WOSIA huu ni halalai au Batili? Je mambo gani yanaweza kubatilisha wosia?

kidadari

JF-Expert Member
Jul 26, 2012
8,647
9,574
Habari Ndugu naomba mwongozo katika uandishi wa wosia.Marehemu kaacha wosia kama ifuatavyo.
Marehem alikua na watoto 4 na kwa mke mmoja, wosia ukaaandikwa Mali zake zigawanywe kwa watoto 3 (majina yametajwa) na mke 1 na kila mtoto ameandikiwa mali atayorithi ISIPOKUA mtoto mmoja(1),
Wakati wosia unaandikwa mtoto huyo alikua ameshazaliwa.
-Tarehe ya wosia ipo
-mashahidi 3 walioshuhudia wosia ukiandikwa wapo hai
-sahihi za mashahidi na mtoa wosio zipo.
NB: Mambo gani yanaweza kunatilisha wosia wa marehemu?
 
Wewe elewa kwamba mali ni zake, hata angeamua kuzigawa zote kwa watoto yatima anaruhusiwa, so as long as watoto wake ni above 18yrs na hawako chini ya uangalizi wa baba yao na hawajibiki nao tena kisheria.
 
Huo wosiah hautambuliki mbele ya macho ya sheria, marehemu atleast angemrithisha ata saa ya ukutani uyo mtoto mmoja....invalid will,objection moja tu hapo wosiah chali.
 
Habari Ndugu naomba mwongozo katika uandishi wa wosia.Marehemu kaacha wosia kama ifuatavyo.
Marehem alikua na watoto 4 na kwa mke mmoja, wosia ukaaandikwa Mali zake zigawanywe kwa watoto 3 (majina yametajwa) na mke 1 na kila mtoto ameandikiwa mali atayorithi ISIPOKUA mtoto mmoja(1),
Wakati wosia unaandikwa mtoto huyo alikua ameshazaliwa.
-Tarehe ya wosia ipo
-mashahidi 3 walioshuhudia wosia ukiandikwa wapo hai
-sahihi za mashahidi na mtoa wosio zipo.
NB: Mambo gani yanaweza kunatilisha wosia wa marehemu?
Kama ameshagawa mali kwa wosia , kubatilisha labda afufuke aandike upya
 
Huo wosiah hautambuliki mbele ya macho ya sheria, marehemu atleast angemrithisha ata saa ya ukutani uyo mtoto mmoja....invalid will,objection moja tu hapo wosiah chali.
Kama mtoto ni above 18yrs mzazi halazimiki kumuachia urithi, maana kisheria hawajibiki nae tena.
 
Wewe elewa kwamba mali ni zake, hata angeamua kuzigawa zote kwa watoto yatima anaruhusiwa, so as long as watoto wake ni above 18yrs na hawako chini ya uangalizi wa baba yao na hawajibiki nao tena kisheria.

Hapo linakuja swali la msingi. Why alimleta duniani huyo mtoto ambaye hampendi na ambaye hajaandikiwa urithi.? Jibu ni simple, maadam amemleta duniani na ni damu yake, basi ana wajibika wa kumuachia urithi kila aliyemleta duniani. Hata iweje, hata huyo mtoto awe ametenda kosa kubwa kiasi gani kwa mzazi wake, swala la mzazi kumuachia urithi halikwepeki.

Kesi nyepesi sana hiyo ikipelekwa mahakamani. Na wote watarithi sawasawa.
 
Hapo linakuja swali la msingi. Why alimleta duniani huyo mtoto ambaye hampendi na ambaye hajaandikiwa urithi.? Jibu ni simple, maadam amemleta duniani na ni damu yake, basi ana wajibika wa kumuachia urithi kila aliyemleta duniani. Hata iweje, hata huyo mtoto awe ametenda kosa kubwa kiasi gani kwa mzazi wake, swala la mzazi kumuachia urithi halikwepeki.

Kesi nyepesi sana hiyo ikipelekwa mahakamani. Na wote watarithi sawasawa.
Labda kama huyo aliyenyimwa urithi hayuko of legal weaned age, yaani ni under 18yrs na mzazi awe hai au amekufa anawajibika kumtunza kisheria, so kama mzazi amefariki basi mali za mzazi zinatakiwa zimlee hadi afike 18yrs ndio ziende kwingine.
 
Ka kwambia nani? Na umejuaje kama uyo mtoto yuko above 18?
Nimesema kama yuko above 18yrs. Ila kama huyo mtoto yuko under 18yrs basi huo urithi ni batili, maana bado ana haki ya kisheria ya kulelewa na mzazi wake, hata kama amekufa, mali zake zinatakiwa zimlee, zimsomeshe nk.
 
Sheria ya mirathi inasemaje pindi baba anapofariki na kikao cha familia kikampitisha mama kuwa msimamizi wa mirathi, ila ikatoa kutofautiana kati ya mtoto mmoja na mama ambaye ni above 18 yrs ivyo kupelekea kudai chake mapema kwa kumpeleka mama yake mahakamani?
 
Labda kama huyo aliyenyimwa urithi hayuko of legal weaned age, yaani ni under 18yrs na mzazi awe hai au amekufa anawajibika kumtunza kisheria, so kama mzazi amefariki basi mali za mzazi zinatakiwa zimlee hadi afike 18yrs ndio ziende kwingine.

Hilo uliloliandika hapo ni sawa, ila swala la mtoto kutopata urithi toka kwa mzazi wake wa kumzaa ni halipo. Lazima atarithi tuu provided yule mzazi kaacha mali. Though urithi unaweza usigawanywe sawa kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo umri, ulemavu na uhitaji wa msaada kiujumla wake.
 
Hilo uliloliandika hapo ni sawa, ila swala la mtoto kutopata urithi toka kwa mzazi wake wa kumzaa ni halipo. Lazima atarithi tuu provided yule mzazi kaacha mali. Though urithi unaweza usigawanywe sawa kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo umri, ulemavu na uhitaji wa msaada kiujumla wake.
Hahah, wewe unachekesha, ikiwa hivyo utashangaa watoto 10 wa nje ya ndoa wanajitokeza ilihali watoto wa ndoa ni wawili tu ambao mama yao ndio alishirikiana na baba yao kuchuma mali hawapati kitu. Inabidi baba mwenyewe aandike wosia kwamba ana watoto wa nje ya ndoa kadhaa na wapatiwe urithi kiasi kadhaa.
 
Hapo linakuja swali la msingi. Why alimleta duniani huyo mtoto ambaye hampendi na ambaye hajaandikiwa urithi.? Jibu ni simple, maadam amemleta duniani na ni damu yake, basi ana wajibika wa kumuachia urithi kila aliyemleta duniani. Hata iweje, hata huyo mtoto awe ametenda kosa kubwa kiasi gani kwa mzazi wake, swala la mzazi kumuachia urithi halikwepeki.

Kesi nyepesi sana hiyo ikipelekwa mahakamani. Na wote watarithi sawasawa.
Sheria za wosia zinataka uwe siri sasa hapo ndo shida inaanza na aliyeandika ameshafariki
 
Hapo linakuja swali la msingi. Why alimleta duniani huyo mtoto ambaye hampendi na ambaye hajaandikiwa urithi.? Jibu ni simple, maadam amemleta duniani na ni damu yake, basi ana wajibika wa kumuachia urithi kila aliyemleta duniani. Hata iweje, hata huyo mtoto awe ametenda kosa kubwa kiasi gani kwa mzazi wake, swala la mzazi kumuachia urithi halikwepeki.

Kesi nyepesi sana hiyo ikipelekwa mahakamani. Na wote watarithi sawasawa.
Kama ni lazima apate wakati mwenye mali kaacha wosia asipate kuna haja gani ya wosia kama haueshimiwi?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom