mtu kitu
JF-Expert Member
- Apr 23, 2011
- 702
- 508
Zanzíbar mjini, Nungwi na Pemba yote hakuko shwari,Mimi mkazi wa Dar es salaam nimekuja Liwale (nyumbani) kuwacheki wazazi . Nilichokikuta huku ni hatari. Kuna kata hapa mjini inaitwa Likongowele hali si shwari, mawakala wamepigwa na umma, nyumba ya diwani mteule Mussa Mkoyage imechomwa moto.
Kuna kata ya Lilombe huko wananchi mpaka wanafikia hatua ya kukatana viungo muhimu kama miguu na masikio. Kwa ufupi kata nyingi zimegubikwa na vurugu. Mkihitaji picha na video nitaweka kama patakuwa na ulazima.
Cha ajabu sioni media yoyote ikitipoti hizi vurugu. Je, mtandao kuzimwa ndio sababu?
Je, kuna wilaya au jimbo lingine Tanzania vurugu zingali zipo mpaka sasa?