Zanzibar: CUF hawaepukiki

Kama
wamefuta matokeo ya uchaguzi halali bila kutumia kifungu chochote cha sheria toka kwenye katiba au hata kanuni za uchaguzi, Shein atashindwa kuteua makamu wa Rais KWA KUTUMIA MAMLAKA ALIYOPEWA?
 
Makamu wa Rais atatoka kwenye chama UPDP kwani ndio wamepata mwakilishi mmoja kule Pemba. Yaani itakuwa serikali ya vichekesho a.k.a ya Mazuzu. Hivi Shein anajisikiaje atakapokuwa anaongoza serikali iliyowekwa madarakani pasi kuzingatia katiba?
 
Kwan matokeo ya wawakilishi yapoje kwa ujumla
 
Ninachokijua mimi ni ccm imefanya huu uchaguzi na ikijua nini kinatokea, na siyo imetokea kwa bahati mbaya kinachokuja sasa baada ya mataifa wahisani kuinyima misaada znz ambayo yenyewe haiwezi kujiendesha na kufanya maendeleo bila mkono wa nchi wahisani, sarakasi wanayokuja nayo ccm ni kutaka mwafaka na cuf lakini katika ajenda watakazo ongea suala la uchaguzi wa 25/10/2015 halitakuwepo kwenye ajenda ya muafaka, na usifikiri maghufuli kuwasema wanaccm kuhusu meya wa dar ni kuwa kachoka na siasa chafu za ccm la hasha hii kafanya ili apate huruma ya ukawa wamshauri seif akubaliane na matakwa ya ccm, kwani ukawa unanafasi kubwa ya kusikilizwa kuliko ccm na maghufuli, hapa nasubiri viongozi wa ukawa watasema nini juu ya hili?
 
kama hiyo akili ya magufuli basi,muafaka wa kisiasa ni ndoto kuwepo!
 
Jamani hivi nyie mnakaa nchi gani????
naona kila mtu anajiuliza kuhusu busara zitumike mara ooh katiba inasema,,,kweli?
kumbukeni ccm ni jabali lisilo na haya,, mtashangaa kila kitu wanafanya wao halafu sijui mtasema nini
 

MIMI NIJUACHO, ZANZIBAR HAITATAWALIKA. MAANA WAFUASI WA CUF HAWATAWASIKILIZA VIONGOZI WA CCM KUANZIA SHINANI HADI TAIFA. IN A WAY KUTAKUWA NA CIVIL DISOBIDIENCE. NA NI HATARI KWA UCHUMI NA MSTAKABALI WA ZANZIBAR KWA UJUMLA. NGOJEENI TUONI SI YETU MACHO.
 
Mzee Tupatupa nafikiri hizo asilimia wameziweka makusudi kwa sababu zao,wasingeshindwa kuweka 89%
 
Hivi maCCM kama yameikanyaga katiba tuliojiwekea ituongoze wakatangaza marudio ya uchaguz haramu yatashindwa kulazimisha kumzawadia hamad rashd umakamu ili kuficha aibu ya karne.
 
Kama hakuna aliyepata >10% ili awe makamu wa Rais wa SMZ basi, hakuna VP. Hakuna serikali ya mseto ila ni ccm full suit.

Kama mmeamua kususa manake hakuna mseto partner katiabmpira kwapani, ndio itatoka wapi tena uwezi oa mjomba wala shangazi sababu mwali kala kona maisha yanaendelea. Utaenda kuoa kwengine fursa itakapo patikana.
 
Unashindwa kuiuliza hiyohiyo katiba
Ikitokea mtu akapata 99%
pia inakuwaje??
hiyo katiba imeweka ukomo wa Asilimia kwa mshindi!?
HIVI unayajua hayavau ulokuwa unauliza uambiwe..?? Maana umeanza kama anayefahamu lakini umeishia kuonyesha hujui lolote kwenye hilo
 
Yaani nime kereka sana na hizi sarakasi za CCM, wanataka muafaka kwani hawakuwa wakijua wanachokifanya kitaleta matokeo ya aina gani!!?. Unafiki na uzandiki tu umewajaa, huyo Shein anahubiri muafaka na huyo mamluki wao Hamad Rashidi anahubiri muafaka ni kama vile walipanga kabla waseme nini.

Kama kweli kura walizopata ni halali wasi wasi ni wa nini!!?. Ci wajilie vyao huko Ikulu!?Wana majeshi wana vifaru wana mitutu ya bunduki wasi wasi ni wa nini kama sio unafik tu umewajaa.. Mnapoka matakwa ya wananchi kwa nguvu bado mnategemea uungwaji wa mikono!?.
 
Kama mmeamua kususa manake hakuna mseto partner katiabmpira kwapani, ndio itatoka wapi tena uwezi oa mjomba wala shangazi sababu mwali kala kona maisha yanaendelea. Utaenda kuoa kwengine fursa itakapo patikana.
kinachotakiwa kufuatwa ni katiba na si mitazamo kama wako...
 
Hamad Rashid alidhani..
1. Angekuwa mshindi wa pili
2. angepata 10%
hivyo angekuwa makamu wa kwanza wa raisi

Kwa sasa kazi wanayo
 
Ni kweli maana punda unaweza ukamfikisha mtoni lakini kunywa maji ikawa ishu... pale 100% ni maamuzi yake
 
Nadhani kwa miaka 20 sasa CUF imekua mstari wa mbele kutaka kujenga umoja.
Walikubali kuibiwa mara 4 na mara walisema wataitoaa lakini haikua hivyo ccm iko radhi nchi ivurudwe na majeshi ya tanganyika lakini hawako tayari kukaa benchi kwa njia za kikatiba.
Na hili CUF Wasahau hata kukiwa na mapatano gani hili ni donda ndugu...kupatana mtakua mnajihangaisha tu na wapenzi na wazanzibari watachoka watakata tamaa.
Nikiangalia Maalim anavopendwa na kusikilizwa namfananisha na Mahatma Ghandi. .
Ghandi alikua kipenzi cha wahindi kwenye struggle ya uhuru...na aliwaingoza wahindi katika falsafa yake ya peaceful struggle bila kupigana na Uingereza walisalim amri...
Hivyo Maalim unapendwa na wazanzibari
Wanajua umefanya kila kitu cha uwezo wako kuwaleta ccm kuwa nchii ni yetu sote na kila mtu ana haki sawa lakini ccm imechukua hati miliki ya utawala..wamegeuka masultani..hata kama watu hawawataki basi watakaa kwa jeshi.
Maalim our Ghandi its time to lead the strugle kwa peaceful disobidience mpaka usuluhishi wa kweli kutoma UN utapo kuja Zanzibar...hii ndo njia ilobaki..
Zaidi ya nini Ghandi alifanya msome falsafa yake...sasa hivi No to any mazungumzo...wakati wa mazunhumzo umepita
 
Unashindwa kuiuliza hiyohiyo katiba
Ikitokea mtu akapata 99%
pia inakuwaje??
hiyo katiba imeweka ukomo wa Asilimia kwa mshindi!?
We ni kilaza tu, ushindani wa CCM na CUF, nani anaweza kupata 99%
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…