika umri huu hakikisha ushaanza kuwekeza kwenye miradi hata midogo kulingana na kipato chako kwa ajili ya baadae.
(usitegemee chanzo kimoja cha mapato)
5. Katika umri wa miaka 40 hakikisha una makazi ya kudumu ama maandalizi ya makazi yawe katika utekelezaji mkubwa.
(miliki hata kiwanja)
6. Katika umri huo jaribu kupunguza baadhi ya tabia hatarishi kama ulevi, uvutaji wa sigara/bangi, uzinzi na tabia zingine zinazoweza kuathiri afya yako.
(punguza kula bata sana)
7. Ikiwa ni muajiriwa basi huu ndio umri sahihi wa kufanya maandalizi ya kustaafu. Yaani inabidi utengeneze mazingira utakayoishi baada ya kustaafu.
(usibweteke na ajira)
8. Miaka 40 ni rika la mpaka kati ya ujana na uzee. Hakikisha unajiweka katika maadili mema ili uwe kioo cha familia na jamii kwa ujumla. Ikiwezekana ishi katika falsafa za kimaadili ili watoto wako wajifunze.
(acha kufanya uhuni)
9. Katika umri huu hakikisha unatumia muda mwingi kukaa na familia na ndugu zako pindi unapopata muda ulio nje ya majukumu ili kupanda mbegu ya umoja na mshikamano kwa watoto wako.
(Epuka kushinda vijiweni Muda wote)
_________________________________,
Wazungu wanapenda sana kusema kuwa "Life begins at 40" . Msemo huu huwa una maana kwamba mstakabali wa maisha ya binadamu mara nyingi unatafsirika pindi anapofikisha umri wa miaka 40 na kuendelea.
Leo nataka nikupe dondoo kamili za maisha ikiwa haujafikisha umri huo ama umefikisha.
1. Kwa umri huo ni muhimu uwe na familia kwa maana ya mke/mume na watoto ikiwa Mungu amekujalia.
(sio umri wa kutafuta mchumba huu)
2. Katika umri huo, hakikisha una kazi maalumu yenye kipato cha uhakika (hata kama ni kidogo) iwe ni kilimo,
biashara, ajira n.k
(sio umri wa kuanza kusaka kazi)
3. Kwenye umri wa miaka 40 punguza sana kusoma ili utumie muda mwingi kusomesha watoto na ndugu zako.
(sio lazima uongeze elimu)
4. Katika umri huu hakikisha ushaanza kuwekeza kwenye miradi hata midogo kulingana na kipato chako kwa ajili ya baadae.
(usitegemee chanzo kimoja cha mapato)
5. Katika umri wa miaka 40 hakikisha una makazi ya kudumu ama maandalizi ya makazi yawe katika utekelezaji mkubwa.
(miliki hata kiwanja)
6. Katika umri huo jaribu kupunguza baadhi ya tabia hatarishi kama ulevi, uvutaji wa sigara/bangi, uzinzi na tabia zingine zinazoweza kuathiri afya yako.
(punguza kula bata sana)
7. Ikiwa ni muajiriwa basi huu ndio umri sahihi wa kufanya maandalizi ya kustaafu. Yaani inabidi utengeneze mazingira utakayoishi baada ya kustaafu.
(usibweteke na ajira)
8. Miaka 40 ni rika la mpaka kati ya ujana na uzee. Hakikisha unajiweka katika maadili mema ili uwe kioo cha familia na jamii kwa ujumla. Ikiwezekana ishi katika falsafa za kimaadili ili watoto wako wajifunze.
(acha kufanya uhuni)
9. Katika umri huu hakikisha unatumia muda mwingi kukaa na familia na ndugu zako pindi unapopata muda ulio nje ya majukumu ili kupanda mbegu ya umoja na mshikamano kwa watoto wako.
(Epuka kushinda vijiweni Muda wote)