Why UKAWA will loose the 2015 Election


Kutokana na maelezo yako nimeshapata jibu wewe ni Pro-Chadema,kwani ni kawaida yenu kukimbilia udini,ukabila etc No wonder ndio mana watu wanahusisha Chadema na ukristo kwa sababu ya watu kama nyinyi.Zitto na kura za waislam?? kweli?? is this the best you can come up with??
 
basi hukutakiwa kusema ndugu zangu chadema mtu usio na chama, the problem unatoka unaingia

watanzania wote ni ndugu zangu, siangalii itakadi wewe kuwa ndugu yangu. Kama ni mtanzania inatosha kuwa ndugu yangu
 
Unachosha sana watu, wewe ni mbishi asiyetaka kujifunza bali unataka watu wakubali yako tu.
 

2010,kura za Slaa hazikutokana na Zitto kuwepo Kigoma au umaarufu wake. Dr Slaa alikuwa na umaarufu kuliko Zitto,na kura za Kigoma hazikutoka jimbo la Zitto pekee ila hata majimbo mengine. Dr Slaa alikuwa maarufu kuliko Zitto na ndiyo maana watu walipata hamasa kuongeza wabunge ni kwasababu ya Slaa. Ni mwaka ambao jeshi kwa mara ya kwanza lilitoa tamko kuhusu uchaguzi Mnadhimu akiwa Lt Jenerali Shimbo. Hii yote ni kwa ajili ya Slaa. Watu wa Kigoma walimpa Slaa kura kwa mapenzi yao kwa Slaa na Zitto. Huyo Zitto mwenyewe kama ccm wangempigia mgombea wao kampeni asingepita kwani ukiangalia kura zake hakushinda kwa kishindo ingawa ccm walimwachia. Ndiyo baada ya matokeo alikiri kuwa udini ulipunguza kura zake na ndiyo maana anakimbia jimbo mapema aende mjini kwenye waislamu wengi. Kama ni maarufu mshauri agombee tena Kigoma kaskazini uonr atakachoambulia.
 

Ndugu,

Mifanano ipo, na inaweza kuwepo, sisi pia tunatafuta katiba mpya kama wenzetu walivyofanya. Utafutaji huo huweza kubadilisha mifumo ya kisiasa, ilitokea Kenya na Ruto alikuwa muhimu kwenye kumchagua raisi, nilichojaribu kusema ni kwamba ndugu Zitto atapiga uRuto kwenye chaguzi zijazo.
UKAWA haikowepo kabla ya bunge la katiba; Miuongano na mifumo mipya hainishangazii hata kidogo kwenye uandishi wa katiba mpya.
Hoja ya udini kwa kweli sijachunguza vya kutosha kuweza kuchambua itakavyoyumbisha chaguzi zijazo.
Jaribu kujadili kwa hoja na mifano ili tuelewe sote, jazba haisaidii mkuu
 
Simple furaha ya MaCCM ni UKAWA KUSHINDWA!!
Kumbuka ZZK hana wala hakuwa na msaada wowote Kwa ushindi wa UKAWA!!
Mfadhiri wa ACT ni TISS ili kuibomoa CDM,
Tumeona Uchaguzi wa Serikali za mitaa, hao ni MaCCM B!!
 
Last edited by a moderator:
watanzania wote ni ndugu zangu, siangalii itakadi wewe kuwa ndugu yangu. Kama ni mtanzania inatosha kuwa ndugu yangu

acha kupotosha kwa context unayoongea huwezi sema ndugu hata kama wote ni watanzania
 

You go ahead and support that politically mutant being. But with me I might only support another Zitto not the disturbed Zitto Zuber Kabwe that I now know better!!
 
unachosha sana watu, wewe ni mbishi asiyetaka kujifunza bali unataka watu wakubali yako tu.

pumzika kidogo halafu rudi jf upate raha duniani
 

tatizo mshikaji Simple hajibu hoja kama hizi, kuna mtu kumuuliza humu anafahamu historia ya ODM hadi akaibeza UKAWA eti lengo lake lilikuwa katiba tu na sio uchaguzi, namaliza post zote sijaona jibu
 
Last edited by a moderator:
Kawe,Ubungo,Iringa mjini,Rukwa na mengineyo

Umeshiba propaganda mfu, yeye ana faida gani kwao, maana kwao hajapata uungwaji mkono kwanini mshibe imani ya kwamba ndio alisaidia majimbo ya wenzake? Nyinyi kwa kiwango kikubwa hii michango yenu ndio ilimfanya Zitto ahakikishe anaivuruga cdm bila kujali ili mradi apate madaraka ya juu. Hilo limekuwa wazi kwa chama.chake kipya. Sina tatizo na Zitto kuhamia chama.kingine kwani ni haki yake na ni ukweli usiopingika ana uwezo mzuri kiuchumi, lakini nilochogundua ana udhaifu wa kuzira kutoa ushirikiano iwapo anakosa madaraka ya juu. Udhaifu wa aina hii pia ninauona kwa wabunge wengi waliokuwa,mawaziri, pindi walivuliwa uwaziri wao hata utendaji wao na uwakilishi wao wa kibunge ulishuka. Sasa mtu kama huyo unategemea angekuwa na matokeo mazuri uchaguzi huu kama tayari moral ya ushindi imeshuka.

Kwa hali ilivyo nguvu waliyonayo cdm imekuwa kubwa kutokana na wao kuzunguka.nchi nzima kufanya kazi ya kueneza chama toka 2010. Hebu nitajie toka mwaka 2010 Zitto amekwenda mara ngapi kwenye mikutano ya kujenga chama.yenye tija zaidi ya ugomvi kuwa ndio sifa yake kubwa kwa miaka hii 5? Usilazamishe kukubalika kwa Zitto kwa hisia za kiccm na kipropaganda wakati in real sense sio sehemu ya nguvu ya chama iliyopatikana miaka hii 5 iliyopita baada ya uchaguzi. Ila kama yeye Zitto ataendesha siasa za majitaka atafanikiwa kupunguza kura za ukawa kwenye uchaguzi mkuu kwani mafisadi wataendesha siasa chafu kupitia media, ukichanganya na tume kutokuwa huru, jeshi la polisi linalofanya kazi kwa mazoea kwamba lazima ccm ishinde kwani wote wanalindana kwenye wizi ndio litakalofanya ccm ishinde tena kwa tabu na sio hilo la Zitto kuondoka kama mnavyolazimisha hapa.
 

Zitto kawaambia wabunge 10 toka chadema wataenda ACT we noma sana mkuu
 
Simple furaha ya MaCCM ni UKAWA KUSHINDWA!!
Kumbuka ZZK hana wala hakuwa na msaada wowote Kwa ushindi wa UKAWA!!
Mfadhiri wa ACT ni TISS ili kuibomoa CDM,
Tumeona Uchaguzi wa Serikali za mitaa, hao ni MaCCM B!!

Ningependa kuiona Tanzania inayoongozwa na watu wengine, sio viongozi wa sasa. UKAWA haikuundwa kwa ajili ya kuiondoa CCM madarakani, iliundwa ili kupingwa katiba inayopendekezwa: Sasa ni wakati mzuri kwa wao kubadili mbinu na miongozo ya umoja wao ili kuchukua uongozi wa nchi. Nionavyo mimi, mpaka sasa hawajajipanga vya kutosha, kuviongoza hivi vichwa( Mbowe, Mbatia,Lipumba,Slaa) kupata kuafikiana KIUCHAGUZI si lelema, INAWEZEKANA iwapo;
- Viongozi hao niliowataja wataacha TAMAA za madaraka na rasilimali.( Kusimamisha mgombea uraisi uleta ruzuku kubwa)
-Watanitajifunza kutoka miungano yao iliyopita na mingine ya nchi za jirani
-watatengeneza mkakati madhubuti wa kuchukua dola
-wajivue dhambi ya kumyanyapaa ndugu Zitto
 
 
mtoa mada kwanza kabisa hujiamini na hiyo ni factor mojawapo ya kushindwa kwako. poor analysis
 
Haya bwana kwahiyo hao wengine wa chadema ikiwemo Slaa mwenyewe hakufanya campaign huko? Halafu bado haujajibu swali langu kwanini kwenye jimbo lake la zamani (Kigoma Kaskazini) Chadema walishindwa uraisi ? au ndio hakufanya campaign huko

Kabla ya uchaguzi ule Zitto alikuwa amedeclare kuwa tangu nchi kupata uhuru serikali haikuwahi kuisaidia kigoma kaskazini na kihoma yote kwa ujumla kama serikali ya kikwete. Ilikuwa either awe mkweli au afanye unafiki wa kisiasa, ile kuponda tu hadi kieleweke.
 

Hii mada imekuwa kama umetaka kumjenga Zitto ila ni kama umesababisha watu waanike udhaifu wake na kwenda mbele zaidi kwa kumdhihaki. Unawataja viongozi wa ukawa kwamba hawawezi kuelewana kwani wanapenda sana madaraka tena cdm wamemuonea sana Zitto!! Hivi uko serious,? Unawaona hawa wengine wanapenda sana.madaraka, umesahau kilichomfikisha hapo Zitto alipo keo ni ugomvi wa kupenda sana madaraka? Kama sio na yeye kupenda madaraka imekuwaje ajiunge na kipya tena.chinj ya siku 7 yeye ndio mkuu wa chama tena kwa cheo ambacho sio cha utaritibu uliozoeleka. Sina tatizo na hicho cheo kwani ndio ubunifu wenyewe lakink kweli mwanachama wa wiki moja kweli? Hivi hicho chama muda wote kilikuwa kinaongozwa na vibuyu ama? Hivi kuna uwezekano wa mtu kwenda ccm/cuf/nccr au hata chausta na wiki hiyohiyo kuwa mkuu wa chama.

Nakushauri kama umeamua kujitoa ufahamu na kuamua kumtetea Zitto kwa aina hii naona kama unamuanika tu hapa. Achana na hizo post zinazokudhalilisha na kumdhalilisha tu Zitto.
 


Mkuu tunaweza kuanza kwanza na Kura alizopata yeye Jimboni kwake?
vipi walizopata CHADEMA jimboni kwake unakumbuka ni ngapi?
 
Mkuu tunaweza kuanza kwanza na Kura alizopata yeye Jimboni kwake?
vipi walizopata CHADEMA jimboni kwake unakumbuka ni ngapi?

Nakwambia jamaa ameamua kuchosha tu watu, hana data wala nini ni mahaba niue kwa Zitto wa Kabwe tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…