Yuko wapi mbunge wangu Shibuda?

mastersajenti

Senior Member
Joined
Dec 4, 2015
Posts
165
Reaction score
24
Wadau mnijuze aliko mbunge wangu Mh.sana Shibuda .Mkuu huyu hakujua kuwa chadema yeye baadae amepotea kabisa kimya kimya.Chezea siasa wewe
 
Nimesoma leo ni mwenyekiti wa chama cha Ada-tadea na ni mwenyekiti wa umoja wa rufaa ya wananchi yupo na dovutwa fahmi nassoro
 
Siku hizi ni mwenyekiti wa Vyama visivyopata ruzuku Tanzania
 
Wadau mnijuze aliko mbunge wangu Mh.sana Shibuda .Mkuu huyu hakujua kuwa chadema yeye baadae amepotea kabisa kimya kimya.Chezea siasa wewe

Jimboni kwake ametolewa na mbunge wa ccm anaitwa Mashimba Joel Ndaki.huyo ndo mbunge wa hlo jimbo jawa sasa,Shibuda wametupa kule..
 
Huyo nae acha apotee,mtu gani hana msimamo na kujipendekeza kwingi kwa wakubwa,kazi ya kubomoa upinzani tu,acha atokomee,yeye si alisema ni zaidi ya chama!
ukiona umezaa mtoto ana kichwa kama cha mbunge wako huyu,basi umezaa zero upstairs
 
Ameenda kufundisha fasihi simulizi huko?
 
yupo anafuga ming'ombe huko maswa, alidhani kusaliti chama mchezo akale kiburi chake.
 
Ni katibu mkuu wa chama fulani mfu ambacho hakijawahi fanya mkutano mkuu na wala msajiri wa vyama vya siasa hana mpango nacho.
 
Nimesoma leo ni mwenyekiti wa chama cha Ada-tadea na ni mwenyekiti wa umoja wa rufaa ya wananchi yupo na dovutwa fahmi nassoro
Wamekutana na dovutwa woote wapiga dili... aiseee
 
Kaungana na wasaka tonge wenzake....
 
Nami naomba kuuliza, ivi yule mbunge aliwahi kutamka bungeni kwa kuwaambia wabunge wa upinzani wana ( ASHKI ) bado ni mbunge?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…