Ya Kitwanga yanafanana na ya Makonda

Ya Kitwanga yanafanana na ya Makonda

mwanaone

JF-Expert Member
Joined
Apr 2, 2011
Posts
637
Reaction score
760
Uigizaji mtupu serikali ipo katika kujisafisha tu.

1: Hawataki Makonda afukuzwe kwa tuhuma za vyeti fake. Sababu kubwa ikiwa Bashite atafukuzwa kwa vyeti fake hii itaonyesha vetting wanayosema wanafanyiwa viongozi in mapungufu na waliohusika na kumfanyia vetting Makonda itabidi wawajibishwe.

2: Pili itaonekana usalama wa taifa hawafanyi kazi yao ipasavyo na Rais ni rahisi kudanganywa na wasaidizi wake. Hii ni kashfa kwa Magufuli maana yeye anajifanya hawezi kudanganywa. Makonda alimdangamya Rais kwa kujifanya anapigana vita ya madawa kumbe anapigana na vita binafsi.

3: Ili Rais asiaibike inabidi itafutwe scandal kama ile ya Kitwanga ili apate sababu nyingine ya kumfukuza Ili Rais asionekane amekosea kwa muda mrefu.
Hili la Clouds limepangwa na usalama wa taifa na Makonda maksudi Ili kumpa Rais sababu nyingine ya kumfukuza Makonda.

4: Makonda angefukuzwa kwa ajili ya vyeti fake ilibidi au itabidi apelekwe mahakamani na ushahidi upo wazi Makonda angefungwa.

5: Makonda angefukuzwa kwa kashafa ya kuhongwa na watuhumiwa wa madawa ambapo ushahidi upo wazi ni kesi ya mahakamani na angefungwa.

6: Kwa ufupi hii kashfa ya Clouds ni kumnusuru Makonda na kifungo kama walivyofanya kwa Kitwanga.
 
Wakuu mnaona shida ipo wapi?
Kwanini Magufuli aliweza kumfuta kazi Rafiki yake wa siku nyingi, sasa anashindwa huyu aliyekutana naye huku mjini juzijuzi tu?
 
Hii kashfa ya Makonda haitozimwa kwa kutumbuliwa tu Bali tunataka apelekwe mahakamani
 
Mafia mobb wa cicily wanawatoza watu mashuhuri kodi kwa ajili ya usalama wao na mali zao. Ukienda kushitaki vyombo vya dola taarifa zinawafikia mafia siku hiyohiyo na unaongezewa kodi mara mbili ukikataa mali zako zinaporwa au zinateketezwa au wewe na familia yako mtauawa kulingana na jopo lao litakavyoamua.
Wanakutajia mali zako zote na pato lako kwa mwezi na wanakuomba uwape 1% tu ya pato lako lako kwa mwezi.
Mambo anayofanya bashite ni ya kimafia, anamtawala rais na sasa anataka vyombo vya dola vimtii yeye. Tupaze kelele bunge na mahakama vimuwajibishe kabla mtandao wake wa kiuhalifu haujawa mpana zaidi
 
Huu ni utawala wa kulindana Kama mkuu alivyosema "nitawalinda wastaafu" Mimi nashauri angesema tu nitawalinda ninaowapenda wote hata wakifanya makosa
 
Mkuu kwani hapo hawezi kufungwa na ushahidi upo wazi kabisa?? Kosa la kuvamia ofisi ya watu with armed men tunaweza ongezea na kosa la kutishia watu maisha sababu wanasema alitumia hao askari kuwatishia watu maisha yao. Me siamini kama huu ni mchezo uliopangwa. Huyu jamaa anachanganyikiwa kila siku aiseh duuh.
 
Mkuu kwani hapo hawezi kufungwa na ushahidi upo wazi kabisa?? Kosa la kuvamia ofisi ya watu with armed men tunaweza ongezea na kosa la kutishia watu maisha sababu wanasema alitumia hao askari kuwatishia watu maisha yao. Me siamini kama huu ni mchezo uliopangwa. Huyu jamaa anachanganyikiwa kila siku aiseh duuh.
Hao ni polisi Na wanajeshi sheria zipo chini Yao.
 
Uko sawa kabisa wanataka kutuletea mambo ya movie hapo wapotezee swala la vyeti feki eti tunataka hatua zaid ile iliyofanyika ni jinai na wale askar nao tena na bunduki waliwe tu ili iwe fundisho..kamuvi ka bashite ngja tuone
 
Kufukuzwa u-RC kwangu mimi naona ni adhahu tosha kwa makonda sababu alijisahau sana, hayo ya mahakaman watajuana wenyewe wanasiasa
 
Wakuu mnaona shida ipo wapi?
Kwanini Magufuli aliweza kumfuta kazi Rafiki yake wa siku nyingi, sasa anashindwa huyu aliyekutana naye huku mjini juzijuzi tu?
Labda kuna Siri ambayo bashite anaijua ya mkuu
 
Hii series jamani mbona kama inakaribia kuisha wakati wadau ndio kwanza tuko addicted, I hope kuna season 2.
 
Saa nyengine Hili suala bashite napata fikra linaachwa liwe hivi kwa kuwa kidogo linatupotezea muda Na kutusahaulisha hali ngumu ya uchumi tuliyonayo Na utekelezaji hafifu wa ahadi za mkuu
 
Makonda hakufanyiwa Vetting just alichaguliwa tu ukuu wa wilaya na hao unaosema hawakufanya vetting walisema lakini nothing done
 
JF raha sana cha muhimu ni kuwa na bando tu yaani full episode hii nchi bhana tamthilia tupu
 
Bashite amejaaliwa akili za ujanja, alipoona ccm wanakutana dodoma akaenda SA ili wajumbe waache kumzungumzia wajue amekimbia. Mkutano ulipoisha amerudi anaendeleza ubabe.
 
wamfukuze kwa ile kashfa ya kupewa viwanja kigamboni kimagumashi basi
 
Back
Top Bottom