Who is in control? Nani hasa anatawala nchi yetu?

salisalum

JF-Expert Member
Joined
Oct 27, 2010
Posts
434
Reaction score
159
Ndugu Watanzania naomba tutafakari hii hoja iliyoko kwenye swali, nani hasa kwa sasa anaongoza nchi yetu?

Kwa nini nimeleta hii hoja? Nina sababu kadhaa ambazo nitazitanabaisha hapa chini:
1. Ndugu Samia Suluhu Hassan akiwa bungeni mara baada ya kujitangaza mshindi katika uchaguzi ambao kiukweli haukufanyika, aliwaomba wajumbe kwenye ukumbi wa bunge wasimame na kukaa kimya kwa muda kuwatambua na kuwakumbuka watu wote waliouawa kuanzia tarehe 29/11/2025. Samia huyu huyu akiwahutubia watu wanaodhaniwa kuwa wazee wa Dar es salaam hakuwataka hao wazee kusimama na kuwakumbuka hawa marehemu. Katika hotuba yake alionyesha kuchukizwa sana na victims hawa huku akiwatuhumu kutaka kuiangusha serikali. Alisema pia nguvu iliyotumika (kuua) ilikuwa sawa. Haiwezekani kiongozi akawa na hizi extremes mbili kwa wakati mmoja. Haiwezekani kuwa na kiongozi anayetaka kuwangoza watu kuvuka dhahama na sintofahamu iliyotokea lakini wakati huo akiwa kachomoa upanga.

2. Waziri wa mambo ya ndani amesikika hivi karibuni akiwaagiza polisi waache kukamata watu bila kufuata sheria. Waache kukamata watu wakiwa bila sare zao rasmi, waache kukamata watu wanaotuhumiwa kwa makosa madogo kama makosa ya mitandaoni usiku wa manane huku wakiwa na silaha nzito, na mengine mengi. Hata hivyo ukamataji usiozingatia sheria bado unaendelea kama ilivyokuwa na ukamataji kwa namna ya utekaji unaendelea. Haiwezekani kama nchi ina uongozi ukafanyika upuuzi wa namna hii.

Kama polisi hawamsikilizi waziri wa sekta yao wanamsikikiza nani?

Who is really in control?
 
Something that is clear Samia lost control
 
Who are You ??? Alieagiza shoot to kill .......leo kawageuka anasema IGP alichelewa take action .....ile saa 4 walipoanza fujk ubungo na mabibo......kafara tu mbatoana sasa utapata wapi wengine ? Kutoka mbinguni au humo humo ? Unafiki tuuuuu.....hakuna wekedi wala nini kula kwa zamu kutumika kama condom.....period
 
Pilisi ndio wanatawala nchi kwa sasa.
1. Wao ndio hutoa taarifa kwa umma za seeikali kila siku.
2. Simbachewene aliwaambia wasiteke au kukamata watu usiku, tarehe 28 walimteka yule diaspora kule Moshi na kutoa tamko baadaye sana.
3. Polisi ndio kila kitu kwa sasa JW wakasome.
4. Ukitoa ushahidi kwa yaliyotokea oktoba 29, Yule polisi kwenye tume anawapa polisi taarifa na kesho utakua Ruvu kwenye sandarusi.
 
Mkuu 'Slisalum', ni swali zuri ulilouliza, na mada iliyofuatia imefafanua vizuri mawazo yako, ambayo umeyawasilisha vizuri kabisa..

Nchi yetu sasa hivi inaendeshwa na watu ambao hawakupata ridhaa ya waTanzania kuwaongoza. Wapo madarakani kwa kutumia mabavu

Hili janga la mauaji halikutokea kwa bahati mbaya, ni janga ambalo lilikuwa linajitengeneza tokea huko mwanzo katika harakati za kushika mamlaka kwa nguvu.

Anzia kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa. juhudi zote zilifanyika kuhakikisha uchaguzi huo ulikuwa ni maandalizi ya unyakuaji wa madaraka kwa nguvu.
Vyama vya upinzani, na viongozi wao; hususani CHADEMA, mbinu ziliandaliwa mapema kuwadhibiti wasiingilie mipango ya watawala kubaki madarakani kwa nguvu.
hata pale walipolegeza masharti ya kuwepo na Katiba Mpya kabla ya uchaguzi; na badala yake pawepo na marekebisho kidogo ya sheria za uchaguzi ili pawepo na uchaguzi huru na HAKI, hili pia likaonekana ni hatua ya kuingilia mipango ya watawala kubaki madarakani kwa lazima.
Huko ndani ya chama CCM kwenyewe; watawala ambao ndio viongozi wa chama hicho wakaona wafanye mbinu za kubadili taratibu, hata za kumpata tu mgombea wa urais

Unaposoma na kutafakari mtiririko wa haya yote, na mengi mengine kama hayo, inawezekana vipi usijue ni nani anayetawala taifa hili?

Ni nani aliyepanga na kuwezesha mipango yote hii kama siyo hao hao waliopo kwenye madaraka kinyume na matakwa ya wananchi?

kiuwezo kifikra, Samia Suluhu Hassan siyo mtu mwenye uwezo mkubwa alichojaliwa sana ni kuwa mtu laghai na mwongo sana, na anapofanya hivyo hana hata chembe ndogo ya aibu.
Kwa hiyo, unapoona akidai kwanza kwamba waandamanaji walivuka mpaka toka nchi za nje kuja kufanya maandsamano hapa; na hapo hapo anadai vijana wetu wenyewe wamerubuniwa kwa kupewa pesa wakaandamane; wakati huo huo akiwalaumu wazazi kwa kutowazuia watoto wao wasiende kuandamana na walipouliwa wenye makosa wakawa ni wazazi
Yoote haya huwezi kuona huyu ni mtu wa namna gani huyu; kiasi kwamba uwe na mashaka naye juu ya kutumiwa tu na watu wengine ambao pengine ndio wanaoongoza nchi hii?

Lakini nikirudi nyuma na kuungana nawe kwenye swali lako; nami labda naweza kusema/kuuliza, ni nani anayemuwezesha huyu mwanamke?

Kuna pesa nyingi sana imetumika kuwanunua wakuu woote wa vitengo muhimu aliowapanga yeye mwenyewe kwa kuwateua katika nafasi hizo, akiwa tayari na picha ya kumwezesha kubaki madarakani.

Hawa sasa, wanaomwezesha kwa pesa nyingi; hata katika kampeni za kuwasomba watu. mabango na takataka nyingi nyingine. Hawa labda ndio tunaweza kuwatazama kama sehemu ya kutawala nchi, akina Roastam azzizi na hata wafadhili wengine toika nchi za nje

Lakini kiujumla, mhusika mwenyewe toka mwanzo ni Samia Suluhu Hassan, kwa msaada wa Genge lake la akina Kikwete; na mbaya zaidi BAKWATA na wao wakawa ni sehemu ya tatizo hili.

tusitafute saana mhusika mwingine wakati mhusika mkuu anajulikana.
 
Umeuliza swali zuri sana na lenye kuhitaji tafakuri ya kina Sasa subiri uone majibu kutoka Kwa machawa....
 
Hamna kazi za kufanya ndo maana kutwa mnakesha humu. Nchi inaenda na ilani ya CCM inatekelezwa by 2030 unakuja ushindi wa kishindo
 
Msanii mkongwe na maarufu kabisa Jay 2 the Kay, ndiye cotroller mkuu wa nchi since then.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…