Zanzibar: CUF wamegoma kweli, CCM mbele kwa mbele!

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,137
17,908
Sasa ni dhahiri kuwa CUF hawatashiriki uchaguzi wa marejeo wa Jumapili ingawa majina ya magombea wao yatakuwemo kwenye karatasi za kupigia kura. ZEC ya Jecha ilishasema kuwa hakuna mgombea aliyejitoa kisheria.

Dodosa zangu za hapa Unguja na kule Pemba zinaonesha kuwa CUF hawatashiriki katika uchaguzi huo,ikiwa ni pamoja na kutotuma mawakala wakati na baada ya kupigwa kura. CUF pia imewasihi Wajumbe wa ZEC wanaotokana na chama hicho kujiweka mbali na uchaguzi wa marejeo.

Wakati huo huo,CCM imejipanga kila idara kushiriki uchaguzi wa Jumapili. Imesema kuwa haitishwi na maneno kuwa uchaguzi huo ni wa maruhani na kwamba watajichagua wenyewe kwenye maonesho ya mazingaombwe ya Jumapili. CCM ni mbele kwa mbele!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Unguja,Zanzibar)
 
Washiriki ama wasishiriki, ushindi ni lazima kwa CCM. Wakati wa kudekezana umeshapita. Demokrasia hii tumeiga kwa wazungu
 
Washiriki ama wasishiriki, ushindi ni lazima kwa CCM. Wakati wa kudekezana umeshapita. Demokrasia hii tumeiga kwa wazungu
Kweli demokrasia mmeiiga kwa wazungu ccm mbele kwa mbele jua Na wanzanzibar wanajua wanachotaka Na sio kwa ccm mnachotaka uwezi kuwa Kiongozi Bora kwa mabavu
 
Ninashauri serikali yangu iendelee kupunguza matumizi yasiyo ya lazima na badala yake raslimali chache zilizopo ziendelee kutumika kwa mambo muhimu yenye manufaa.

Uchaguzi ni moja ya matumizi makubwa sana ya fedha umma. Mwaka jana fedha nyingi zimetumika kutarayirsha na kkuendesha uchaguzi usio kuwa na umuhimu. Sasa tena fedhanyingine nyingi zinatumika kuendehsa uchaguzi usio wa lazima. Majeshi mengi yanapelekwa kulinda amani zanzibar kwa gharama kubwa pasipo sababu. Malipo ya viongozi wa ZEC ni matumizi mabaya ya fedha za umma. SMZ inaendeshwa kwa gharama kubwa pasipo sababu ambazo zingeweza kujenga miundo mbinu mingina kuboresha maisha ya Watanzania .

Kwa kuwa hakuna sababu ya kufanya uchaguzi Zanzibar, ambao mara nyingi hugubikwa na malumbano na hatimaye umwagaji damu za watu wasio na hatia na uharibifu wa mali, i kiwa ni pamoja na matumizi mazito ya majeshi yetu, ninashauri Zanzibar ifanywe mkoa wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama ilivyo Mwanza, Kilimanjaro, Ruvuma, Tanga n.k.

Utaratibu wa kuwatangazia Watanzania wanaoishi Zanzibar kwamba sehemu hiyo ni sehemu safi kabisa kama zilvyosehemu zingine za Tanzania na hivyo, hakuna sababu ya kuwa na kasrikali kake na chaugzi zak. na badala yake kutakuwa na mkuu wa mkoa, RPC, Mkurugenzi wa maendeleo n.k kama ilivyo mikoa mingine na pasipo shaka maisha yao yatakuwa safi na salama chini ya serikali kuu moja.

Na hii pia itaawsaidia Wanzanzibar kuondokana na malalamiko kwamba serikali ya muungano inawasahua katika suala la maendelo badala yake budget zao na maendeleo yao yote yataratibiwa na kuendeshwa kama ilivyo mikoa mingine.

Kwa mantki hiyo hapatakuwa na uchaguzi kufutwa wala kurudia wala kunyanyaswa wala nini. Wote sisi ni Watanzania na utatkuwa kwa pamoja watanzania.

Tena ikibidi kkuwe na Chama kimoja tu cha siasa TAnzania ili tubanane huko huko kwenye arena moja. Kinyume cha hapa, hivi viini macho vinaelekea kuligharimu taifa na wala si Zanzibar peke yake.
 
Washiriki ama wasishiriki, ushindi ni lazima kwa CCM. Wakati wa kudekezana umeshapita. Demokrasia hii tumeiga kwa wazungu
La busara ni Jecha kuwapa ushindi kutokana na timu pinzani kutofika uwanjani. Hili la kuendelea na mechi bila kushiriki timu pinzani sio kishekesho tu ni uwandazimu. Fungeni mabao hadi elfu ukweli unabaki pale pale hiyo siyo mechi.
 
Watu wekeni akiba ya maneno, watu kama Lizaboni, Tatamadiba na wenzao nashindwa kwa kweli kuwaelewa, mabandiko yao, mawazo yao wanayoyaweka humu siwaelewi. Ila akipandacho mtu ndicho akivunacho, na hakuna marefu yasiyokua na ncha, walikuwepo mangwinji wa hiyo maneno wako wapi? kama unabisha muulize Ghadafi na wenzie, na mtalipwa hapa hapa kama sio nyie hata vizazi vyenu vitarithi hiyo laana, jaribuni kufuatilia vizazi vya machifu waliosimamia kuuza watumwa na kuuza nchi kwa wakoloni. Muwe na utu andika kitu usimujeruhi mwenzako, Siasa sio dhihaka wala kejeli ni maisha ya watu tunaongelea na mstakabala wa maisha yao ya hapa duniani na maandalizi ya maisha ya milele kwa Baba.
 
Sasa ni dhahiri kuwa CUF hawatashiriki uchaguzi wa marejeo wa Jumapili ingawa majina ya magombea wao yatakuwemo kwenye karatasi za kupigia kura. ZEC ya Jecha ilishasema kuwa hakuna mgombea aliyejitoa kisheria.

Dodosa zangu za hapa Unguja na kule Pemba zinaonesha kuwa CUF hawatashiriki katika uchaguzi huo,ikiwa ni pamoja na kutotuma mawakala wakati na baada ya kupigwa kura. CUF pia imewasihi Wajumbe wa ZEC wanaotokana na chama hicho kujiweka mbali na uchaguzi wa marejeo.

Wakati huo huo,CCM imejipanga kila idara kushiriki uchaguzi wa Jumapili. Imesema kuwa haitishwi na maneno kuwa uchaguzi huo ni wa maruhani na kwamba watajichagua wenyewe kwenye maonesho ya mazingaombwe ya Jumapili. CCM ni mbele kwa mbele!

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Unguja,Zanzibar)
ushujaa wa cuf umetukuka dunia nzima .
 
Watu wekeni akiba ya maneno, watu kama Lizaboni, Tatamadiba na wenzao nashindwa kwa kweli kuwaelewa, mabandiko yao, mawazo yao wanayoyaweka humu siwaelewi. Ila akipandacho mtu ndicho akivunacho, na hakuna marefu yasiyokua na ncha, walikuwepo mangwinji wa hiyo maneno wako wapi? kama unabisha muulize Ghadafi na wenzie, na mtalipwa hapa hapa kama sio nyie hata vizazi vyenu vitarithi hiyo laana, jaribuni kufuatilia vizazi vya machifu waliosimamia kuuza watumwa na kuuza nchi kwa wakoloni. Muwe na utu andika kitu usimujeruhi mwenzako, Siasa sio dhihaka wala kejeli ni maisha ya watu tunaongelea na mstakabala wa maisha yao ya hapa duniani na maandalizi ya maisha ya milele kwa Baba.
kwanini unasumbuka na watu wanaoishi kwa kuchumia tumbo ?
 
Kama wapinzani CUF hawatashiriki CCM wanashindana na nani? Na huyo atakayetangazwa kama mshindi atakuwa na haki ya kikatiba ya kuwaongoza wazanzibari?
 
.......hasara kwa mchukuzi.


Nina Ombi mkuu,

would you please do a favor kwa kuondoa hii picha hapo kwa avatar yako?

Ni ombi tu...sina maana ya kuingilia uhuru wako...samahani mkuu

upload_2016-3-18_12-14-22.png
 
Back
Top Bottom