Maudhui ya wimbo uitwao Chezea
Pengine yanayokosoa
viongozi wasiojali wananchi
yaliamsha shangwe kutoka
kwa wananchi waliohudhuria
sherehe za miaka 53 ya Uhuru wa Tanganyika katika Uwanja
wa Uhuru, Dar es Salaam jana. Wimbo huo wa Kwaya ya AICT
Makongoro kutoka Mwanza
ulionekana kuwaingia wengi
ambao walitingisha vichwa
vyao na wengine kupiga
makofi kuashiria kukubaliana na maudhui yake. Cheo ni dhamana, hakuna
aliyezaliwa nacho uliye
madarakani yapasa kusimama
kwenye haki wala
usijidanganye walio chini
hawajui kitu, haki ya mnyonge haipotei, bali
inacheleweshwa. Keki inapokatwa kila mtu
aipate, hivyo inapogawiwa ni
vyema kila mtu aipate lakini
ikiishia juujuu elewa kwamba
chini manunguniko yataanza,
mwisho wake ni vurugu, chezea pengine usichezee
amani, ni miongoni mwa
maneno yaliyopo kwenye
wimbo huo. Waimbaji hao waliwataka
wanasiasa na waandishi wa
habari kutokubali kununuliwa
na kuwa chanzo cha kupotea
amani.
"Chanzo gazeti la mwananchi"