Yaliyojiri katika Mkutano wa CHADEMA, Mbeya

Yaliyojiri katika Mkutano wa CHADEMA, Mbeya

Mbeya hoyeee, duh hawa wanajitambua tangu kitambo jamani hii nyomi si ya kawaida
photo.JPG
HIKI CHAMA SI TULIAMBIWA KINAKUFA?
Hapo ndipo unapogundua akili za watabiri zilivyo ndogo
 
Mkuu hiyo picha ni original kweli Mbona kama jamaa vidonda vya tumbo vinaweza kuyibuka.ndungai eti akapiga kijembe eti watu wanashangaa Mbona bunge limetulia sana eti Kuna wabunge wameshauri adhabu iongezwe.
Mkuu unafikiri wao hawajutii uamuzi walichukua.Haya yanatokea sasa yanawaumiza sana.

Nafikiri kwenye picha hizo mmeona kuwa hakuna hata lori moja la kubebea watu ili kuwaleta mkutanoni.Watu wametembea kwa miguu kutoka maeneo mbalimbali ya jiji hadi viwanjani.

Nasikia Morogoro kulikuwa na usafiri wa kupeleka watu kwenye mkutano.Kwenye zile picha niliona malori,watu waliamua kuja nayo kama usafiri binafsi au ndo kama kawaida yetu kukubali kubebwa kwenye malori ili kwenda kusikiliza agenda za kuzungumzia CHADEMA.

KUNA SWALI LIMETOLEWA KWA WATANZANIA KAMA TUNAJIVUNIA KUWA WATANZANIA AU TUNAVUMILIA KUWA WATANZANIA? BY:WENJE.
 
Wakuu,

Leo CHADEMA wanafanya mkutano wa hadhara jimbo la Mbeya mjini, nia ni kuendelea kushtaki uonevu unao fanywa na kiti cha spika.

Mkutano unafanyika kwenye kiwanja maarufu kilicho pewa jina la DR slaa.

YANAYOJIRI:

• Maandamano makubwa yametusua katikati ya jiji la Mbeya.

• Watu ni wengi sana! Kama kawaida wanakuja kusikiliza kile wanacho kikosa kwenye vyama vingine.

• Dr slaa anaonekana ni kipenzi cha wana Mbeya! Naomba niweke hakiba ya maneno!

• Mkiti wa Mbeya Mjini, Mwambigija anafungua mkutano: watu wa Mbeya wasingemwelewa Mbunge wao Sugu iwapo asingeinuka bungeni kwenda kuzuia udhalimu na uminyaji haki wa kiti bungeni! Wasingemwelewa!

• Anasema muda wa CCM kutawala umesha-expire, kila mtu anajua hivyo. Amewataka polisi kuacha mpambano wa kuwania udiwani wa CHADEMA na CCM, wasiingilie kati kupendelea na kuibeba upande mmoja.

• Dkt. Slaa kailipua ikulu kwa matumizi ya kifisadi ya bil. 29, fedha ambazo zimewekwa kwenye kitengo kipya cha Presidential Delivery Beareu! Zingeweza kujenga madarasa 4142 Shule ya Msingi, 2071 sekondari, zahanati 580, vituo vya afya 290, bila kuwachangisha wananchi hata senti!

• Dkt. Slaa kamlipua Waziri wa Maji Maghembe kwa kujipelekea mradi wa maji wa bilioni 50 jimboni kwake, wkt miradi mingine ya maji nchi nzima imetengewa bil. 4 tu

• Dkt. Slaa amesema Mwakyembe alilazimisha kampuni ya CCM Jitegemee Trading Company, kupata zabuni kwenye eneo la CCM, SUKITA thamani ya bil. 10 kwa kauli ya kushnikiza ''tuwasaidieni tu''

attachment.php

photo.JPG

well done.........
 
Si walisema CDM ni chama cha kaskazini? Hivi Mbeya napo ni kaskazini?
 
mheshimiwa supika naomba muongozo,kuhusu hii dozi ya CDM wanayoigawa huku nje ya bunge bila kufuata kanuni tukufu za bunge lako😛eace:😛eace:😛eace:
 
Ombi langu kwa wanachadema wote na wananchi wote wanaotaka mabadiliko na maendeleo ya kweli tujitokeze kwa wingi kwenye kila chaguzi zinazoendelea na zitakazokuaja hapa nchini na siyo tu kujitokeza kwenye mikutano kama nilivyoona kwenye picha juzi kule iringa na jana mbeya kama tumeamua kuleta mabadiliko basi hatuna budi kujitokeza kwa wingi kwenye chaguzi na kupigia kura bila kununuliwa.

Kwa umati huu niliouna hapo mbeya ccm wanahaki ya kuogopa chadema.
 
Nawasihi sana CDM, sasa waanze kwenda ZANZIBAR. Mfano CDM iliweka mikutano Mwanza, Mbeya Na Iringa ambayo nimeisikiliza {niliweka extreme kwenye cm, nikampigia mtu aliyekuwa mkutanoni na kuisikiliza mikutano yote live}.. Viongozi hao wameongea mambo ya mbolea sana sana. CDM ikiongea Mtu unaelewa kitu inayoongelewa, nsikilizie CCM waongee utashangaa sana, Mtu unakuwa busy kusaka lau kitu kimoja tu uipendee CCM unakosa. Sisi tusio Na vyama Mara nyingi hatupendi kuwa biasis but tell me my Friend CCM utaisapot uanzie wapi?

Sasa hivi wamekuja Na Gia ya Kupambana Na CDM Kwa Matusi, tena wanajitapa "Ohoo ukiwaachia CDM wanajidai sana" so Ccm mmewaachia Cdm? Kwenye Nini ? So what!!?,.... solution mliyoiona ndio kuwamiminia matusi ya Nguoni?!?! Shit!! Hawa Ccm naamini anaewashauri ni shetani.

Back there, CDM Watumbue Jipu la Muungano, waelezee sintofaham zote zilizojificha Kuhusu yunion hiyo inayolalamikiwa, CDM waelezee A-Z Ya Serikali Tatu, faida Na hasara zake Wazanzibar waelewe hili..

Chonde chonde CDM Hapana kuongelea UDINI, Kwa Uzuri Wala ubaya.. Said Issa Mohamed, Jembe la Ukweli ambaye ni Makam Mwenyekiti CDM Zanzibar alishafafanua Kwa usahihi Na Unyoofu propaganda hii ya Udini Na kuimaliza sidhani Kama kuna haja ya kuinadi popote, Waachiwe CCM wenyewe wahangaike nayo iwatafune.. CCM inakufa vibaya!! TANU died silently lakini CCM inakufa vibaya dear...!!

Wazanzibar ni binaadam kama wewe Na mimi, unajua binaadam yeyote akiambiwa ukweli lazima auelewe Kwa Sababu ukweli ndio asili ya mwanadam Hata kama ni mwovu., CDM wakiongelea ukweli Wa Masuala ya Zanzibar pasipo kuwahadaa kama CCM wanavyofanya, Wala kuleta propaganda zenye Sumu lazima wananchi wote waikubali..

Mie nikwambieni propaganda Za Matusi, ugaidi, udini.. Nasema Hata Kama zingekuwa Za kweli still mwananchi hawezi kuziafiki Wala kuzisikiliza, mwananchi huyu mnyonge, kapigika, yuko chokambaya, Bado Na umaskini wake anadhulumiwa, Watoto wake wako home Kwa kukosa Ada, matibabu hapati Hata akipata amezungushwa mbaya, Hana pa kushtaki akidhulumiwa, kila ataposhtaki atageukwa Vibaya Na kujuta, Haki haipo popote, polisi Na raia ni paka Na panya, Mtu akiibiwa kitu, akipigwa, akigongwa Na gari, bora wamalizane wao Kwa wao ila mkithubutu kumpelekea Kesi yenu mlinda Amani mmekwisha, utasumbuliwa Na polisi zikutoke fedha ilihali wewe Ndo mshtaki[tena nowadays polisi Hata ile chembe ya waoga, haya , Aibu imepungua sana, SIO polisi wote ila wengi wao hawana Cha kuogopa, Mtu anakutupia namba haloo NITUMIE Kwenye hii Tigopesa au mpesa Wala haogopi, au akikunasa njiani akiingia Ndani ya GARI lako Na kuona chenji umeziweka mahali Ndani ya GARI utasikia "Nipe hizi hizi zinantosha" anaziokota mwenyewe zote huyo anashuka jamani??!!?]... Nchi hii? Halafu kitokee Chama Chenye majibu haya kisha Misukule flan waseme hao ni magaidi, Mara wadini ok wawe magaidi au wadini whatever tunawataka Kama watakubali kujaribu kutuondoa huku. Wakishindwa tutawatupa NJE Na kuchagua wengine kulikoni kuwarudisha nyie mlio prove kishindwa..
 
Back
Top Bottom