Wito Kwa Wanataaluma Kuunganisha Nguvu Ili Kuleta Mabadiliko Ya Kweli Na Maendeleo

Jul 14, 2008
1,820
1,031
Kabla hujaanza kusoma tembelea hapa:

https://www.jamiiforums.com/habari-na-hoja-mchanganyiko/48898-kongamano-la-wanataaluma-katika-baadhi-ya-picha.html

--------------------------------------------------------
Wazalendo Wenzangu;

Wazalendo na Wanataaluma Wenzangu;

Tunalo deni katika Nchi yetu la kutambua kuwa sisi kama Wasomi na Wanataaluma tunayo sehemu kubwa sana katika kuleta maendeleo na mabadiliko ya kweli katika nchi yetu.

Ni kweli kuwa Serikali na Viongozi wanayo sehemu yao ya kufanya katika kubuni mikakati na sera za kuleta maendeleo ikiwa ni pamoja na kuleta maendeleo ya ujumla. Ingawa pia katika katiba raia anayo haki ya kuwajibisha watendaji hasa wa serikali. Ni sisi tu kuchukua hatua za kisheria kufuatana na taratibu zilizopo.

Lakini ikumbukwe pia kwamba, kila mtu binafsi anayo nafasi yake ya kuleta maendeleo ya nchi kwa kuanzia yeye binafsi, familia, jamii nk. Haitoshi kwetu sisi kuridhika kuwa kwa kuwa tunazo kazi nzuri na bora, na kwa kuwa tuna viapato vya kuridhisha na nyumba za kuishi na usafiri na kusomesha watoto katika shule tunazopenda, basi suala la maendeleo zaidi halituhusu sana japokuwa tunao uwezo mkubwa sana wa kuleta mabadiliko .

Umefika wakati sasa lazima tukubali kuwa Wanataaluma na wasomi sasa tunayo nafasi kubwa sana ya kufanya kuliko wakati mwingine wowote. Kila mtu anayo sehemu yake na tunatoa wito kuwa wakati sasa umefika.

Tafakari sana na amua sasa kuunganisha nguvu zetu za kiakili, kitaaluma na kisomi kuleta mabadiliko ya kweli.

Fanya kila uwezalo kuhudhuria kuwa sehemu ya mabadiliko ya vitendo na wala si maneno ambayo hazijatufikisha kunakostahili.

Tunatoa mwito sasa ni vema kila mtu anyevutiwa akajisajili kuwa mwanachama wa Mtandao wa Wanataaluma. Registration ni TZS 50,000/=. No Monthly fees ni TZS 10,000. Unaweza kulipa kwa njia yoyote rahisi hata kwa kukatwa airtime kidogo kidogo tu.

Pia tunapenda kutoa mwito kuwa sasa Wanataaluma wanachukua nafasi yao ya kuleta maendeleo na mabadiliko katika nchi. Tunahitaji rasilimali zote hasa Utaalamu na Pesa.

Kama uko tayari kujitolea katika lolote tafadhali tueleze na tuwasiliane.

Pia kama uko tayari kuchangia kila siku kupitia kukatwa automatically Air-Time kila siku kati ya TZS 150 hadi TZS 1200 kwa siku, tafadhali tujulishe. Kuna utaratibu tunaandaa lakini tunahitaji sana support yenu.

Kwa walioko nje ya nchi na Mikoani; tunahitaji kufungua matawi au Chapters kila mahali. Kama una uzalendo na nia ya kweli ya kusaidia maendeleo ya nchi kwa kuweka maslahi ya taifa mbele, tafadhali tuwasiliane. Tuunganishe nguvu na akili zetu.

Fanya sehemu yako.

Kwa walio tayari wawasiliane moja kwa moja na mimi au:
Mr. Emmanuel Mmari
TPN Finance and Administrative Manager
Email: emmammari@yahoo.com
Mobile: 0715 740 047

Wasalaam


Sanctus Mtsimbe
President - TPN
---------------------------------------
Tanzania Professionals Network
TOHS Building - Dar Group
Nyerere/Mandela Road
P.O. Box 21605
Dar Es Salaam, Tanzania
---------------------------------------
Dir. Tel: + 255 - 22 - 216 3805
Fax Line: + 255 - 22 - 2115 571
Mob. Tel: + 255-754 833 985
---------------------------------------
E-Mail: president@tpn.co.tz
Web: www.tpntz.org

 
Back
Top Bottom