WIZI

kunze

JF-Expert Member
Joined
Nov 22, 2016
Posts
398
Reaction score
470
Toka kwa mama yangu Heriety Chumira, Habarini za asubuhi wapendwa wangu? Huyu kaka anaitwa Zuberi Auli Zuberi, binti yangu jana jioni saa 12 alirequest bolt kutoka Yombo kwenda Kinyerezi, unaporequest inatokea picha na namba ya dereva kwa bahati nzuri binti yangu alimfananisha dereva na kaka wa rafiki yake hivyo akasrceen shoti hiyo picha na kumtumia rafiki yakr kumuuliza kama huyo ni kaka yake, kumbe ni Mungu tu alitaka picha ya kaka awe nayo, walivyofika mitaa sitakishari akawa anampitisha njia za vichochoroni hali imliyomtia wasiwasi binti yangu na kumuuliza kulikoni wanapita njia za ndani ndani wakati barabarani hakuna foleni dereva akadai anaogopa traffic kwakuwa hana leseni, kufika mbele kidogo akazima gari na kusema anahisi mafuta yameisha binti yangu akaanza kupata wasiwasi na kumuuliza dereva kulikoni lakini akamwambia binti yangu ashuke asukume hili ikiwaka wafike barabarani kuna petrol station baada ya binti yangu kushuka dereva aliwasha gari akaondoka ndani kukiwa na pochi yenye oesa, simu mbili vitambulisho vya benki ya CRDB, NMB, Kitambulisho cha Taifa chake na cha binti yake na documents mbalimbali. Amefungua kesi STK/RB/9567/3921 kituo cha polisi sitaki shari Heriety Chumira] @jenniferkyaka @wema_emily @halimayahya
 
Sijui tutaponea wapi, haya tunaomba apatikane mwehu huyo.
 
Mmeripoti Bolt?
 
Wabongo uaminigu 0
 
Kuna wizi unafanyika siku hizi... wezi wanazunguka na magari wakikuona umesimama mkao wa kuita Uber au hizo Bolt wanajifanya ndio wao umewaita...wanafanya hivi sababu wanajua kuna watu hawako makini kwenye kuverify usahihi wa dereva au aina ya gari. Sasa ukipanda tu gari ndio unakutana na haya yaliyompata huyo mhusika wa huu wizi. Ndio maana nikauliza kabla ya kushtaki polisi je mliwasiliana na Bolt kujua kama wanamtambua huyo Dereva?
 
Swali muhimu...
 
Mi maswala ya Bolt/Uber etc huwa nawaza sana wale wanaowasaidia wengine kwa nia njema kuwaombea usafiri huo, kisha mwombaji hapandi wanapanda wengine. Tatizo likitokea linaleta picha ingine ya hatari
 
Sasa hivi nchi yetu imejaa majizi na matapeli, Mshana Jr naye hataki kusaidia na yale mambo yake! Hawa jamaa ni wa kupiga vipapai tu! Juzi wamekimbia na 2m yangu kwenye bag, nawaza nimwachie Mungu au niwapeleke Sumbawanga?
 
Pia ni vema unapoita usafiri kabla hujapanda unapiga picha aina ya gar na namba zitakusaidia kama utapata tatizo ukifika salama delete ipo mkuuu safi
 
Doesn't make sense! Ndio maana wanatuma na picha ya dereva kuepuka ujinga huo!
 
Miye naogopa sana gari ya peke yangu bora nipande mikweche ya jumuia.
 
Doesn't make sense! Ndio maana wanatuma na picha ya dereva kuepuka ujinga huo!
Kama umesoma vizuri nilichoandika na umeelewa basi utaelewa pia nilichomaanisha. Ni wizi unafanyika sana haswa usiku kwenye maeneo ya starehe. Unaita isafiri lakini cha ajabu inakuja gari nyingine kabisaa kunifamya yenyewe ndio umeiita sasa hapo usipokagua tu imekula kwako. Nimeshuhidia wengi wamelizwa kwa hii style.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…