Zanzibar: Dr. Shein akwama,aishiwa muda wa kumchagua Makamu wa kwanza wa rais

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Rais wa Zanzibar,Dr. Ali Mohamed Shein amekwama katika kumteua Makamu wa Kwanza wa Rais wa Visiwani humo. Kikatiba,Makamu wa Kwanza wa Rais anapaswa kupendekezwa na chama chake na kuteuliwa na Rais.

Chama kinachopasa kumpendekeza Makamu wa Kwanza wa Rais ni kile kilichokamata nafasi ya pili uchaguzini na kupata asilimia zisizopungua kumi ya kura zote. Kwa mujibu wa matokeo ya uchaguzi,hakuna chama hata kimoja cha upinzani chenye sifa za kumpendekeza mteuliwa wa Makamu wa Kwanza wa Rais.

Siku saba za kikatiba,baada ya kuapishwa kwa Rais,zinaisha leo. Kuanzia leo kutakuwa na mkwamo mpya wa kikatiba na kisiasa Zanzibar. Kwanza,Serikali ya Umoja wa Kitaifa haitaundika kwakuwa hakuna chama cha upinzani chenye sifa za kumtoa Makamu wa Kwanza wa Rais au kushiriki kuunda SUK kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar. Na pili,kukosekana kwa Makamu wa Kwanza wa Rais ni kutotekelezwa masharti ya Katiba.

Dr. Shein yuko njiapanda!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
IMG_20160323_110930_068.jpg
 
Hahahah zamani nilikuwa nashangaa sana mababu zetu kukubali kirasi kutawaliwa na wakoloni nikijiuliza hivi hawakuwa na akili za kufikiri? Walikubalije kutawaliwa? Hawa waZanzibar wanionesha kumbe kutawaliwa ni rais sana cha muhimu ni kutanguliza masilahi binafsi mbele kuliko masilahi ya umma.

Kinachofanyika Zanzibar ni viongozi wa CCM zanzibar kutawala waZanzibar kwa niaba ya serikali ya Tanganyika na wao kina Shein bila kutambua hilo wapo wapo tu utadhani chief Mangungo kalewa mvinyo wa Mjerumani
 
Mleta mada mbona unajichanganya umeandika hakuna chama kilichopata zaidi ya 10% , sasa kama katiba inasema hivyo au huo muafaka basi chama kitakacho chagua makamu ni kimoja nacho ni ccm , mpaka hapo smz watakapo fanya marekebisho ya katiba au muafaka na hivyo vuama vingine. Period hakuna propaganda zingine zaidi ya hivyo
 
Siku saba za kikatiba,baada ya kuapishwa kwa Rais,zinaisha leo. Kuanzia leo kutakuwa na mkwamo mpya wa kikatiba na kisiasa Zanzibar. Kwanza,Serikali ya Umoja wa Kitaifa haitaundika kwakuwa hakuna chama cha upinzani chenye sifa za kumtoa Makamu wa Kwanza wa Rais au kushiriki kuunda SUK kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar. Na pili,kukosekana kwa Makamu wa Kwanza wa Rais ni kutotekelezwa masharti ya Katiba.


Na hapo ndipo panapojitokeza Nafasi kwa CUF kufungua kesi ya Kikatiba kutaka Uchaguzi urudiwe!. Kwa maana haiwezekani Dr.Shein kuunda serikali kwa kuwa kuna mapungufu ambayo tayari yako kinyume na Katiba ya Zanzibar!
 
Mleta mada mbona unajichanganya umeandika hakuna chama kilichopata zaidi ya 10% , sasa kama katiba inasema hivyo au huo muafaka basi chama kitakacho chagua makamu ni kimoja nacho ni ccm , mpaka hapo smz watakapo fanya marekebisho ya katiba au muafaka na hivyo vuama vingine. Period hakuna propaganda zingine zaidi ya hivyo

Kwani kiswahili nayo ngumu kiasi hicho!

10% ni kutoka chama cha Upinzani!. Kukosekana kwa hiyo 10% maana yake Serikali haiwezi kuundwa! Unaelewa Ukuu wa Katiba ya Nchi?
 
Hii siku sio ndefu sana kabla hatujasikia makamu wa kwanza wa rais. Sijui atakuwa nani. Mungu atupe uzima tuone
 
.....sarakazi nyingine atakayofanya shein ili kuwazuga wazenj kuwa ana serikali ya umoja wa kitaifa ni kuwateua jamaa kumi kuwa wawakilishi toka hivyo vyama vya hovyo vilivyokosa wawakilishi kwenye uchaguzi...alafu kati ya hao majamaa kumi wengine anawapa uwaziri kwenye serikali yake....ili kuonyesha ana serikali wakilishi.....hii ndio option pekee yuko nayo...na nlimsikia seif idd akisema hili.....Hili la makamu wa kwanza ndio imetoka....katiba haimruhusu...lakini kwa kiwango walichofikia cha kuvunja katiba wanaweza hata kuibadili na kufanya watakavyo....Nliwahi kusema kuwa ccm zenj wanafurahia sana hali hii....maana wanaweza kufanya watakavyo.....
 
Rais wa Zanzibar,Dr. Ali Mohamed Shein amekwama katika kumteua Makamu wa Kwanza wa Rais wa Visiwani humo. Kikatiba,Makamu wa Kwanza wa Rais anapaswa kupendekezwa na chama chake na kuteuliwa na Rais.

Chama kinachopasa kumpendekeza Makamu wa Kwanza wa Rais ni kile kilichokamata nafasi ya pili uchaguzini na kupata asilimia zisizopungua kumi ya kura zote. Kwa mujibu wa matokeo ya uchaguzi,hakuna chama hata kimoja cha upinzani chenye sifa za kumpendekeza mteuliwa wa Makamu wa Kwanza wa Rais.

Siku saba za kikatiba,baada ya kuapishwa kwa Rais,zinaisha leo. Kuanzia leo kutakuwa na mkwamo mpya wa kikatiba na kisiasa Zanzibar. Kwanza,Serikali ya Umoja wa Kitaifa haitaundika kwakuwa hakuna chama cha upinzani chenye sifa za kumtoa Makamu wa Kwanza wa Rais au kushiriki kuunda SUK kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar. Na pili,kukosekana kwa Makamu wa Kwanza wa Rais ni kutotekelezwa masharti ya Katiba.

Dr. Shein yuko njiapanda!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam


Ninyi Lumumba, tangu lini katiba ikawa na maana wala thamani machoni penu? Anasubiri kikwete amshauri cha kufanya halafu atakifanya kwa nguvu ya majeshi kama alivyojitawaza. Hatutegemei lolote linaweza kufanywa na ccm kwa mtengamano wa kikatiba labda liwe na maslahi kwao binafsi.

Subiri mtaona.
 
Rais wa Zanzibar,Dr. Ali Mohamed Shein amekwama katika kumteua Makamu wa Kwanza wa Rais wa Visiwani humo. Kikatiba,Makamu wa Kwanza wa Rais anapaswa kupendekezwa na chama chake na kuteuliwa na Rais.

Chama kinachopasa kumpendekeza Makamu wa Kwanza wa Rais ni kile kilichokamata nafasi ya pili uchaguzini na kupata asilimia zisizopungua kumi ya kura zote. Kwa mujibu wa matokeo ya uchaguzi,hakuna chama hata kimoja cha upinzani chenye sifa za kumpendekeza mteuliwa wa Makamu wa Kwanza wa Rais.

Siku saba za kikatiba,baada ya kuapishwa kwa Rais,zinaisha leo. Kuanzia leo kutakuwa na mkwamo mpya wa kikatiba na kisiasa Zanzibar. Kwanza,Serikali ya Umoja wa Kitaifa haitaundika kwakuwa hakuna chama cha upinzani chenye sifa za kumtoa Makamu wa Kwanza wa Rais au kushiriki kuunda SUK kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar. Na pili,kukosekana kwa Makamu wa Kwanza wa Rais ni kutotekelezwa masharti ya Katiba.

Dr. Shein yuko njiapanda!

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
Najiuliza maswali mengi majibu sipati;
1) kuna raha gani kutawala kimabavu ilhali ulijua hujashinda?
2) ikiwa pamoja na misaada ya wafadhili ulishindwa kuinuaaisha ya wananchi, itakuwaje bila misaada?
3),kuna faida gani kuendelea kuona mpasuko ukiongezeka zanzibar?
4) kuna faida gan kutumia miaka mingine 5 ijayo kushughulikia mgogoro znz wakati dawa ni kufanya haki yaani kuwapa cuf ushindi wao mambo yasonge?
5) hivi nani yuko nya ya mkwamo huu..mkapa? Kikwete? Magufuli? ,siamini kama jecha au sheini pekee, kwangu haiingii akilini...nisaidieni naoma giza mbeleni...
Ni kweli sisi ni tajiri na tunapaswa kujitegemea lakini kwa maandalizi ya kutosha na sio kwa ghafla namna hii. Tutakamuana sana
 
Kwani kiswahili nayo ngumu kiasi hicho!

10% ni kutoka chama cha Upinzani!. Kukosekana kwa hiyo 10% maana yake Serikali haiwezi kuundwa! Unaelewa Ukuu wa Katiba ya Nchi?
Uko sawa maana vyama vya upinzani nilipata 3% na 1% na vingine 0% hivyo kwa asilimia hizo aziwezi kutoa makamu kutoka chama pinzani
 
Back
Top Bottom