ngoshwe
JF-Expert Member
- Mar 31, 2009
- 4,131
- 931
Nimeungana na watanzania wengine wakereketwa wa nchi hii kufuatilia majadiliano yanayoendelea katika kongamano la "WEF, 2010".
http://www.weforum.org/en/events/WorldEconomicForumonAfrica2010/Webcasts/index.htm
Najaribu kupambanua jinsi gani viongozi wetu walivyo na upeo tofauti wa kutazama, kuyaelezea na kuyatafutia ufumbuzi matatizo mengi ya nchi zetu za kiafrika. Inasikitisha sana kuona wapo viongozi ambao wana mtazamo wa juu kabisa kwa maendeleo ya nchi zao na kuna wale ambao ni dhahiri kabisa wanatumia muda mwingi kuyatangaza matatizo ya nchi zao ambayo wanayajua na yapo kwenye ilan na mikakati ya maendeleo kama nguzo ya kuwajenga kisiasa zaidi na kujipatia umaarufu wa kuongea tuuuuu pasipo hatua madhubuti za kuyakwamua.
Kwa mfano, wakati uchumi wa Tanzania unategemea zaidi ya asilimia 80% kwenye kilimo, nashangaa kusikia Mhe. Rais wetu anasema kuwa kwa sasa moja ya vipaumbele ni kuongeza uwezo wa Hifadhi ya Taifa ya Chakula (National Food Serves ) kwa kuwa tulishindwa kuwasidia wenzetu wa Kenya walipoomba msaada. Kwa mtazamo wa kiuchumi, ina maanisha kuwa Serikali imejikita zaidi katika kuhifadhi ziada bila kuwa na mikakati madhubuti ya kuwasaidia wakulima kuzalisha kuzalisha ili kupata hiyo ziada ya kuweza hata kuhifadhi kwenye hizo Hifadhi za Taifa za Chakula.
Ukifuatilia kumbukumbu za matukio, unaweza kuona kuwa hata hiyo Hifadhi za Taifa za Chakula (National Food Reserve) imekuwa ikitumika tu kuhifadhi mazao aina ya nafaka (sana ni mahindi) tena pasipo kutimiza lengo na mbaya zaidi imekuwa ikitumiwa na wanasiasa kwa ajili ya kujipatia umaarufu hata katika kipindi ambacho hakuna njaa. Hifadhi hiyo ya chakula imekuwa pia ikitumiwa kama ghala la chakula cha misadaa wakati wa maafa zaidi na kupoteza maana yake halisi ikiwemo kusaidia kuongeza uzalishaji kwa wakulima kwa kusukuma bei za wafanyabishara binafsi na kuwa na mazao mbadala ya kuhifadhi zaidi ya mahindi..
Isitoshe, kwa muda mrefu nchi yetu pia imeshidwa kumudu hata kukabiliana na maafa kupitia hiyo hifadhi ya chakula ya taifa na imekuwa ikitegeme pia kuagiza mahindi kutoka nje ya nchi kupitia wafanyabiashara binafsi ili kuhifadhi pia kwenye hiyo Hifadhi ya chakula (ikumbukwe pia si zaidi ya miaka saba imepita, Serikali imewahi kununua mahindi kutoka kwa majirani zetu wa Kenya "National Cereal Board" nchi ambayo haina uwezo wowote wa kuzalisha chakula kuliko Tanzania kutokana na rasimimali zake na kwa sasa hao wakenya wapo wengi hapa nchini wakinunua mzao kwa staili tofauti kwenda kuuza nje. Pia tumewahi kuagiza si mara moja mahindi toka Marekani na kwingineko duniani kwa maana kuwa hatujajitosheleza kiuzalishaji wa ndani.
Kwa maana nyingine ni kuwa, hatuwezi kuwa na ngo la kuongeza uwezo wa Hifadhi ya Taifa ya Chakula ambayo haiendani na lengo la kuwafanya wakulima wetu kuzalisha ziada, ikwemo kutowasaidia wakulima hao kuongeza ukubwa wa mashamba yao, kutumia mbinu bora za kilimo, kulima kilimo cha kibiashara na kadhalika. Vinginevyo, itakuwa ni kuishia kuwafanya wakulima wakose soko la maana kwa kuwa tuna njaa ya kitaifa na kuwazuia kuuza mazao yao nje ya nchi pale tunapodhani tuna njaa wakati ambao hatujawasaidia kwa mtaji wowote kuzalisha.
Wakati kwa wenzetu wa Malawi wanaelezea mafanikio makubwa katika kilimo kufuatia uamuzi wa Serikali yao kutoa ruzuku ya pembejeo kwa wakulima kuanzia mwaka 2005, Tanzania ambayo imekuwa ikitoa ruzuku hiyo kwa wakulima tokea mwaka 2003, imeshindwa kabisa kuelezea mafanikio yoyte ya ruzuku hiyo ya pembejeo ambayo imekuwa ikitumia fedha nyingi za umma sasa kupitia mfumo wa vocha (Voucher system). Badala yake tunajififia kwa kuongeza wagani (extension officers) ambao wanaenda kusimamia wakulima wasio na mtaji,mashamba ya kueleweka, miundo mbinu ya umwagiliaji wala mfumo bora wa masoko!...
Mtazamo wangu ni kuwa labda matatizo yanayofahamika kwetu huwa ndio yanatumika kwa ajili ya kuombea kura tu. Yaani hatuwezi kujifunza kutoka kwa wenzetu?.
http://www.weforum.org/en/events/WorldEconomicForumonAfrica2010/Webcasts/index.htm
Najaribu kupambanua jinsi gani viongozi wetu walivyo na upeo tofauti wa kutazama, kuyaelezea na kuyatafutia ufumbuzi matatizo mengi ya nchi zetu za kiafrika. Inasikitisha sana kuona wapo viongozi ambao wana mtazamo wa juu kabisa kwa maendeleo ya nchi zao na kuna wale ambao ni dhahiri kabisa wanatumia muda mwingi kuyatangaza matatizo ya nchi zao ambayo wanayajua na yapo kwenye ilan na mikakati ya maendeleo kama nguzo ya kuwajenga kisiasa zaidi na kujipatia umaarufu wa kuongea tuuuuu pasipo hatua madhubuti za kuyakwamua.
Kwa mfano, wakati uchumi wa Tanzania unategemea zaidi ya asilimia 80% kwenye kilimo, nashangaa kusikia Mhe. Rais wetu anasema kuwa kwa sasa moja ya vipaumbele ni kuongeza uwezo wa Hifadhi ya Taifa ya Chakula (National Food Serves ) kwa kuwa tulishindwa kuwasidia wenzetu wa Kenya walipoomba msaada. Kwa mtazamo wa kiuchumi, ina maanisha kuwa Serikali imejikita zaidi katika kuhifadhi ziada bila kuwa na mikakati madhubuti ya kuwasaidia wakulima kuzalisha kuzalisha ili kupata hiyo ziada ya kuweza hata kuhifadhi kwenye hizo Hifadhi za Taifa za Chakula.
Ukifuatilia kumbukumbu za matukio, unaweza kuona kuwa hata hiyo Hifadhi za Taifa za Chakula (National Food Reserve) imekuwa ikitumika tu kuhifadhi mazao aina ya nafaka (sana ni mahindi) tena pasipo kutimiza lengo na mbaya zaidi imekuwa ikitumiwa na wanasiasa kwa ajili ya kujipatia umaarufu hata katika kipindi ambacho hakuna njaa. Hifadhi hiyo ya chakula imekuwa pia ikitumiwa kama ghala la chakula cha misadaa wakati wa maafa zaidi na kupoteza maana yake halisi ikiwemo kusaidia kuongeza uzalishaji kwa wakulima kwa kusukuma bei za wafanyabishara binafsi na kuwa na mazao mbadala ya kuhifadhi zaidi ya mahindi..
Isitoshe, kwa muda mrefu nchi yetu pia imeshidwa kumudu hata kukabiliana na maafa kupitia hiyo hifadhi ya chakula ya taifa na imekuwa ikitegeme pia kuagiza mahindi kutoka nje ya nchi kupitia wafanyabiashara binafsi ili kuhifadhi pia kwenye hiyo Hifadhi ya chakula (ikumbukwe pia si zaidi ya miaka saba imepita, Serikali imewahi kununua mahindi kutoka kwa majirani zetu wa Kenya "National Cereal Board" nchi ambayo haina uwezo wowote wa kuzalisha chakula kuliko Tanzania kutokana na rasimimali zake na kwa sasa hao wakenya wapo wengi hapa nchini wakinunua mzao kwa staili tofauti kwenda kuuza nje. Pia tumewahi kuagiza si mara moja mahindi toka Marekani na kwingineko duniani kwa maana kuwa hatujajitosheleza kiuzalishaji wa ndani.
Kwa maana nyingine ni kuwa, hatuwezi kuwa na ngo la kuongeza uwezo wa Hifadhi ya Taifa ya Chakula ambayo haiendani na lengo la kuwafanya wakulima wetu kuzalisha ziada, ikwemo kutowasaidia wakulima hao kuongeza ukubwa wa mashamba yao, kutumia mbinu bora za kilimo, kulima kilimo cha kibiashara na kadhalika. Vinginevyo, itakuwa ni kuishia kuwafanya wakulima wakose soko la maana kwa kuwa tuna njaa ya kitaifa na kuwazuia kuuza mazao yao nje ya nchi pale tunapodhani tuna njaa wakati ambao hatujawasaidia kwa mtaji wowote kuzalisha.
Wakati kwa wenzetu wa Malawi wanaelezea mafanikio makubwa katika kilimo kufuatia uamuzi wa Serikali yao kutoa ruzuku ya pembejeo kwa wakulima kuanzia mwaka 2005, Tanzania ambayo imekuwa ikitoa ruzuku hiyo kwa wakulima tokea mwaka 2003, imeshindwa kabisa kuelezea mafanikio yoyte ya ruzuku hiyo ya pembejeo ambayo imekuwa ikitumia fedha nyingi za umma sasa kupitia mfumo wa vocha (Voucher system). Badala yake tunajififia kwa kuongeza wagani (extension officers) ambao wanaenda kusimamia wakulima wasio na mtaji,mashamba ya kueleweka, miundo mbinu ya umwagiliaji wala mfumo bora wa masoko!...
Mtazamo wangu ni kuwa labda matatizo yanayofahamika kwetu huwa ndio yanatumika kwa ajili ya kuombea kura tu. Yaani hatuwezi kujifunza kutoka kwa wenzetu?.