telex
JF-Expert Member
- Apr 26, 2015
- 406
- 103
Wizi ktk mabasi ya mikoani hasahasa katika kituo kikuu cha mabasi ubungo umekua ni kero isiyo na tiba kutokana na ubunifu unaojitokeza kila kukicha.
Leo asubuhi dada mmoja aliekua akisafiri na basi moja kutoka dar es salaam kwenda mkoani mbeya amejikuta akilia kama mtoto baada ya kuibiwa simu yake ya gharama ndani ya basi hilo.
Ilikuwa hivi;
Dada huyo aliekua amekaa siti moja na kijana mmoja mtanashati na mwenye umbo la unene, kijana huyo ambae alilipa nauli ya watu wawili huku akimweleza kondakta kua yupo mwenzake atapandia kibaha maili moja, huku jamaa huyo akiwa bize kuwasiliana na huyo wa kibaha gafla alimwomba abiria mwenzake simu yake ili aendelee kuwasiliana na mwenzake kwani simu yake ilizima chaji.
Dada wa watu pasipo kujua anaibiwa alitoa simu yake ndogo aina ya nokia tochi akampatia jamaa mawasiliano yakaendelea mpaka dakika zikaisha, dada wa watu kwa huruma ya kitanzania huku gari ikiingia stendi maili moja akatoa simu yake kubwa (smartphone) akampatia jamaa ili amuelekeze ndugu yake gari ilipo, jamaa akionekana kuingiwa na jazba na hasira mpaka akasimama ili angalie nje na simu ikiwa sikioni akimwambia mwenzake njoo kwenye geti la kutokea gari inakaribia kutoka fanya haraka.
Jamaa alipoona gari inatoka alisimama kutoka kwenye kiti na simu sikioni na kushuka kwenye gari huku akimsihi dereva amsubiri kwani anaenda kumfuata mwenzake.
Dereva alisogeza basi hadi kwenye kituo cha crdb kibaha kwa lengo la kusubiri abiria wake. Huku tukiwa tunasubiri ndipo akasimama dada huyo na kudai kua jamaa kashuka na simu yake ya bei mbaya.
Takribani dakika kumi tulisubiri jamaa hakurudi safari yetu ikaendelea..
Nawasilisha.
Leo asubuhi dada mmoja aliekua akisafiri na basi moja kutoka dar es salaam kwenda mkoani mbeya amejikuta akilia kama mtoto baada ya kuibiwa simu yake ya gharama ndani ya basi hilo.
Ilikuwa hivi;
Dada huyo aliekua amekaa siti moja na kijana mmoja mtanashati na mwenye umbo la unene, kijana huyo ambae alilipa nauli ya watu wawili huku akimweleza kondakta kua yupo mwenzake atapandia kibaha maili moja, huku jamaa huyo akiwa bize kuwasiliana na huyo wa kibaha gafla alimwomba abiria mwenzake simu yake ili aendelee kuwasiliana na mwenzake kwani simu yake ilizima chaji.
Dada wa watu pasipo kujua anaibiwa alitoa simu yake ndogo aina ya nokia tochi akampatia jamaa mawasiliano yakaendelea mpaka dakika zikaisha, dada wa watu kwa huruma ya kitanzania huku gari ikiingia stendi maili moja akatoa simu yake kubwa (smartphone) akampatia jamaa ili amuelekeze ndugu yake gari ilipo, jamaa akionekana kuingiwa na jazba na hasira mpaka akasimama ili angalie nje na simu ikiwa sikioni akimwambia mwenzake njoo kwenye geti la kutokea gari inakaribia kutoka fanya haraka.
Jamaa alipoona gari inatoka alisimama kutoka kwenye kiti na simu sikioni na kushuka kwenye gari huku akimsihi dereva amsubiri kwani anaenda kumfuata mwenzake.
Dereva alisogeza basi hadi kwenye kituo cha crdb kibaha kwa lengo la kusubiri abiria wake. Huku tukiwa tunasubiri ndipo akasimama dada huyo na kudai kua jamaa kashuka na simu yake ya bei mbaya.
Takribani dakika kumi tulisubiri jamaa hakurudi safari yetu ikaendelea..
Nawasilisha.