sifongo
JF-Expert Member
- Jun 5, 2011
- 4,895
- 5,308
Mbona povu mkuu?
Mara Manji mjinga, mara Manji sijui kitu gani mbona mnatapatapa? Matusi ya kumtukana mtu asiyehusika yanakujaje? Au wewe ndio umeamua kulikuza soka kwa maneno makali kwa mfadhili wetu?
Simba fanyeni mazoezi, mambo ya kumtafuta mchawi wala hayana tija. Timu zote zimejiandaa kushindana sasa kama mlitarajia ubwete sasa mmekumbana na mambo si mambo rudini mjipange, sio kutukana watu.
Y ang a Hoy eeeeeeeeeeeee!!!
Mkuu sitoki povu na sijasema manji ni mpumbavu direct nimesema kama kweli anahusika na hujuma za mgomo wa wachezaji wa Simba, hata mimi ni mshabiki wa Yanga lakini nataka timu yangu ishinde au kuchukua ubingwa kwa kuonyesha soka sio kuifanyia hujuma timu nyingine, hembu niambie kama mfadhili wenu atahonga timu za ndani na akachukua ubingwa vp mutakapokutana na timu kama nje, ataenda kuhonga na huko? na kama munaamini katika kuhonga na hujuma ina maana gani sasa munasajili wachezaji kwa bei mbaya ubora wao mutaujuaje?
Tunataka soka la kisasa, kama ambavyo wengi tunakwera na baadhi ya ushindi wa CCM kwakua wananunua shahada za kupigia kura pia tukerwe pia na hujuma kama hizi katika soka.