Allen Kilewella
Rejea bandiko la
Troll JF lenye orodha ya mambo ya Muungano. Soma #9 inayosema '' utumishi katika serikali ya Jamhuri ya Muungano'' haikusema mambo yanayohusu Muungano!
Pili, Wizara zote zina nembo ya '' Jamhuri ya Muungano wa Tanzania'' hakuna nembo ya mambo yasiyo ya Muungano.
Tatu, kwavile zinatumia nembo ya Jamhuri ya Muungano , Wizara zote ni za Muungano.
Ndio maana kazi ya kwanza ya Mchengerwa baada ya SSH kuingia ilikuwa kuidhinisha 21% ya ajira ni za Zanzibar
21% haikusema ajira za mambo yasiyo ya Muungano, zinasema ajira za Muungano kwa maana popote nembo ya Jamhuri ya Muungano inapotumika.
Nne, na kwavile nembo za Wizara na Taasisi ni '' Jamhuri ya Muungano'', na Mzanzibar ana Passport ya Jamhuri ya Muungano, kumkatalia ajira katika jambo lenye nembo ya Muungano ni kumnyima haki kikatiba.
Vitambulisho vya (NIDA) Wazanzibar walivichangamkia kuliko Watanganyika, na wakwanza alikuwa Marehemu Maalim Seif. Wote akina Jusa, OMO, Mansour , Duni wana NIDA, majukwaani hawataki muungano.
Vitambulisho vya NIDA ni kulinda masilahi yao kama umiliki wa ardhi, ajira za watoto wao , access ya soko la watu milioni 60m masomo kwa watoto wao(HESLB) n.k. huku Tanganyika, si mapenzi ya Tanzania.
Hivi unadhani kwanini Wazanzibar walikataa Serikali 3 Bunge la Katiba ! wakamtisha JK ndani ya NEC
Hayo mambo ya Muungano ! 90% si ya Muungano!Katika mambo ya Muungano kila jambo lina mbadala Zanzibar! sasa hivi Wana jeshi lao linatoa mafunzo kama Monduli halifunzi Mtanganyika , ingia youtube
Bila Tanganyika mada hizi zitajirudia kila siku!
Pascal Mayalla JokaKuu