Ya Ridhiwani na mahakamani yameishia wapi?

Ya Ridhiwani na mahakamani yameishia wapi?

justo james

Member
Joined
Apr 29, 2011
Posts
7
Reaction score
0
Habari ya leo wana JF wenzangu, najua kwa sasa macho yote ya watz yapo kwenye suala la posho na tumesahau kabisa kuhusu mkwara aliowachimba DK. Slaa na Mch. Mtikila, ninachojiuliza ni mbona alitoa siku saba na kwamba wasipomuomba msamaha atakwenda mahakamani, mpaka leo siku saba hazijafika au? Mpaka leo sijaona yeyote kati ya hao akiomba msamaha wala Ridhiwani akienda mahakamani kuwashitaki. Inaonyesha walichosema ni ukweli mtupu. Nakumbuka Dk. Slaa alimwambia utakuwa umevunja rekodi ya mafisadi waliosema watatupeleka mahakamani wakaishia kukaa kimya. So nazidi kuiamini CDM kwamba hawakurupuki katika habari wanazowapa watz, wanajipanga kwanza na wanahakikisha kuwa data ni za kweli kisha wanazirusha hewani.
 
maana yake ni kuzidi kuonyesha uzuzu wa Watz, pia inapoteza heshima ya "first family" maana huyu ni mwanafamilia wa hii nafasi ya juu kwa sasa. Nasi wananchi wa kawaida inabidi tuwaangalie/tutawaangalia kama watoto wengine waliotangulia.
Mfano Rz1 vs Madaraka
 
Rev Mtikila naye vipi? Alinukuliwa akisema atampeleka yeye...ama kakatiwa kitu kidogo katulia?
 
Mahakamani sio mahali pa kukimbilia kama vile mtu anavyoingia msalani, unahitajika umakini katika ukusanyaji wa vielelezo na ushahidi wa kuuweka mahakamani. Nadhani dogo bado anajipanga kama yule jamaa wa Tembo Card Master Card. Tusubiri tuone.
 
Katoto haka katakuwa ni "kajizi'' isipokuwa wanaokashutumu juu ya huo ukwasi nao inaonekana hawana uhakika na data zao kutokana na habari za kuambiwa.Angepatikana mtu mwenye data madhubuti ningeweza kumsupport ili tusonge nako.Narudia tena "kamekaa kiwiziwizi" kama sio "kimjini mjini" na dalili yake ni kuwa kameamua kujipotezesha ili tukasahau kama kapo.Sorry kwa lugha hii kwani ningemkubali iwapo angetimiza tamko lake la siku saba.Vinginevyo ni MNAFIKI kabisa kwa alama hizi tatu katika imani yake:-
1.Kutoa ahadi na kutotimiza.
2.Kusema uongo na
3.Kutoaminika.
 
kesha data huyu anajuwa mziki wa mahakamani utafumua mambo mengi sna!!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom