Zakaria air bus yaua Sirari

Zakaria air bus yaua Sirari

Muwazi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2014
Posts
355
Reaction score
81
Kuna taarifa kuwa basi la Zakaria limeua watu 5 na wengine kadhaa kujeruhiwa huko Sirari ikiwa inatokea Sirari kwenda Mwanza leo asubuhi. Mwenye taarifa kamili atujuze.
 
Mh !!!! Hadi sasa hatujasikia hii!!
 
Kama unachafua jina la biashara ya watu???!!!!

Hata kama ni ajali,huwezi andika vingine???!!!

Kujenga jina sio lelemama jamani tuwe makini
 
Kama unachafua jina la biashara ya watu???!!!!

Hata kama ni ajali,huwezi andika vingine???!!!

Kujenga jina sio lelemama jamani tuwe makini

Sio kuchafua kama unavyofikiria OLESAIDIMU maana hapo nimesema tetesi nakuuliza kama kuna mwenye taarifa hizo atujuze.
 
Last edited by a moderator:
Kuna taarifa kuwa basi la Zakaria limeua watu 5 na wengine kadhaa kujeruhiwa huko Sirari ikiwa inatokea Sirari kwenda Mwanza leo asubuhi. Mwenye taarifa kamili atujuze.


Hao unaowategemea kukujuza hapa si wangeshapost thread kama ni tangia asubuhi?

Huenda ikawa uchakachuzi wa habari, kumbuka leo asubuhi wengine tumerudishiwa Namanga tukienda kumlilia Kibaki
 
Mkuu MUWAZI khabari hzo ni za kweli na Tumepoteza Sister katika Ajali hyo,Its too Sad tunataraji kumpumzisha leo 22/07.Mwanza Mjini Maeneo ya Nyakato
 
Mkuu MUWAZI khabari hzo ni za kweli na Tumepoteza Sister katika Ajali hyo,Its too Sad tunataraji kumpumzisha leo 22/07.Mwanza Mjini Maeneo ya Nyakato

Poleni sana Babaticha kwa msiba huo mlioupata. Tuko pamoja katika wakati huu mgumu. May she R.I.P
 
Last edited by a moderator:
Kama unachafua jina la biashara ya watu???!!!!

Hata kama ni ajali,huwezi andika vingine???!!!

Kujenga jina sio lelemama jamani tuwe makini

Taarifa hii ya ajali ni kweli ilitokea ila kwa taarifa ya R.F.A leo asubuhi ni kwamba alifariki mmoja na wengine watano kujeruhiwa na kulazwa katika hospitali ya Tarime.
 
Taarifa hii ya ajali ni kweli ilitokea ila kwa taarifa ya R.F.A leo asubuhi ni kwamba alifariki mmoja na wengine watano kujeruhiwa na kulazwa katika hospitali ya Tarime.
Haya pima kichwa cha habari yako!!!
 
Habari yangu inatofautiana na ndio maana nilisema ni tetesi na pia nikaomba wenye taarifa kamili watujuze OLESAIDIMU.

Sawa mkuu ila kwenye biashara ya abiria neno "kuua" lina athari kubwa kuliko linavyotamkika!!!!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom