Wizi huu wa nmb mobile umezidi jamani...

Wizi huu wa nmb mobile umezidi jamani...

bysange

JF-Expert Member
Joined
Jan 11, 2011
Posts
4,456
Reaction score
1,565
Napenda kwanza kuwasalimu ndg zangu wa jf kila mmoja kwa imani yake.
Hawa nmb wanahuduma kadhaa wa kadhaa kwa ajili ya wateja wao ila leo naomba nizungumzie hii huduma ya nmb mobile.Wizi walioweka ni wa kificho mno na uko hivi;
Mara tu unapopiga ile namba ya ya huduma(*150*66#)wanakata hela tsh 36.2 kama huduma haipatikani na hapo ni kwa sekunde 30.kama utajaribu tena maana yake utatumia dakika moja na kukatwa tsh 72.4 bila huduma.hivyo kwa siku ukijaribu kutumia huduma hii bila mafanikio kwa uchache wa mara 5 maana yake utakatwa 72.4*5=tsh362 mara siku tatu nilizojaribu bila mafanikio nimepoteza tsh 362*3=tsh 1086.
Je kama huduma hii itatumiwa na watu elfu kumi itakuwa ni 1086*10,000=tsh 10,860,000 kwa siku hizo tatu.
Kwanini wawe na makato kabla ya MUAMALA(TRANSACTION)?
Kwanini wasiweke mfumo kama wa mpesa,tigo na airtel money,kuliko huu wizi wanaotufanyia?
Ndg zangu na huduma za mabenki mengine ni kama hivi au ni usanii tu wa hawa nmb?
Chanzo mimi mwenyewe kama muathirika wa huduma hii,naomba kuwasilisha
 
Da hawa nouoma kweli kanetwork kanapotezwa kinamna ee da washawahi kunilamba hao jamaa da
 
Hata TPB ni hivyo hivyo acha watuibie si tumekosa mtetezi.
 
Tanzania ya leo kila sekta ni wizi mtupu; hizi huduma zinazoanzishwa kila kukicha kwa minajiri ya kumnufaisha mteja, hakuna ukweli wowote, na ndio maana tunasema mwenye nacho atazidi kuongezewa na mlala hoi, hii ndiyo Tanzania ya leo!
 
Hata TPB ni hivyo hivyo acha watuibie si tumekosa mtetezi.

Mtanzania ni mtu mjinga kuliko wote duniani. Unaweka makalio kwenye jamvi kutwa kucha ukisubiri mtetezi? Haki haiji kwenye sinia kama pilau ya msiba!
 
Mbona mim natumia line ya tigo kwenye nmb mobile hakuna kitu kama hicho
 
Napenda kwanza kuwasalimu ndg zangu wa jf kila mmoja kwa imani yake.
Hawa nmb wanahuduma kadhaa wa kadhaa kwa ajili ya wateja wao ila leo naomba nizungumzie hii huduma ya nmb mobile.Wizi walioweka ni wa kificho mno na uko hivi;
Mara tu unapopiga ile namba ya ya huduma(*150*66#)wanakata hela tsh 36.2 kama huduma haipatikani na hapo ni kwa sekunde 30.kama utajaribu tena maana yake utatumia dakika moja na kukatwa tsh 72.4 bila huduma.hivyo kwa siku ukijaribu kutumia huduma hii bila mafanikio kwa uchache wa mara 5 maana yake utakatwa 72.4*5=tsh362 mara siku tatu nilizojaribu bila mafanikio nimepoteza tsh 362*3=tsh 1086.
Je kama huduma hii itatumiwa na watu elfu kumi itakuwa ni 1086*10,000=tsh 10,860,000 kwa siku hizo tatu.
Kwanini wawe na makato kabla ya MUAMALA(TRANSACTION)?
Kwanini wasiweke mfumo kama wa mpesa,tigo na airtel money,kuliko huu wizi wanaotufanyia?
Ndg zangu na huduma za mabenki mengine ni kama hivi au ni usanii tu wa hawa nmb?
Chanzo mimi mwenyewe kama muathirika wa huduma hii,naomba kuwasilisha

najua fika utakuwa unatumia mtandao wa vodacom, kama hutaki makato hayo hamishia huduma hiyo ya mobile kwenye tigo au airtel huwa hawakati .
 
Mi mwenyewe juzi nilikumbana na paranja la nmb mobile hakuna huduma salio limekatwa?? Natamani hata kujitoa
 
Back
Top Bottom