Onana ni mchezaji mzuri lakini ana utoto mwingi sana na anapenda sifa. Baada ya kufunga tu goli moja basi akanza upuuzi wake wa kutembea na mpira wakati wenzake wanasubiri mpira mbele.
Na benchi la ufundi la Simba likumbushwe ili liwe linakemea wachezaji wake maana Simba wakiwa mbele kwa tofauti ya goli moja tu basi wachezaji wote wanaanza upuuzi wa pasi fupi fupi mara visigino badala ya kutafuta tofauti ya magoli mawili na kuendelea. Goli moja halina "cover" maana yake hata sekunde moja ikibaki linaweza kurudi. Na juzi kama Ajibu angetulia wakati ameshamchungulia Ayoub yupo mbele kidogo ya mstari wa goli nafikiri "week end" ingekuwa mbaya sana kuanzia kwa wachezaji, benchi la ufundi, viongozi, wanachama na mashabiki wa Simba. Wakiendelea na huo upuuzi ipo siku hawataamini kitakachotokea.