Nyamemba
JF-Expert Member
- Nov 3, 2011
- 845
- 447
Zikiwa zimebaki wiki mbili kabla ya ziara ya Mkuu wa nchi,mh Jakaya Kikwete katika mkoa wa Mara,mapya yameibuka baada ya viongozi waandamizi Mkoani kuandaa kile kinachoitwa kukwamisha malengo ya ziara hiyo.
Kwanza kabisa kuna miradi kadhaa inatakiwa kufunguliwa ikiwemo ya maji na ukaguzi wa maabara katika shule za sekondari,lakini kutokana na miradi mingi ya maji kuchukuliwa na baadhi ya viongozi wa CCM hasa wajumbe wa NEC miradi hiyo imejengwa chini ya kiwango hali inayotia wasiwasi iwapo unaweza kumleta kiongozi wa nchi kuifungua.
Hayo ni maneno ya baadhi ya watalaam mjini Musoma wakionyesha wasiwasi wao iwapo kweli Mh Rais atafanya kilichokusudiwa,"unajua tender nyingi hasa wilayani zinachukuliwa na either makada wa CCM au marafiki zao,hali hii inapelekea miradi mingi kujengwa chini ya viwango"alisema kiongozi huyo.
Mfano timu yetu ilitembelea miradi ya maji wilayani Serengeti na kukuta MNEC wa pale ameijenga chini ya kiwango na Mh Rais ndo anatakiwa aizindue,sasa hapo inakuwa mtihani.
Kwa upande wa maabara hakuna kilichofanyika zaidi ya kuyageuza madarasa na kuyakarabati eti yawe maabara,kwa kweli tutaaibika iwapo mh Rais ataamua kuendelea na kile anachokuja kukifanya ndugu yangu,na wengine wetu (watendaji) hatujui hatma yetu iwapo hili litajulikana,alisema afisa mmoja wa ofisi ya RAIS.
Kwanza kabisa kuna miradi kadhaa inatakiwa kufunguliwa ikiwemo ya maji na ukaguzi wa maabara katika shule za sekondari,lakini kutokana na miradi mingi ya maji kuchukuliwa na baadhi ya viongozi wa CCM hasa wajumbe wa NEC miradi hiyo imejengwa chini ya kiwango hali inayotia wasiwasi iwapo unaweza kumleta kiongozi wa nchi kuifungua.
Hayo ni maneno ya baadhi ya watalaam mjini Musoma wakionyesha wasiwasi wao iwapo kweli Mh Rais atafanya kilichokusudiwa,"unajua tender nyingi hasa wilayani zinachukuliwa na either makada wa CCM au marafiki zao,hali hii inapelekea miradi mingi kujengwa chini ya viwango"alisema kiongozi huyo.
Mfano timu yetu ilitembelea miradi ya maji wilayani Serengeti na kukuta MNEC wa pale ameijenga chini ya kiwango na Mh Rais ndo anatakiwa aizindue,sasa hapo inakuwa mtihani.
Kwa upande wa maabara hakuna kilichofanyika zaidi ya kuyageuza madarasa na kuyakarabati eti yawe maabara,kwa kweli tutaaibika iwapo mh Rais ataamua kuendelea na kile anachokuja kukifanya ndugu yangu,na wengine wetu (watendaji) hatujui hatma yetu iwapo hili litajulikana,alisema afisa mmoja wa ofisi ya RAIS.