Wakuu kama jamaa alivyosema hapo awali kuwa unapoenda sehemu mfano kuuza chombo chochote cha moto mfano pikipiki na gari inatakiwa muwe angalau wawili na sio peke yako,,,,
Kuna huu ushuhuda hapa na mimi ulinitokea pale sinza kijiweni kuna mtu alinipigia simu mi nikiwa zangu hapa chuoni st.joseph kwamba kaiona pikipiki yangu boxer kwenye mtandao wa kupatana na anahitaji kuichukua na kanambia nikutane na jamaa yake ambaye ni fundi wa pikipiki pale sinza kijiweni na kwamba yeye yupo kikazi jeshini kibaha na kasema maagizo yote amemuachia huyo jamaa yake basi mi nikajitolea nikamfuata na dereva wangu huko sinza kijiweni tulipofika hapo nikampigia simu huyo fundi ambaye namba zake nilipewa na boss wake aliyepo kibaha jeshini kweli nikamkuta huyo fundi pikipiki anatusubiria na alikuwa na rafiki yake ndipo wakaiangalia hiyo pikipiki yangu na wakaikagua vizuri na sisi tulikuwa wawili na wao walikuwa wawili jumla wanne ndipo mmoja ambaye ni fundi akasema tutangulie naye na ndiye kaagizwa na boss wake so tukampakiza kwenye pikipiki yangu tukaenda maeneo fulani hivi sipakumbuki kwa jina maana mimi nilikuwa mgeni maeneo hayo na tulipofika sehemu fulani yule jamaa ambaye ni fundi tuliyekuwa tumembeba kwenye pikipiki kasema tupaki maeneo hayo ili amuangalie mdogo wake na huyo bosi aliyemwagizia ndipo yeye kashuka kwenye pikipiki nikamuona anaelekea chumba fulani hivi kiko kama baa na alipoingia humo ndani alikaa wakiongea na huyo mdogo wake na boss kama dakika tano hivi na baada ya hapo nikawaona wakitoka nje na huyo mdogo wake na boss alipokuja na kuzungumza nasi alisema kuwa ela ya kununulia hiyo pikipiki ameachiwa mke wa boss kwa hiyo twende tena sehemu fulani sipajui jina kwa sababu ya ugeni wangu maeneo hayo ndo huyo mke wa boss anapatikana kwa hiyo yule jamaa ambaye ni fundi pikipiki aliyetupokea pale sinza kijiweni pindi tunakuja akatushauri kuwa mmoja wetu kati yangu mimi na dereva anaweza tangulia na huyo mdogo wake na boss ili twende kwa mke wa boss akatupatie ela tuliokubaliana na ndipo tukashauriana na dereva wangu kuwa twende wote pamoja na ndipo safari ikaanza lakini mdogo wake na boss alitaka kuendesha pikipiki ili aiangalie (test) na yeye kama ipo salama so hatukuwa na njia yoyote ya kumkataza kwa sababu tulipanda wote kwenye hiyo pikipiki mimi na dereve wangu lakini dereva akiwa ni mdogo wake na bosi na safari ilipoanza tukaenda mpaka sehemu flani tena hapo sinza kwa ndanindani uswahilini tulipofika tukakutana na kidaraja flani hivi cha mwinuko ambapo ili ukipande ukiwa na pikipiki inatakiwa uwe peke yako ndipo mchezo wote dereva wangu akausoma akanambia mimi nibakie nimepanda pikipiki afu yeye atangulie juu ya hicho kidaraja tukakubaliana safari ikaanza ya kupanda hicho kidaraja tulipokimaliza afu tukapanda wote kama awali hapohapo si mbali sana na hicho kidaraja huyo mdogo wake na boss akasema ngoja nimpigie boss kuwa tumefika mahali aliposema yeye na alipompigia boss kuwa tumefika hiyo sehemu boss kasema kuwa ile ela ambayo alikuwa ameipangia kununulia hiyo pikipiki eti mke wake kaitumia kuongezea kwa ada ya shule ya watoto wake na akanipigia na mimi simu akiniomba msamaha kwa hayo yote yaliotokea basi nikachukua pikipiki yangu mi na dereva wangu tukarudi nyumbani,,,,,
Ndipo mi na dereva wangu tukajua kabisa ule ulikuwa ni mchezo wa sisi kuibiwa pikipiki na kwa kufanikiwa kuvuka kile kidaraja chenye mwinuko nikiwa nimeipanda ile pikipiki na dereva wangu akiwa ametangulia mbele yake akihakikisha usalama wa ile pikipiki ndipo mchezo wote tukaumalizia pale na ndipo silaha yote ya kuibiwa pikipiki ikakomea pale nawahakikishia wadau tusingekuwa wawili ile pikipiki hakika ingeibiwa hapohapo kwenye hicho kidaraja cha mwinuko kwa maana angefanikiwa kupanda akiwa peke yake angetokomea nayo kwa hiyo namshukuru sana mungu kwa kutuepusha na hilo janga na namshukuru sana dereva wangu aliyekuwa anajitambua kwa haya masuala ya wizi hakika nimejifumbua macho mpaka saivi na nawashauri kuweni makini sana kwa hawa matapeli wa mjini,,,
ASANTENI NA MUNGU AWABARIKI..