What is time?

Tazama uzi -- tundiko hili.

Pia uzi huu.

Kusafari kiwakati ni jambo linalowezekana.

Unachofikiri kuhusu 'maada', 'unafasishi', 'wakati' na 'nishati' huenda ni 'ndicho sicho'.

Ulimwengu hauna 'wakati' mmoja--na nyakati zote si nyakati hasa ila 'SASA'.

Fikiri kana hivi kila nukta ifanyayo 'tukio' ni kama wakati mmoja, kana mkondo, watoka mbele kurudi nyuma vivyo hivyo mwingine kutoka nyuma kwenda mbele.

Mifanyiko yote ni mchanganyiko wa 'kweli' na 'si kweli'--ulimwengu wote ni mchanganyiko wa 'habari' na 'kionekacho kana kitu ama dutu'; japo ni si kitu kwa hali nyingine.

Unaweza kuona basi, kilicho hapa, kilicho hapa lakini kisicho hapa hasa, vile vile kilicho kule mbele ya wakati kadri vile kilicho unakoweza kudai ni nyuma ya wakati.

Vitu vipo katika namna ya 'ulimwengu mmoja' na hali hapo hapo ni 'alimwengu sambasamba nyingi' isivyo idadi. Wewew kama kitu hai, upo katika ulimwengu huu kwa wakati huu, lakini wewe pia upo katika alimwengu nyingi sambamba ambamo wewe waweza kuwa hivi ama vile isiwe sawa sawa na hapa ulipo sasa. Je. ni wapi wewe wawa ni 'Moja'?

Vitu vyote vilivyohai na visivyo hai -- kadri ya vina vya tafsiri vyetu, vyatungika kwa namna ya mtungiko wa habari... Ukitambua siri na fumbo za habari, basi wewe waweza kutenda ama kufanya hata yale ambayo katika hali ya kawaida vina vya upeo, maarifa na tafsiri ya mtu vingalikusema ni 'miujiza' ama 'kisichowezekana'.

Kwanza nikupe ufafanuzi wa nishati kwa namna inayoweza kubeba haya yote,

"Nishati ni uweza na uhali kuweza kupangilia msimamo kutokea mvurugiko kipunde"...

Kwa kusema hivyo, ina maana tunachokijua leo na kukitaja kama 'kazi' kinaweza kutendeka bila 'nguvu'... Yaani kama 'kazi' ni zao la 'kani' na umbali; pia kazi inaweza kufanyika pasipo 'kani' lakini kudhahirika kupitia 'uhali'. Kadiri hii ni uweza ulio katika 'habari'...

Nitakupa picha ya zoezi la kutanua uwezo wa kumaizi hili... Fikiria kana tunaishi katika ulimwengu 'unaowaka' na 'kuzima' kwa kasi ya ajabu mno kuweza kukadirika... Kila unapowaka ni kadri ya mpangilio--unapozima ni kadiri ya mvurugiko; kichosaidia vitu kufutika na kutukia vile vile kutokea kadri ya tukio la kadiri moja hadi ingine ni 'habari' ama 'neno'... Basi jaribu dhanio kama unaweza kuiandika habari kuwa tofauti basi unaweza kuathiri uthibitiko wa uendelevu wa dhahiri kuto hata landana na 'unafasishi'...

Hili lina kuletea picha ipi? Katika Jaribio la kudhanika Uadilifu; Ukiwa na meza yenye pembe nne, tuziite pembe A, B, C na D; halafu kwenye pembe moja ukaweka kapira 'O' kadogo--kenye uso mwororo sana--juu ya uso mwororo sana wa meza; basi kama meza hiyo tena yenye uso bapa sana ikiwa na kipira kwenye tuseme ncha A halafu tukawa na namna ya kifaa chenye kuweza kusoma na kuhifadhi habari za mitetemo ya hali ya juu sana kukadirisha 'kipira O' katika ncha A basi ikiwa tutasogeza kipira O kiende kukaa katika ncha C, pembe mtazamano na A -- na huko nako kifaa hicho hicho kikasoma na kuhifadhi mitetemo ya hali ya juu ya hicho katika nafasi husika -- basi hili linawezekana; kama chombo hicho hicho kwa kadri ya kuweza kusoma lakini pia kinaweza 'kutekenya', kwa namna ya utetemeazi, kikitetemeazisha kipira O kilichopo katika ncha C kwa kadri ya mitetemo ya hicho kilipokuwa ncha A--nini kitatokea? Ikiwa chombo hicho kina ubora na ufanisi wa hali ya juu ya kusoma na kutetemeazisha basi kipira O kitaitika kwa jambo ambalo katika upeo na uzoefu wetu wa kawaida hatujawahi kudhani inawezekana--kipira O kitapotea ncha C na kutokea ncha A... Ina maana hakitasafiri toka ncha C kwenda A kwa tunavyoweza kudhania, kukatikizia katika unafasishi wa dhahiri juu ya meza...

Unaweza kusafiri kutoka nukta A kwenda B bila 'kusafiri'... Tuite 'telepotia'. Je, 'wakati' umwekwenda wapi katika hili?

Hili ni moja, kati ya mengine mengi yanayoweza kutaka usahau unachofikrir unajua kuhusu maada, unafasishi, wakati na nishati.

Rejea

A. R Bordon, D.H Hasler, J. A. Sanchez, F. M Maye, R. B. Soligen (2009). BIOGEOSYSTEMICS--The Sonobioelectronic and Sonobioelectrogravitic Nature of Life on Earth and Why Pilot-Wave Subquantum Mechanics and Information Is not Enough, Life Physics Group - California, Adobe Acrobat

Emerging Technology, ArXiv (2016). Physicists Create World’s First Time Crystal
Physicists Create World’s First Time Crystal

Richard Lighthouse, (2020). The Blinking Universe, Lulu

Lacerta Files (2000). The Lacerta Files
Question/Answer 4:

"Yes. In order to explain that, one has to acknowledge the physical reality of the sphere of influence {Feldraum}. I’ll try to do it…wait just a second…you are going to have to separate yourself mentally from the illusion that that which you see is the true nature of the universe. It is, at best, the surface of a side. Imagine for yourself that all the matter here —you, this table, this pencil, this technical device, this paper— does not really exist, but that it is rather only the result of a field oscillation and a concentration of energy. All matter that you see, every creature, every planet and star in this universe, has an “information-energy equivalent” in the sphere of influence which is located on a main field —the general level {of things}. Now, there is not only one level, but several. Last time, I had mentioned that highly-developed species which is capable of changing levels (which is something completely different from the simple bubble changing, for bubbles are a part of each and every level). Do you understand? Dimensions, as you call them, are a part of a solitary bubble, bubbles or universal foam are a part of a level, and levels are layers in the sphere of influence, while the sphere of influence, acting in the capacity of single physical size, is essentially unending; it is composed of innumerable information-energy layers and general levels. There are in the sphere of influence no null-levels; all are the same, but they are separated by means of their energy conditions. I notice that I am confusing you now. I think I ought to stop with this explanation."
 

Pia tazama tundiko hili.

Mind and Form...
11 Agosti 2015 saa 09:17 mchana/ jioni
Yes I elder brother Steve... Give thanks that what i share, 'clicks' a certain connection button to the 'hidden attribute' of yourself; and would love to add some more from a friend who complemented the last post in an interesting manner as well...

====

In the dualistic model everything exists as a coincidentia oppositorum. Things exist because of the balance between 2 opposing forces. There's no violation of physical laws for something to spring from nothing as long as that something has a parity of an equal and opposite partner. This linear relationship between opposing parties is what creates spatial separation and dimensionality. This occurs when the initial linear separation is itself separated from its opposite akin to the vertical detaching from the horizontal.

The 'dot' or the singularity, which is everything considered together absent the notion of space or time, must be separated in order for the birth of space and time to occur. It all boils down to the manner in which the separation occurs.

The perpendicular separation of horizontal and vertical planes is the most fundamental of splits after the primary separation of direct opposites that produces the planar area. The first split produces linearity. The second split which is perpendicular produces the circular plane. It's the third separation, the Triple, where the vertical splits from the horizontal that reality as we know it exists and it's this relationship that I believe can be represented in the flower of life pattern. The adjacent circles when viewed as perpendicularly related take on a whole new meaning. The hexagon naturally arises when a central circle is designated as a focal point with the expanding layers being added around its perimeter but really the 3 dimensional shapes that appear within the pattern are just a way of relating the different planes to each other. In this sense any circle can be linked with any other to produce an infinite variety of shapes.

My understanding is that motion is just the manifestation of energy in one of its forms. The unfolding of the universe is a process of the horizontal becoming the vertical, the linear becoming the circular, the high energy state of oscillation becoming the more diffuse energy state of rotation. And yet the end state is the beginning state. The alpha is the omega only viewed inversely from a new perspective.

I believe that on the grandest scale you step out time all together and all is laid out like a vast multidimensional tapestry. Our experience is that of choosing a thread and following the course through. Even upon its completion that thread still exists because time as Einstein said is just a stubbornly persistent illusion.
People state that perpetual motion doesn't exist but if that were truly the case then this universe wouldn't be here. Everything is cyclical. Even scientists acknowledged that energy and information cannot be destroyed or created only transformed.

Nathan S Baker
====

We really connect to each other in these typical talks espcially if one and one is part of the same hidden gemstone of being in the other dimensionality...

So--as Kahlil Gibran would have said (As Almustafa in 'The Prophet' and rephrasing), if i am to talk--what should i really talk but that which is already moving within the sacred space of your being?

Sometimes these intriguing things have a catch with our souls--our hidden paths and will to become something--in space and time.


My friend Nathan, has hinted on Energy and Information--referring these two to the contemporary scientific postulations--the indestructibility of both; but then this extrapolates the fact that all physical activities that we observe do shift their form, from time to time/condition to conditions, however, there can be no end of change/transformation to the assumed temporal states of material substances... This is valid, and interestingly--it reverts into the baffling supposition of the non existence-- of either 'beginning' or 'end' for the material world-- of the universe that we tend to observe and 'know'...

So then this calls us to contemplate upon what we deem to be, or refer to it as 'time'; but let us first take a look at the fundamentals of space as the basis of defining forms.

Brother Nathan has reiterated the 3 Dimensional modality of reconstituting matter out of an imaginative 'dimensionless dot'--something which delights my imaginative senses for it reminds me of the works of Kant and P D Ouspensky in the book 'Tertium Organum', the Third Canon of thought(I am too fond of this book)... Trying to resolve the objectivity of sensual sightness out of a dot, flat then a block; again with state of imbibing consciousness of a subject...

We can use the analogies of the 'dot', but at the same time we've got to be aware that it could be inadequate to explain our visible reality properly. Again, it is fabulous to use our imagination and start from any point of our potent mental conception; however, there is one conception that to me seems quite plausible; that i have learned from an alien source, the Entity 'Bashar' as channeled by Darryl Anka; it explains our living cosmos as something like this :

"The totality of Time and Space is like the fabrication of an infinitesimal point of light, out of boundless dark void; so light and agile, to a point that it can move at the infinity speed--thus with that sense of motion and the virtue of it being infinitesimal, it happens to move in all directions and be in all space at the same time... And under certain auspiciousness of it crossing itself all over and over again and in certain geometrical fashions, it yields the occurrence and existence of all and everything--all that has happened, is happening and is to happen."

We can all thus note how fascinating and interesting Bashar's description is. Such is a 'dynamic' definition of all possible attributions of 'particle','motion' and 'position' by transposing all that into 'Probable Geometry'; whereby there is no real particle but something which tends towards the smallest size possible... No motion really, as such an infinitesimal point can be here and there at the same time due to its 'infinity speed' in all directions... Lastly but not the least to take, it dodges 'time' the way we prefer to observe it 😀 ... Only thing which is--is Radiant Point Source.

Now to me Solid Reality or Geometry is analogous to the 'Salt' Jesus used to talk about in many occasions... Jesus was fond of calling his disciples the 'salt of the earth and the light of the world'. We the people who are in search of true knowledge and mystery of life, are the disciples of the World and its hidden Kingdom and treasure. For the master, the awakened one in such grand reality, always glorifies the living abundance of its treasures, keys to its mysteries and practical maneuver of unconceivable immediate possibilities which can even transcend 'time' or 'space'. Being the living incarnate of 'The way, Truth and Life'... The whole world is already the womb which can deliver 'the Sons of God' whenever one or two people is/are ripe; or have risen to a sufficient level of becoming disciple. One who is ready to 'die and be reborn' spiritually. Thus a master can be a guide-- he can be a midwife to help with the process of 'death/rebirth' of the disciple. Passing of the 'old person' in a disciple into 'the new man' of the 'heavens' and its everlasting glory--if s/he continues to live on Earth his/her presence facilitates the process and activity of anchoring the 'Will' of the Higher Order; which is full of Grace, Abundance and Love, and thus probable Goodwill above All (when chosen as a healing path or exaltation as per the willed/accepted sanctifying conditions) 'That which has been', 'IS' and 'will be'-- what we can call 'God'...

Technically, in modern talking we can say, God is the higher form of information laying, programming and execution which tends to operate as separate intricate order of all and everything yet within the single intelligence of both lower and higher, inner and outer, Above and Below, Heavens and Earth. Geometry is then the key to unlock the door; when one's will is one with the will of the Higher or Intricate Reality then it is a portal to comprehend the 'Many Mansions' of the Kingdom of Heaven. Its from such intricateness, Jesus used to say quite frankly, 'The Kingdom of Heaven is at hand, it is within you'



Jesus talked about salt and light to foreshadow the alchemical mysteries--possible transformation and transmutation of things constituting the material and mundane life; but specifically in his case, to try link that with the possible evolution of human culture towards perfection or purity of certain hidden order; the one which is like a shinning gemstone with its glory of our collective seed/blossomed flower-- reality somewhere across the space-time reality. It is because of the underrated (mis)comprehension of Jesus' beautiful analogies to help us figure out the way to grand reality, Blessed One OSHO, couldn't resist to expound some in one of his discourses--to the disciples who would listen; and let it penetrate their heart, mind and soul as a dossier for spiritual rebirth; the talk which reiterated the essence of one of the gospels of Jesus; which came to be compiled in a book, 'Come Follow to You'.

Now the 'universal gravitation' orchestrating order of the universe--how does it add up to singularity, stellar discs and the 'expanding universe'?

In the trying science of today, it is said that it is impossible to determine both position and velocity of a subatomic particle(Heseinberg's principle). So an electron could be nothing but a fictitious object which seems to explain some 'physics in demand' and in some occasions (then it is to say-- partially). Experiments can accommodate something like the existence of it as a particle--yet at the same time, under different settings (conditions) attributing the same thing to a 'wave like' phenomenon. So again, it is to note--all this much is the same with the revolving planets around the stars... You cannot tell for certainty what is the exact position and velocity of the Earth(Planets). Though there is an average to its velocity to periodically exact one year(again there is long and short year), but even the motion of the earth is not constant--for it is revolving the Sun while reverberating to the mysterious 'breath'... and thus I prefer to link such orchestrating power to the 'heartbeat of the Divine'. At least we can say the earth is nearly spherical although it is a compromise--something which is quite intriguing to observe again--apparently reality avoids 'perfect regularities' of shape from time to time. Therefore, evidently, we are pushed to explore its forms in between the flat, cylindrical, and spherical abstractions; thus probably through a 'cone'(Therein conic sections in consideration).


From the above, it can be noted that a cross section of a flat surface/shape is single dimensionality--a straight line. Likewise for cylindrical form is a two dimensionality--a 'square' can fit a bill under auspicious dimensions. A 'triangle' is for the cone. Then again an auspicious condition to yield a 'square' or 'equilateral triangle' is exacted by a 'circle'-- to influences and incite regularities. And here is where the 'Sacred Geometry' begins to yield its significance in the course of 'blueprints' and 'subtle influence' behind all shapes and form; and in relationship to intelligent-able forms of motion or pattern.

I love to the core the 13th chapter--13 significant lines, of the book of the mystical Apostle--Paul's first epistles to the Corinthians... I was born the 13th day of month of January not by mere coincidence, LOL... And chapter 13 of that book talks about LOVE and Knowing things in part, and a 'Hope' to come into 'knowing' in full when One comes to 'meet' himself as a full grown one -- and as the Divine would have come to reflect him in full... What if the Scientists who don't have a thing for Love do miss something in their inherent comprehension of the grand reality? What if the 'Universal Gravitation' and Harmony of all motions is the effect of hidden cause which is 'Love' as the core essence of preservation of 'meaningful order'?

What is it precisely, that Paul talks about-- mentioning the 'mystical knowledge of God' that which is for those who are meant to comprehend it, and are ordained by the spirit of Truth -- inherent in those who seek that truth, to their innermost core of inquiry and pursuit?:

'But we speak the wisdom of God in a mystery, even the hidden wisdom... But as it is written, Eye hath not seen, nor ear heard, neither have entered into the heart of man, the things which God hath prepared for them that love him... But the natural man receiveth not the things of the Spirit of God: for they are foolishness unto him: neither can he know them, because they are spiritually discerned. But he that is spiritual judgeth all things, yet he himself is judged of no man. For who hath known the mind of the Lord, that he may instruct him? but we have the mind of Christ.

How can we decode the significant keys of life and reality out of what Paul says, such to unveil the physics behind all matter and motion? Lets correlate things and find the figurative correspondence of man, universe, destiny and time.

Novelty and expiration in all human experience can be resolved to a certain 'God Function'. The full expression being a 'complex function', as it is with the language of the mathematics, inherently consisting of 'Real' and 'Imaginary' variables. This could be empirical to all forms and formulas of life, material and existence(In totality, its talking 'space-time'); But how are both variables of the equation tied to each other? If there is a hidden course yet also a visible attribution to all life--what is the intermediary of all matter? What if all paths of motion and floating object is simply a 'slowing down' of 'hidden exaction'-- thus supposing both particles and motion are in fact a certain 'illusion' trying to effect another un-manifesting 'particle'; and through the living essence of some sort of a 'complex function'?

We all follow all of this mainly because we have a mind... And this mind is the key to all enigmas of life. Through the mind we may think we know, yet all that we really know could be nothing but imaginative constructs out of complex information processing and sensations... What we 'see' may not be exactly what we interpret, believe/deem to be or infer. Let me truncate this mind talk by suggesting the strange possibilities for anyone to consider... (1) Mind is not necessary something within ourselves, mind can be a medium which is continuous to all forms--both visible and invisible to our senses or perception. (2) We 'qualify' the mind in order to process information, but our crucial essence of 'mortality' could be something beyond mind. (3) Mind is the actual medium which actuate, substantiate and subsisting the 'complex function'. Therefore if we really seek to know who are we really, lets prepare to penetrate and know the depths of our purest desires, seed potentialities and culmination of being--something which suggests that we have a mind which serves our 'lower' nature, delighting in mixture of truth and falseness; yet again there could be a 'higher' part in us which represents the true light and blueprint of all and beyond all causality. Truth of the matter being, all occasional novelty or expiration in human experience save nothing but exacting another hidden order of 'glorification'--salt and light in another dimensional structure/essence.

By Christ Mind, Paul supposes higher nature which consummate both light and darkness of the ordinary qualified mind. Towards unfiltered infinity intelligence, is the ability to see things in full; to meet yourself face to face... To get to know yourself as the Divine, knows you to be One; a particle coming in from the cold only to realize all its ordeal in the domain of 'space-time' that such has been nothing but grand illusion... Having been a complex self determinism in the dark; with the perpetual self conscious mechanism to condition oneself in a 'limited environment' and 'condition' we can now refer as space-time.

That has been a talk on mind in relationship to a self conscious entity; situated in the universe of an infinity active intelligence.
Mind is the agent to animate such infinity intelligence... Now talking about infinity intelligence, we are thus stepping into the realm of true endless possibilities--knowledge and instrumentation, mastery or limitation, imitation/correspondence and magic, materialization and de-materialization...

So lets get down to the physics of mind, light and form; by light i refer a close analogy of light to the 'Radiant Point Source' of Bashar... We 'qualify' the mind to effect 'certainty'; by the virtue of a 'triangle'... This is very important to all who want to study all and everything; from Perpetual Mechanics to Quantum Teleportation. And again, if you desire to sort out a definite 'piece of information' out of an infinite intelligence consider an 'imaginary circle' as your decoder to filter out 'imaginary infinite directional paths' and perfecting 'real coincidences'(exacting rudimentary order out of pervasive chaos).

'Body, Mind and Spirit' or 'Father, Son and Holy Ghost' are three aspects of all manifestations. It is mentioned in various theological doctrines that God is One in Three, TRINITY. In as much this is to be true in actual essence, all our knowledge and experience is to change forever. We can come into a certain interesting comprehension... that we actually live in body-mind-spirit 'complexion' in all scales of being and activity. Lets truncate the talk regarding this complexion by suggesting the possibilities of existing various fractal 'densities' of self awareness, comprehension and influences which invigorate both animate and inanimate things.

Discretion of forms is possible through subtle rhythms in conjunction to vibration... preciously correct to refer such conjunction as the kind of 'sympathetic vibration'... A mind can be a tool... to attune rhythms and to will a pattern. Mind can be a bridge between two adjacent dimensions of visible and invisible worlds to exalt or demote the qualities and attributes of objects under its influence. Objects under influence 'qualify' their state of being/manifestation with some sort of 'magical link' to a certain 'organic constitution' which is hidden/un-manifested--it is the mind which determine the order, state and level of its 'being'. Thus by the term 'densities', it implies that certain context of activities of 'inanimate things' could be in service to~by manifesting the hidden aspects of certain complete 'sphere of influence'. The terminology of a 'Soul' for example, can serve to explain such continuum of reality; to suppose some sort of invigoration-- suggesting the hidden presence of the typical 'sphere of influence'; when the tapestry, complexity of manifestation and causality are associated with something like a 'self', then something like the 'higherself' or even supreme soul can serve the purpose to illustrate the complete scenario and saga of 'Being'. Therefore the soul of anything is a focal point of all assuming intelligence to exact its core activity, manifestation/de-manifestation; and its relationship to other discrete forms of being and activity at certain level of interaction and abiding. It is the living actuating 'information' out of infinite possibilities--infinite traces of a 'single radiant point source'.
 
Pia tazama tundiko hili...

Kutoka: Mwongozo Hai kuelekea Uhuru Halisi seh. V
5 Septemba 2011 saa 12:26 Asubuhi

Elimu yenye kuegama katika kumbukumbu ndiyo shughuli iliyotapakaa kwa sehemu kubwa ya watu wa mataifa-- ambavyo pia ni kielelezo cha jinsi gani tamaduni zao huhifadhika kwa mashauri yenye kupenyezwa kutoka kwa wakubwa kwenda kwa wadogo. Ule uwezekano mwingine wa kiakili ambao waweza kuleta mashauri mapya huonekana ni 'kipaji' maalum kutokana na mtu mmoja mmoja na kumbe huenda hiyo ni jinsi yenye kuwezekana kwa kila mmoja pia; ijapokuwa tu kule 'kulala usingizi' kumewashika wengi basi na wao wakashindwa kuamka. Wachache walioamka waweza 'kutotambulika' miongoni mwa wale wengi waliousingizini. Huku kutoka usingizini, watu huamka kwa jinsi ya mtu mmoja mmoja; na wao huzindua watu wengine kutoka katika ule 'utabia wa kishirika' ulioni mpofu kwa zile hasa adha halisia za ujinga wa kutokutambua muktadha mzima wa mtu na mazingira yake kwa wakati. Wakati unapotimia wanadamu walioamka watawaamsha wengine wengi wasio zinduka kwa msisito wa muktadha mpya wa elimu usioegemia katika utumikivu wa kumbukumbu pekee ila pia kwa dhanania na uishirafu ujao kwa akili ya juu. Huu ndiyo utakuwa muundo wa elimu katika Zama Mpya ambayo itashughulika na sayansi ya antakarana ili kuleta usanisi wa mashauri ya akili ya kawaida ya mtu na muktadha wa uadilifu wa maumbo na nyenendo zote za maisha na uhai. Kwa kuwa elimu ijayo kwa minajili ya kumbukumbu ni 'mfu'-- ila tu hiyo 'hupata uhai' kwa nidhamu ya kimtazamo inayofanya muktadha wa usikronizi na 'mafikara hai' ya uzima wote.

Muktadha wa elimu wenye kutanabai marefu ya mtu kwa kuzaliwa na kufa kwake katika jamii yoyote duniani yaweza kusemwa kuwa yote si sahihi kwa kadiri ya uhakika wa matukio. Kwa kuwa jinsi zote za kutanabahi marefu na mapana ya madhahirisho ni zao la kumbukumbu na ile fanusi(sifakazi-- mfano wa utambi uwakao kutoa mwanga ndani ya taa ya mafuta || hisabati, mahusiano ya elementi za utathminifu katika muktadha wa mafungu ya kadri ya kusema ni seti) ya Uzima uletayo udhahiri wa 'uhai' wa kitu ama viumbe. Ndivyo hivi Historia na Jiografia vizingumziavyo katika mashauri ya kiuchambuzi wa matukio na tarehe ama tena basi kusema watu na kudumu kwao katika maeneo yenye mipaka juu ya sura ya nchi na zile kazi za wao kujishughulisha katika mazingira yao hayo husika ni ile tu seti ya muktadha wa nje wa mambo; kwani kote katika wakati iko hali kwenye kila nukta yake ambamo hiyari yake yeye mwanadamu yaweza kubadili mwelekeo wa mustakabari wake na hivyo kubadili 'taswira' ya utu wake pia.

Basi elimu bora yenye kumfaa mwanadamu kwa kila nukta yake ya kuishi ni ile yenye kumtia yeye yale mashauri ambayo hayatamfunga yeye na kilichopita bali kumuandaa yeye na hata mielekeo mingine tofauti ndani ya kanuni za mienendo na tabia za mazingira yanayomzunguka. Tathmini dhidi ya madhahirisho na wakati ya mtu, ikiwa yaongozwa na mashauri ya 'kumbukumbu' kuna uwezekano wa udhanifu wa kimawazo usio sahihi japo waweza kufaa katika mazingira haya ama yale. Katika sura pana mno yaweza kutokuwa sahihi, vilevile katika sura ya muktadha mdogo sana wa nafasi yaweza kuwa si sahihi pia.

Na hivi muktadha mzima wa msimamo wa maisha ya mwanadamu duniani ni wenye kuhitaji mashauri ya hekima ili kutangamanisha sehemu ya mienendo ya maisha ya mtu na ile mienendo mipana ya ulimwengu na madhahirisho katika wakati.

Japo mtu hufanyika na kuwa kiumbe, hakika ya 'utu' wake yaweza kuwa ni marefu na mapana sana ya 'wakati'. Vyote vifanyavyo sura yake katika ulimwengu wa maumbo na wakati ni tu mfumiko uliosukwa kwa 'ukweli' ulihifadhika nje ya hata mwili wake mwenyewe. Na hivi maisha yake kuzunguka mhimili usionekana na hali 'ukikatizia' kwenye mwili wake na huku ukihuisha nuru ya ufahamu wake dhidi ya vyote vingine vilivyodhahirika. Hakika ya 'utu' yaweza kuwa ni mapana ya zaidi ya urefu wa safari moja ya mtu kutoka kuzaliwa hadi mauti. Kwa kadiri hii basi, kuzaliwa na kufa si kitu ila tu sehemu ya 'mpango mzima' wenye kutangamanisha utumikivu wa maumbo na sura katika muktadha wa uzima wote. Hata mtu akijitahidi sana kupata kina katika nuru ya ufahamu wake ataanza kuihisi hakika ya 'uto kufa'; lakini kwa mashaka ya akili yake ya chini atabaki ni mtumwa wa mashauri ya 'marefu yenye ncha'. Kadri mtu afanyavyo antakarana ndani ya Saikia yake, yeye huanza kuwa na ujasiri wa kuchunguza mambo yote na basi hufika wakati utangamano kamili wa mashauri na maono kwa jinsi ya ndani humfunilia 'Kweli' ya uzima wote.

Katika muktadha wa Uzima wote hakuna 'ukiasi' na hivi pia hakuna 'upahala'; hili huzungumzika kuwa ni 'Roho' au hasa tuseme 'Roho wa Uzima'. Muktadha wa Utu 'huzunguka' katika 'Roho wa Uzima', japo kusema haya yote ni dhana tu katika urahisishaji wa kudadavua mashauri. Roho ni kitu kisichoweza kuja kuonekana na wala kudhahirika kwa jinsi tufahamuvyo maumbo yote. Na hivi hakuna kitu kama 'roho' mfano wa chembe ndani ya kitu au mwili wa kiumbe. Shani ya sura ya mambo yote katika madhahirisho na wakati ni Roho. Shauri la 'Roho' halina budi kutatiza ung'amuzi wa kawaida kwa akili ya mtu kwa kuwa Roho ndiyo kitu pekee chenye 'Uhai' na 'Uzima'. Na hivi tutajapo 'nafsi-roho' au roho ya kitu fulani ni tu kutanabaisha muktadha wa mbegu ipatikanayo katika mwili wa madhahirisho ama wakati ambamo sura ya 'uhai' na 'uzima' inayaweza 'kuhuishikia' maumbo na kuyapa hayo sura ya mienendo ndani ya mienendo ndani mipaka ya uhifadhiko katika mifumo ndani ya mifumo--yote haya katika sura ya upana usio na mwanzo wala mwisho.

Kutokuwapo kwa 'mwanzo' wala 'mwisho' ndiyo huleta shauri la muktadha wa uzima wote kutokuwa na mwanzo wala mwisho. Na hivi 'Roho ya Uzima' haijapata kuwa na mwanzo na wala haitakuwa na mwisho. Binadamu hujibabaisha yeye mwenyewe juu ya mashauri ya yenye mwanzo na mwisho kwa kuwa 'utambuko' wa unafsi wake ni wenye kukirimika katika ulimwengu wa madhahiriko. Penye madhahiriko pana mienendo, penye mienendo pana wakati; na hivi muktadha wa 'Roho ya Uzima' katika mashauri ya kiuwakati hutajwa ni 'Uzima wa Milele'; na hapa tena akili ya chini ya mwanadamu hujikwaa mwendo kushindwa kuikamilisha safari ya kuimaizi 'Kweli' ya 'Mpango Mzima' ilivyo ni Roho.

Japo maumbo huchukua sura ya mienendo, picha ya maua yake katika uwezekano wa kutathminika kwake kinjia na sura huwa ni 'fikara' katika mbegu ya kiroho. Uhakika wa hiyo mienendo ni hizi basi tuziitazo ni 'Kanuni za Asili' za maumbo kwa hali na tabia zake tuwezazo kuona na kurajisi katika kumbukumbu zetu; nazo zikawa ni sahihi katika kila muktadha wake katika wakati na kwa tena kwa mazingira tunayotanabahi uhalisia wake. Utu nao husukumwa kwa miingiliano ya mienendo ya jinsi nyingi japo vituo vyake katika mapito yake ndiyo huzaa taswira tuitajayo kama 'nafsi' na pia 'kheri' ya kufanyika kwa jinsi ya uanadamu. Tofauti na inavyodhanika kwa wengi ya kuwa utu ni ule ufupisho wa uhai wa mwili, upana wa kuyatazama maisha unaweza kufunua kwa mwanadamu muktadha mungine wa ukweli kuhusu uanadamu. Bila huo mashauri yote ya mwanadamu ni yenye kutambaa chini kama mtoto mchanga na halafu ni dumavu. Ni upeo ujao na kina cha mafikara na ufahamu ndivyo antakarana ya mtu huimalika na hata kumng'amulisha yeye pia yale ambayo watu hufa na kuzaliwa na kufa na kuzaliwa bila kutambua uhakika wake katika vizazi vyote vya wanadamu.

Maumbo yote ni maua ya Roho—Ulimwengu wote umefanyika kwa jinsi ya Ua la Uzima. Uzuri na Urembo unaofanyikia madhahiriko yote na wakati ni kutaniko la mienendo katika mifumo inayoingiliana na hivi kufanya vituo vya sura na ishara ya usifaakili unaofanya vitu vyote. Usifa akili huu ni fanusi ya Uzima—muktadha wa unyoofu na mawimbi yaliyoko kote na mote. Mawimbi haya husukuma 'chembe' za maumbo kutungika katika udhahiri wa sura na migando kwa neema ya nguvu ya 'unyoofu'. Jinsi hii pia ndiyo muktadha wa usumaku na umeme utawalao madhahiriko yote. Usumaku na umeme hufumanishwa na roho; na katika madhahirisho yote ni mbegu ya utatu—jinsi ya miale ya nuru na usumaku na uhifadhiko wa hayo yote mawili katika mapana zaidi. Hivi kuendelea pasiko kikomo. Uvumbuzi uliodhirisha penye usumaku pana umeme ndiyo pia uliodhihirisha penye ugani wa umeme au sumaku katika kupambanishwa kimraba—kadri ya mielekeo ya mitiririko ya nguvu kwa kile chenye jinsi ya umeme na kile chenye jinsi ya usumaku, hivi viwili huzaa msukumo wa mwendo katika mwelekeo wa tatu ulio ni mraba kwa uwanda wa usumaku na umeme wenyewe; kitendo cha kuepana na hivi kusogea mbali. Katika mashauri ya taaluma ya umeme husemwa ni 'sheria ya Lenzi'; ile yenye kufafanua ufuaji umeme au utengenezaji mwendo katika mitambo yenye kuzunguka kiumeme. Hii pia ni siri ya mfumiko wa madhahirisho yote. Mielekeo ya kipande tatu hufanya ule kama ni muktadha wa marefu, mapana na kina kwa tofali la mraba. Na ni jiwe la msingi katika kutathmini hali za maumbo na mienendo yote.

Ijapokuwa maumbo huweza kujipanga na kuitengeneza sura fulani bayana, hili hufanyika kwa muktadha wa maumbo mengine yaliyo madogo zaidi katika muktadha wa madhahirisho yote. Madhahiriko mengine huchukua sura kwa mitiririko ya maumbo yenye kubadilika muktadha wake katika bahari ya mawimbi ya uumbiko wote; hii bahari isiyokuwa na mwanzo wala mwisho wa mapana yake. Madhahiriko yenye sifa hii hayatathminiki kwa bahari yenyewe ama mawimbi ila tu ule uchochezi wa kufikia 'Ua' fulani. Basi ua hili huwa ni mbegu na tena huwa ni 'unyoofu' wenye kuweza kuratibu mpangilio. Hili kuwezekana tu pale ambapo pana kipeo cha tatu cha hadhi ya madhahiriko yote; kile chenye kukirimu mfanyiko wa sura ama umbo—hili hufanya 'kizio' cha umbo ama chembe; namna ya uhifadhiko wa sura ya maumbo toka katika mapana ya kiujazo yasiyo na kikomo. Maumbile yote kwa jinsi ya ukutano wa 'unyoofu' na 'mawimbi' hayana 'hakika ya milele'. Hakika ipo kwenye yote mawili uwepo na utowepo wa vitu vyote. Na hivi yote yaliyodhahirika si 'Kweli' kamili ila tu kujumuisha yale yasiyodhahirika—Roho ni yote mawili kwa 'wakati mmoja'.

Twaweza kutanabahi muktadha huu wa udhahiriko wa maumbo kwa kulifikia lile fumbo la Yai na Kuku. Swali la kipi kilianza kati ya Yai na Kuku; limekuwa ni msingi wa mdahalo wa kifalsafa na sayansi ya maumbo. Pia limekuwa ni fumbo katika kujaribu kusimamisha mashauri yasiyo na mzozo juu ya maumbo na asili; uwepo wa yote na kile kilichoyafanya yote—asilishi ya halisia yote. Ikiwa kifaranga cha kuku hutotolewa kutoka katika yai, sasa je, bila ya yai awezakufanyika huyo kuku? Yai hutagwa na kuku, sasa je, bila ya kuku laweza kufanyika hilo yai? Basi tena, iweje tupate kusema ni kile hasa kilianza kati ya kuku na yai?

Kadri hiyo hiyo huleta utata katika muktadha wa udhanifu kimawazo katika kuzungumzia ulimwengu na mungu. Watu wa makabila mbali mbali wanamashauri yao yenye kumzungumzia 'Mungu'. Wakisema ni Mungu aliyeumba ulimwengu wote; swali linaloweza kukaribishwa kwa kufuatia huwa ni basi kwamba kuuliza na yeye huyo Mungu aliumbwa na nani tena? Kwa kuwa vyovyote vile katika muktadha huu, falsafa zote za wanadamu hupwaya kwa kukosa 'maana' ya dhati. Na ndilo tatizo la msingi katika mashauri yenye kufuatisha dhana na mantiki. Basi ndivyo huja maelezo yenye msigano katika udadavuaji wa muktadha mzima wa wezekano halisi kwa ukweli wa jambo na mambo yote. Wapo wanaodai kusema Mungu ndiye aliyeumba ulimwengu na yeye hakufanywa na yeyote mwingine; makabila mengi duniani aghalabu shauri hili lipo miongoni mwa mashauri ya dini zao za asili. Inasikika kupata kusemwa pia kuwa Mungu 'hakuzaliwa' na wala 'hakuzaa'... Lakini haya yote ni kukadirisha tu ugumu wa kufumbua fumbo lenyewe katika minajili ya dhana na mawazo ya jinsi ya utumikivu wa akili ya kawaida ya watu wenyewe.

Kuku na Yai ni nelibini--'kaleidoskopi' ya uzima kamili wa kadri ya vyote viwili; kumaanisha basi nimang'amung'amu ya madhahirisho—mabadiliko endelevu yenye kubadilishana sura na mwonekano kwa kadri ya haraka na harakati zake na tena ndani ya vituo vya muktadha wa kiumbe; mbele ya macho ya mtazamaji. Kadri iwezavyo kuzungumzwa kusemwa ni kibayolojia, muktadha kamili wa kiumbe chenye kutajwa hai ni jumuiko la chembe ndogo ndogo zenye kuungana pamoja katika kudhahirisha sifakazi maalum; wakati mwingine yaweza kuwa chembe moja pekee ama mkusanyiko chembe kufanya muktadha sifakazi moja kama 'tishu' na tena hata 'tishu' na tishu' kufanya hadhi kazi pana zaidi. Chembe chembe hizo ndiyo 'kizio' cha muktadha wa uhai wenyewe wa kiumbe hai chote kizima. Katika mfanyiko wa viumbe hai ni chembe hai hukomaa na kugawanyika kimaumbo kamili na hivi kuongezeka ukubwa kwa kadri ya jinsi ya kiumbe hai husika. Ifikapo ukamilifu fulani wa kimaumbo kiumbe halisia huchukua sura yake ya uhai na kukidhi ufafanuzi wa hicho 'kuwa hai'. Kisha katika muktadha wa jinsi ya kiumbe kimoja hicho nacho hukunjuka sura ya shani yake na kudhahirisha harakati, mielekeo na mienendo ilivyo hiyo minajili ya nelibini kulingana na kudra zake za kufanyikia.

Yai ni mapana ya kituo kimoja na kuku kuwa ni kituo kingine. Katika kuku twaona 'hiyari' ya wawili ili kutunga yai moja. Huchukua tembe na jogoo kugusana kimwili ili kutunga yai. Basi kumbe huitaji yai na yai ili kufanya kuku na kuku kusudi yai-kuku-yai kudumu mwenendo wake kinelibini. Na hivi katika yai hakuna 'hiyari' ila tu ubidifu wa kuwa aidha jinsi ya kike ama ya kiume. Kati ya yai na kuku kuna mpaka wa muktadha wa kuja kudhahirika 'kuku'. Yai laweza kustahimilisha mawezekano yote iwe ya kike ama kiume lakini kuku hana budi kufanyika kwa jinsia. Akiwa tembe hawezi kuwa jogoo na akiwa jogoo hawezi kuwa tembe; ila kwa namna ya kipekee, yenye kuhusisha 'kutaniko la kimwili' na tena palipo na jinsia mbili ni moja yenye uwezekano wa moja kwa moja kuendeleza madhahirisho. Jinsia hiyo ni ile ya kike. Ni jinsia ya kike yenye uwezo wa kustahimilisha mtungiko wa maumbile yenye kuja kufanya madhahirisho ya kiumbe na jinsia ya kike au kiume; na hivi basi kubakiza kuwa katika jinsi ya kiume ndiko kwenye mbegu ya jinsia moja kwa wakati na halafu kwa kutawaliwa na 'mazingira' fulani yasiyofahamika vema lakini kuhusisha uwiano wa kimazingira yenyewe ya kuwapo kwake viumbe hai na saikia jumuizi--hali ya 'kutotabirika' kwa jinsia itayofuatia baada ya kitendo cha 'kutaniko la kimwili' na mtungiko mpya.

Kufanyika kwa kiumbe hai ni kwenye kubeba sehemu ya utambuko wa kimwili na jinsia. Viumbe hai kama wanyama si vyenye kujitambua kwa kila kitu kinachofanya ama kufanyikia ndani ya miili yao. Utambuzi wa kimiili huwa na kadri ya 'uso' tu wa miili yenyewe na mengine yote ni maendelezo ya utumikivu wa akili za viumbe vyenyewe. Kwa mfano mwanadamu hawezi kwa hakika kushuhudia kuwa ana maini ndani ya mwili wake na hayo yamekaa wapi ndani yake; hawezi kusema maji na chakula katika mwili wake husagwa vipi na kusharabiwa katika mwili wake wote. Pia hawezi kueleza pumzi avutayo ni yenye kustahimilisha vipi viungo vya mwili wake na mapana ya kutumika kwake. Hawezi kuzungumzia haya kwa hakika na angali yote yakiwa ni sehemu ya muktadha 'unaotathmini' uzima wake kwa wakati na msukumo wa pilika zake za kila siku. Viungo vyote vya ndani ya mtu na viumbe pia hufanyika kwa tishu zile zenye kufanywa kwa chembechembe ndogo ndogo na tena zilizo ni 'kizio' cha uhai—seli. Hata viungo vya ndani vya nyama kama moyo na ubongo vyote ni kutaniko la tishu zifanyazwo kwa seli za idadi nyingi sana sifanyazo kazi kwa utangamano unaratibiwa na 'mawimbi ya uzima'. Mawimbi haya ndiyo yale yenye kuja kwa sura ya rithimu. Rithimu hii huratibu tabia na mabadiliko ya seli zote; kuanzia kutungika, kukomaa na kufa. Na hivi japo kiungo chaweza kuonekana kudumu kwa miaka mingi, seli zinazounda viungo hivyo si za muda mrefu kama dhahiriko la kiungo chenyewe. Seli nyingi katika miili ya viumbe hutungika, kukomaa na kufa na hali uzima wa kiumbe kuonekana uko pale pale... Hata mwanadamu afikapo uzeeni, mwili wake wote ushakufa seli nyingi sana na mara kadhaa kulingana na rithimu na majira yaletwayo na mawimbi ya uzima. Kwa kuwa seli hufa kwa kupokezana na nyingine mpya zilizotungika na kuongezeka, mtu kwa kadri ya utumikivu wa akili yake yeye hujionana ni yule yule siku zote za kuishi kwake.

Basi ndivyo tunaweza kusema wazi 'mtu' ama 'kiumbe' si mwili hasa. Kinyume na inavyochukulika na kufikirika hata katika ulimwengu wa sayansi leo ya kwamba mtu hufanyika na 'kutosha' kuwa mtu kwa ile mifumo na mienendo yote ya kimwili; huu si ukweli—ni nusu ukweli ulio ni hatari kuliko uongo kamili. Kwa kuwa ile sehemu yake yenye kuonekana kama ni ukweli kuwa ni hivyo yaweza kumzuzua mwenye kutazama na kumpelekea yeye kwenye hitimisho la mashauri lisilo sahihi. Uongo kamili hukosa shikilizo katika halisia; lakini 'nusu ukweli' inacho kiungo chenye 'kujishikiza' kwenye 'halisia' kamili. Basi mtu ni 'kweli' iliyochanganyikana na 'usikweli' na tena kwa jinsi ya ajabu kujitahidi pamoja katika kudhahirisha sura ya 'utu'. Mwanadamu kiumbe kinachobebwa na viumbe katika michakato ili kukirimika 'sura' yake. Utu ni mbegu ijayo kwa muktadha wa 'Saikia' kamili ambamo ndani yake mna yote 'yanatosha' kukadirisha muktadha wa mtu katika kudhahirika juu ya mwili wa nyama.

Ndani ya Saikia kuna muktadha wa vitu vitatu kuchambulika kipekee--nafsi-roho, akili na nafsi. Nafsi huhusisha muktadha wa akili, kumbukumbu ya mtu kujichukulia katika mazingira yake akitumia mwili kama chombo cha 'uhalisia' wake. Huu ni upande wa chini wa akili ya kawaida; upande wa juu wa akili huwa ni dhahania kwa uadilifu wa kiutu kwa unafsi wa mtu mwenyewe. Haya yote huakisi mawezekano ya Ua la ndani la mtu lililo ni nafsi-roho; sehemu ya sura ya 'mpango mzima' kwa utu ndani ya Roho wa Uzima wote. Nafsi-roho ndiyo hii 'Sonafi' katika mwingiliano wa mwili, akili na uzima—Jua la utu lenye kuungazia uwezekano wa neema zote za mfanyiko na mdhahiriko wa ubinadamu.

Uhalisia wa Saikia ifungamanavyo na mwili ni jinsi ya msalaba; japo mwili hutungika na kufa, saikia ya mtu ya mtu haitungiki na kufa na mwili. Mapana ya kuzaliwa na kufa si mapana na marefu ya Saikia ila tu mkatizio wa Saikia yenyewe katika mfanyiko wa mwili. Saikia ni 'mgeni' katika mwili na tena mpangishaji tu. Saikia huchanua na kukomaa katika mwili na huku ikiendesha mwili kwa sura ya hivyo hivyo na hali mwili ukatapo pumzi Saikia 'hujikunjia ndani' kama mbegu yenye kusubiri na kuhitaji pahala pengine penye kustahili hiyo kumea na kuchipua tena. Mbegu ya 'utu' ina usiku na mchana kama ilivyo katika mizunguko mingine ya kiuhai yenye kuja na misimu na majira—rithimu zifuatishazo namna ya 'mawimbi ya uzima' na 'wavu' wa maumbo-wakati. Iwapo katika giza huwa ni 'chembe ya ndoto' na mang'amu ng'amu yake; japo hayo yote huwa ni ya mpito tu. Yale ambayo watu wa makabila huzungumza kuhusu 'mahala pa wafu' ni sehemu za mpito ambazo 'hazina uhalisia' wa kutosha kuneemesha 'mbegu ya utu'. Ni pahala penye giza tororo ama mbalamwezi kwa Saikia ya mtu japo upo ufundi wa kutumia sehemu hiyo ya mpito katika 'kuhifadhi' kwa kana vile 'kugandisha' kadri mbali mbali ya uwezo na karama mahususi zilizopata kufikiwa na kutambuliwa ndani saikia ya mtu aliyeachia mwili. Na basi Sakia ya mtu huweza kunasa katika wavu wa maumbo-wakati na kudhahirika mtu mwenye kuishi upya.

Saikia ya mtu inasapo katika mtungiko wa mwili mpya hutuama kama ngozi ndani ya ngozi kiutumikivu wa akili—kama vile kitunguu kinachofutikwa na maganda yake ya nje na ndani. 'Sehemu ya nje' hufanya muktadha tuli wa akili katika ufahamu mbalali na ile ya ndani kuwa chipukizi la 'Saikia changa' na hai--kuendana na mwili na mazingira mapya. Ndiyo hivi kuwa kila jambo ambalo mtu hutenda katika ulimwengu wa madhahirisho hubakiza kumbukumbu katika Saikia ya mtu mwenyewe. Katika kiini cha saikia na mwili ndipo sonafi hutawala shani ya yote na kudra za kipekee kwa mtu katika 'mapana' ya wakati na uzima wa mwili. Sonafi ni mhimili wa 'utu' katika mtu. Sakia ni kioo kinachooakisi sehemu ya nuru yake kujijenga rangi na muktadha wa kimadhahiriko. Sonafi imefanyika kwa kweli yenye kupita jinsia ile ya kike ama kiume... Na hivi kudhahirika kwa mtu katika mwili wa kike au kiume ni matokeo tu katika ulimwengu wa madhahiriko. Kadri Saikia nasavyo mwili yaweza kunasuka na tena kunasa tena na tena... Kitendo cha hiki ndivyo kusema utwaaji mwili na marudio yake. Ndivyo hivi mtu aweza kuvuna alichopanda hata maisha mengine nje ya upana wa kipindi cha uhai wake mmoja. Ukoseaji katika njia zenye kheri katika kanuni za 'Roho wa Uzima' hubaki kuwa ni deni katika saikia ya mtu nayo hutawala majaliwa yake katika hata mwili mpya kwa kuwa ni sehemu akili ya mtu huyo huyo kutokana na ushawishi wa fahamu mbalali. Yale yote yenye asili ya ushawishi wa mawazo na hisia kama chuki na hofu hudumisha udhaifu katika saikia ya mtu yenye kuzaa unyonge wa mtu hata maisha mengine. Vile vile misukumo ya vitendo yenye kuambatana na hisia kali hubaki katika saikia ya mtu kumchochea yeye na yale yatakayo mpa yeye sifa ya 'hamasa' ya nguvu hata katika utwaaji mwili mwingine ambao haukusababisha uhalisia huo.

Watu na jinsi mbalimbali za kitabia na kisaikolojia huzaliwa kutokana na matunda mbalimbali ya matendo yao yaliyopita katika muktadha wa utwaaji mwili na Saikia. Saikia hufanya ladha ya mtu mwenyewe kwa kadri anavyohusiana na mazingira—madhahirisho na wakati. Ukali ama upole wa mtu ni mazao ya nuru ya sonafi ilivyochakatishwa katika saikia ya mtu. Yale matendo yenye matendo 'machafu' ya mtu kutinga nuru kupenya na kuakisi hiyo kwa matumizi hasi ambayo yatapelekea marudio ya 'uchafu' na pia mtu kuvutika katika uchafu zaidi. Matendo masafi ni utendaji wowote wenye kheri na tena unaoendana na karama njema za 'roho wa uzima'. Kila mtu afanyavyo yenye kheri yeye hufunguka zaidi kutambua yale ambayo 'Roho wa uzima' wote hukirimu katika ile njia ya mchanuo wa utu. Matendo masafi ni matendo yajayo na 'usafi wa moyo'. Usafi wa moyo hutambulika na kurajisiwa katika Saikia ya mtu pale matendo yake yanapokuwa si yale yenye kuakisika na sura ya uchafu bali ile kheri ya mienendo yenye kudhahirisha mhifadhiko wa viumbe hai na maumbo yote katika mazingira ya utu. Uchafu huja kwa mawazo mabovu, ujinga na kasumba na hivi binadamu kwa asili ni kiumbe aliye katika uwanja wa mapambano. Silaha yake kuu ni nia yake safi na isiyo na mawaaa katika kila analoazimia kutenda—kuwa kwamba basi hilo lipate ile kadri ya kheri na kumuepusha yeye na mikosi. Hili lafanikishwa kwa yale mawazo safi yaliyorajisiwa katika saikia yake kwani hayo hujenga nguzo imara katika kukabili ujinga na mazoea mabovu. Na hivi binadamu daima aweza kusafisha maovu yake kwa kuitafuta ile nia safi yenye kuongoza katika usahihi wa katikati. Kufanya hivi basi, kutaisafisha njia yake na majaliwa yake kwa kadri ya stahiki ya usafi wake, asili ya makosa yake na 'msongo' wa wakati.

Basi viumbe vyote kimefanyikia kwa saikia za namna yake ambayo ndiyo msingi wa 'muumbiko' wake na mustakbhari katika madhahirisho na wakati. Lakini ipo tofauti moja ya muktadha mzima wa kiasili kwa saikia ya viumbe hai vyote. Hiyo hubainisha mfanyiko wa Saikia za vingine vyote kubakiza mwanadamu kwa ardhini na wale Pomboo; pia jamii za Nyangumi katika bahari. Wanyama, miti, mimea, wadudu, vijidudu na samaki huwa na 'Saikia mmeguko' ambayo ni sehemu ya Saikia ya mama Dunia. Naam, Dunia ni kiumbe hai na tena chenye namna ya ufahamu wa namna yake. Mwanadamu ni mwenye sonafi katika Saikia yake inayotawala na kuendesha hadhi ya utu wa jinsi moja moja. Wanyama, miti, mimea, wadudu, vijidudu na samaki huwa na 'saikia ya kimakundi' na tena 'kutawaliwa' na sonafi ya Dunia. Pomboo na jamii za Nyangumi hutawaliwa na saikia kama ilivyo kwa mwanadamu lakini ndani ya muktadha wa saikia pana yenye kutawaliwa na sonafi ya kipekee yenye kudra zenye kulingana na nyota za mbali.

Mhimili wa maumbo yote na mwendelezo wake ni shani ijayo kwa mapaji ya sonafi ambayo ni karama na pia neema ya 'Roho wa Uzima'. Basi ni kwa jinsi hii roho ndiyo yenye kuchakachua mienendo yote na kuipa kadri ya hesabu, mawiano na hadhi pale ambapo 'miale' na 'mawimbi ya uzima' vichakatapo ili kuchukua sura dhahiri. Kama ilivyo karama katika nuru, ndivyo ilivyo kudra katika mbegu za maumbo na muktadha wa madhahiriko katika kote penye mawimbi ya uzima. Miale na Mawimbi ipo pote na kote na hivi 'Roho wa Uzima' ni yote na mote. Na hivi basi si Yai na wala Kuku chenye kumtegemea mwenzake hasa; vyote viwili vinafanyika kwa muktadha wa cha tatu kisichodhahirika katika ulimwengu wa sura. Kunabahi ulimwengu wa maumbo pekee yake ndiyo kwaweza kupotosha ukweli wa jambo na mambo ijapohali ndiyo msingi wa utambuzi wa mwanadamu katika hali ya kawaida. Na pia hata vipimo na tathmini vyaweza kuleta kadiri ya 'mapengo' katika ukadirifu wa mabadiliko kimaumbo kwa kuwa katika mifumo ya viumbe hai kuna fizikia ya kwa nje na nyingine ya kwa ndani. Ni hii ya kwa ndani ambapo kile cha Tatu hufanya mhimili wa kuchakata na fizikia ya nje kwa tabia, hadhi na mabadiliko ya kimaumbo.

Fizikia ya kwa ndani ndiyo hutenda 'miujiza' ya kadri ile ya baiyoholojia ya kikwantumu. 'Tatu' ya Yai ni kadri ya chochote chenye kugawanyika katika mazaliano ama mazidishano ya kiuhai. Kanuni itawalayo uwezekano huu haitegemei hesabu wala kiasi chochote katika muktadha wa madhahiriko ya mapana ya maumbo ya uhai wenyewe ila tu kufanya usikronizi kwa 'uhitaji' na 'uweza' katika nguvu ya kuifanya sura ya kiumbe na hivi pia basi kuistahimilisha mienendo yake ili 'kuhifadhi' sura za madhahiriko na kustawi kwake ndani ya mawimbi ya uzima wote. Mawimbi ya uzima ni bahari isiyokuwa na mwisho na hivi hata tatu ya kiumbe ni 'chembe ya mbegu la fikara' katika mapana ya mabahari isiyokuwa na mwisho kwa jinsi ya kimafikara. 'Roho wa Uzima' ni yote na mote, na hivi maumbo yalidhahirika na yale yasiyodhahirikia hushududia muktadha kwa 'Kweli' yenye kuhusu kinachopata kuwepo. Basi ndiyo kwamba japo kwa jinsi ya majira na 'msongo wa wakati' vitu hubadilika kuwa kimoja hata kingine, kwa ndani kabisa kweli ni ile ile moja katika madhahiriso yote; ni utatu wa 'Mpango Mzima'--Yaliyodhahirika, Yasiyodhahirika yote katika 'Roho wa Uzima'. Ndivyo hivi kuwa 'Roho wa Uzima' ni Mwanzo na Mwisho kwa lolote lenye kutanabahiwa katika utumikivu wa akili ya kawaida ya mwanadamu. Kwani na yeye mwanadamu ni sehemu ya mpango mzima japo ni rahisi pia yeye kudhania vinginevyo. Katikati ya Yai na Kuku ndipo kuna siri isiyo ni kuku wala yai—hapo ndipo 'Kweli' huwa. Palipo Yai, kweli hufutika hilo Yai, na palipo kuku kweli hufutika huyo kuku. Na hivi ni katika ile nukta tu ya katikati ya magawanyo kamili ya kimaumbo na majira yake kamili ndipo siri za 'mawimbi ya uzima' na 'mbegu ya sura' za maumbo yaweza kung'amuliwa--kama vile pia katikati ya kuvuta na kutoa pumzi ama kutoa na kuvuta pumzi. Kadri hii huleta 'usufuri' kwa hatima ya 'vina' vya mienendo yote na maumbo.

Kusingelikuwepo na saikia, huu uhalisia wa maumbo ya kiuhai usingelikuwepo pia. Kwa maana maumbo hayawezi kuwa na ile kadiri ya kudhahirika na kutodhahirika kwa mifanano ila tu kwa muktadha wenye kuhifadhi migando ya sura na mienendo ya kuundika maumbo. Saikia ndiyo yenye kufungamanisha mawezekano ya kimaumbo pamoja na ufahamu wenye nia kwa kiumbe katika muktadha wa misukumo ya kiuhai ya bila ya kufundishwa. Kwa mfano utumbo katika mwili wa mwanadamu, huo haujapata kufundishwa na mtu na wala mazingira yake yenyewe ili kusukuma na kusharabu virutisho vile vitokanavyo na chakula ili viingie katika mikondo vya damu itiririkayo kuzunguka mwili mzima kufaa hitaji la viungo vingine vya mwili—toka siku kwanza seli za mwanzo za utumbo hujua 'wimbo' wa shughuli yake pale wakati uwadiapo. Kila seli ya uhai ina 'ujuzi-mbegu' wa jinsi yake kabisa.

Viumbe vyenye kufanyika kwa jinsi ya mkusanyiko wa seli kama mimea na wanyama pia wadudu huwa ni muktadha wa 'seli moja' isiyodhahiri yenye kustahimilisha sehemu ya muktadha wa zile seli zenye kudhahirika. Huu muktadha hukamilika kwa daraja la Saikia ya kiumbe kwa kuwa hii yaweza kuooana na sehemu ya saikia ya seli na kufanya 'saikia jumuizi' kwa kiumbe kilichovivaa viumbe. Ndivyo hivi basi akili ni chombo chenye utumikivu kwa viumbe hai vyote na kila kiumbe chenye kufanyika kwa mkusanyiko wa seli kina akili--iwe ni mmea, mnyama, mdudu ama samaki... Japo muktadha wa akili yenyewe ni wa kipekee kwa kila kimojawapo. Akili ya viumbe haifanyiki kwa chembe yoyote iliyodhahiri ila tu ule muktadha wa maumbo usiodhahirika moja kwa moja katika ulimwengu dhahiri.

Saikia ya kiumbe ndiyo hufanyika kwa mapana ya 'kukamata' kumbukumbu ili kufaa utumikivu wa 'ujitambuo'. Katika wanyama, mimea na wadudu kuna jinsi zake tofauti za kumbukumbu na hiyari kwa yale yaliyoingia katika kumbukumbu iliyo ni sehemu ya akili--iliyo ni sehemu ya Saikia. Sehemu ya tabia za mimea kama vile kufikia kile kituo cha ukuwakujia wa kuwa na miba ili kujilinda kutafunwa na wanyama ni mazao ya saikia jumuizi ya aina ya mimea yenyewe. Mimea kuwasiliana kwa kutoa gesi na kuchochea mabadiliko kwa ladha ya majani yake ili kuzua twiga asitafune majani yake machanga ni sehemu ya maendeleo ya saikia ya namna hiyo ya mimea ya miti. Vivyo hivyo huwa kwa yale majani ya maua yenye kula wadudu ama yale yenye kunywea yaguswapo. Pia ndiyo basi kusema ni mchanganyiko wa kudra na ukuwakujia kwa mimea yenyewe kama vile miwaridi ipatayo kuota katika tabia nchi ya ukavu na kufanya miba karibu na vikonyo vyake katika kulinda maua yake yenye harufu nzuri na fahari ya kipekee.

Kumbukumbu hufaa kusindikiza mabadiliko ya kisura ; hali kile chenye kutumia hiyo hubaki na kule kujiona kikiendelea kudumu kama kiumbe hai kimoja kisichofanyika kwa jinsi ile ya seli ndogo ndogo zenye kutokea na kufa katika majira mapana ya kipindi cha uhai wake. Saikia ya mwanadamu ina akili yenye kuzaa tafsiri ya kujitambua kama ni kuwa mtu na hali kumbe 'utu' ni muakisiko wa mapana ya minyororo ya madhahirisho ya hata chembe ndogo ndogo sana za kimaumbo katika tu hii kumbukumbu; na huku pia hayo yote kukirimika kwa neema ya ile nuru ya ufahamu na muktadha wa ufananio kwa lile 'Ua la utu' lisilodhahirika ila tu kwa 'mafikara-mbegu' katika 'Roho wa Uzima' na kuchakata kwa 'Wakati'.

Pasipo utumikivu wa kumbukumbu kila tukio daima lingalikuwa ni jipya pasipo 'ushawishi' kwa lile lililolitangulia. Nia isingalikuwepo-- na hivi hata 'maana iliyofichika' isingalikuwepo pia kwa yote. Wakati pia usingalikuwa, maana yoyote na wala shauri la 'Roho wa Uzima'.

Kutambua uthabiti wa maumbo ni shauri lililoandama daima wafikirifu katika vizazi vya wanadamu. Hata kwa wale Wayunani kabla ya zile siku za Socrates kulikuwepo na mashauri mbalimbali kuhusu kufanyika kwa uumbaji wote.

Ndipo tunamtazama mtu aliyefahamika kwa jina la Anaximander; aliyepata kuwepo takribani kati ya mwaka 619 mpaka 540 KK—Aliyepitia shule ya mwalimu na Mkuu aliyemtangulia aitwaye Thales; na yeye Anaximander katika siku zake kuwahesabu Anaximenes na Pythagoras miongoni mwa wanafunzi wake. Huyu huchukulika ni mtu wa kwanza kutoka kwa jamii ya wayunani kupata kuandika mashauri mbalimbali kwa muktadha wa kisomo chake kuwa risala kwa kuielezea asili-- kwa watu wengine kunakili na kusambaza ifaavyo. Kipindi alichoishi kilikuwa ni kati ya kile kipindi cha mapinduzi makubwa ya kiakili na kiufahamu na hivi kuakisika katika minajlili ya tawala na ustawi wa watu kote duniani. Hii basi ni kadri ya kipindi cha miaka 2500 nyuma; na sifa za makundi ya watu, makabila na mataifa yalipitia minyambuliko ya sura kama vile ilivyokuwa bayana huko katika bara la Asia katika nchi za Bara la Uchina, Bara Hindi, Irani, Mashariki ya Karibu na Uyunani ya Kale.

Anaximander alikuwa ni mpendekezaji wa Sayansi—mtu mwenye kutafuta msingi kwa mashauri yenye kudadavua mienendo ya asili. Na hivi yeye alikuwa ni mtu mwenye kutizama na kujaribu kulielezea jambo ama mambo; na hasa nyanja mbali mbali za ulimwengu dhahiri. Kutaka kwake kujua asili ya ulimwengu kulisukumwa na udhanifu kwa imani yake ya kuwa kila kitu katika ulimwengu dhahiri husukumwa na sheria kwa utaratibu fulani—kama ilivyo katika nazo jamii, chochote chenye kwenda kinyume kwa kutibua mizania ipasayo uhalisia wake hicho hakitadumu. Na kama ilivyo kwa wafikirifu wengine wa siku zake, kiu yao katika kupata kuyajua mambo iliwasukuma katika nidhamu ya visomo vya aina mbalimbali—mambo kama yale ya elimu ya Anga na Nyota ilivyo ndiyo kusema ni Unajimu; pia juu ya maumbo. Ndipo hapa pia neno 'fizikia' pia limetokana na lugha yenyewe ya kiyunani kumaanisha 'ma/umbo' ya asili--physis.

Kutokea kwenye Ngano za visa vya Miungu kama vile simulizi la tawala za mpangilio wa manyota na asili yake—kusema ni kosmogoni; kama ilivyokuwa ikichukulika katika Hesiod na Pherecydes; Zeusialikuja kukita mpangilio wake kwa kuwasambaritishia mbali wale ma-Titani waliokuwa wakitishia hali ya utulivu na uenda sambamba wa maumbo na mienendo yake katika Mbingu--yaani utangamano wake. Anaximander alikuwa ni mwenye kusisitiza ya kuwa mipangilio na mienendo ya maumbo si yenye kutawaliwa na nguvu ya jinsi ya mamlaka moja yenye kuamua kila kitu; bali maumbo yote hasa yana muktadha wa kijeometria na hivi basi kuwa na vitovu na njia zake mbalimbali katika kuchukua kwake sura na kudhahirika. Basi ndiyo kuwa akapata kutia msisitizo matukio yote ya nguvu za asili kama vile radi, pepo na mvua--vyaweza kuelezwa ama kutathminiwa kwa muktadha wa nguvu za asili iliyofanyika katika ulimwengu wa mazingira yake yenyewe pasipo na kutaliwa na 'miungu' kama ngano za zamani za wayunani zilivyoshuhudia picha ya maumbo, ulimwengu, mienendo na asili.

Vitovu na njia vinaweza kusakwa ili kudadavuliwa kimashauri kwa kile kitendo cha kujaribu kuitathmini mienendo na kanuni zake. Ndiyo basi husemwa pia Anaximander ni kati ya wanasayansi wa mwanzo kabisa walioamini muktadha wa vitendo ili kukamilisha uchunguzi na tena ndiyo kufanya kisomo juu ya jambo. Na yeye kupata kufanya hivyo na kuandika kumbukumbu la majaribio yake ambayo mengi hata hivyo yalipotea-- na hata katika zile siku za Plato na Aristotle karibia mashauri yake mengi yalikuwa yamekwisha sahaulika.

Ni katika muktadha wa jeometria ndipo basi Anaximander alidhanifu dunia kuwa ni kitovu kwa maumbo yote ya mbinguni na hivyo miili yote yenye kuonekana juu huzunguka dunia. Picha kamili kwa 'ukweli' ilikuwa ngumu kwake na hivi yeye aliishia katika kudhani dunia ni kama kopo la mviringo lenye uso wa juu wenye kufanywa na bahari na mabara ya watu halafu kimo chake ni theluthi ya kipenyo chake; miili yote huzunguka kwa chini ya kopo hili. Makadirio haya yalifanyika kukidhi kudadavua asili ya misimu na maonekano ya miili kama vile jua na mwezi. Basi muundo huu kuogelea katika mapana yasiyokuwa na kikomo na halafu ndiyo basi kutojishikiza kokote.

Katika kulitilia mkazo uhai wa mienendo ndivyo hivi Anaximander alijaribu kueleza asili na mwanzo wa yote kama mwenzake aliyemtangulia huku wote wakijitahidi kujinasua na mapokeo ya kingano. Hata hivyo yeye akijaribu kufuatisha maadhi ya viini vya mashauri yaliyotangulia. Ndimo hapa basi ile dhahania kwa dhana ya 'Aperioni' na Arkh ilivyokuja na kusababisha muktadha wa mashauri ya Anaximander.

Kwa kuwa mwalimu aliyekuwa akimtangulia, Thales, alikuwa ni mwenye kusema ulimwengu unaelea katika bahari ya maji isiyokuwa na kikomo basi yeye Anaximander akadhanifu ile dhana ya 'Apeironi' isiyokuwa na kikomo--akijibandua kutoka katika udhanifu wa maji kuwa ni asili ya kila kitu kilichokuja kuumbika na pia kuongeza dhahania ya 'Arkh' ili kuja kufafanua asili ya maumbo yote.

Ilikuwa ni nia yake kufungamanisha Aperioni na 'Arkh' ili kusudi Aperioni ionekane ni kama kitu-tobo kilicho ni kitovu kisicho tathminika ukatikati pake, basi hivyo kufananishwa na kina; na hali pia Aperioni yenyewe ni kubwa pasipo kikomo—kitu kama 'mwayo' wa uumbaji wote. Kuwa kwake Aperioni katika Arkh basi ni kufanya yote mawili kuwa ni moja la umilele na kadri isiyo na umri. Kusema hivi ndiyo kule kwenye kwenda sanjari na mashauri ya 'usivyokufa' na 'umuda' wa kile kisicho na kikomo.

Aperioni ni mhimili ambao arkh hutiririka kukirimu sura za maumbo na mienendo na hali ikikamilisha ile dhana ya kila kitu kilichofanyika hurudi katika jinsi yake ya kabla. Kilichofanyika kwa jinsi ya Udongo kurudi kuwa ni udongo tena. Basi kama vile waliomtanguliwa walivyopata kuzungumza maumbo kufanyika kwa 'elementi' nne za msingi zilizo na ardhi, maji, hewa na moto-- kosmogoni zote zilianza na kule kujaribu kutambua ni elementi ipi hasa ndiyo ilikuwa ya mwanzo. Thales alikuwa ni mwenye kusema maji; na Anaximander alikuwa ni mwenye kuzungumzia Arkh na Aperioni.

Mwanafunzi wa Anaximander aliyeitwa Anaximenes alikuja kuondoa 'ufumbo' wa Arkh kwa kusisitiza tabia tupu za zile elementi nne kwa kupita kwa wakati, hutosha kueleza mabadiliko ya sura na maumbo ya vitu vyote.

Ili kufanya sifa za kosmogni kuendana na maumbo yalivyofanyika na tena kutokana na zile asili za elementi; mashauri yaliyofuatia yaliegama katika tabia za elementi zenyewe kama kusema tabia zile za ubichi, ukavu, wepesi wa kushika moto na kupoa. Ndiyo hivi Anaximenes alikuja kupinga dhana ya huo mwanzo wenye kuanzia na maji na yeye kudai ni Hewa ndiyo iliyoanza... Kwa kuwa kutoka katika maji huwezi kupata moto kama lifanyikavyo jua; basi hewa yaweza kukidhi kueleza moto na vinginevyo katika huo mwanzo. Na yeye Anaximenes basi kuwa ni mtu wa awali aliyetumia ukaguzi wa mabadiliko ya hali na maumbo kama msingi wa kufafanua kweli za kimaumbo yenyewe katika kupita kwa muda—kama vile kuzungumza, mfano, maji kuwa kana kwamba ni matokeo ya mvuke--kusema ni hewa; uliokuja kupoa kutoka kwenye ile 'hali ya joto' kuja kwenye 'hali ya ubaridi'.

Ni Aristotle aliyekuja kufufua sehemu ya muktadha wa jitahada za Anaximander kwa kujitahadi kukadirisha picha za kimashauri yake na ule mwongozo kwa kukifanya kisomo chenye kuchambua maumbo na tabia za asili kwa msingi wa mtazamo wa kiuchunguzi-- kwa yale madogo madogo yenye kuja kuzaa mapana ya kisomo cha jinsi yake. Ili kukidhi haja yake ndiyo yeye akaleta shauri la 'sabustratamu' yaani 'maada ya msingi' kupunguza 'ufumbo' wa kile cha awali kilichopata kuitwa ni Arkh.

Aristotle alikuja kurasimisha neno 'Arche' kutoka katika neno 'Arkh' lenye kumaanisha mwanzo wa kitu—kule kitokako hicho kwa asili yake. Kulingana na kosmogoni ya kiyunani iliyotajwa kuja na simulizi laHesiod kutoka siku za kale za wayunani, na ndiyo ilifahamika kwa Anaximander na yeye Aristotle;arche ya yote ni 'mvurugiko'--'usosura' usio na kikomo. Ulitajwa huo na Hesiod kama 'mvurugiko manani' wa kimsingi kabisa ambao kutokana nao kila kitu kilikuja kutokeza kuwa na 'usura'. Hii ilielezwa kama tundu kubwa lisilo na mwisho—'mwayo shimo' ambako ni kwenye mizizi ya Dunia, Anga, Bahari na 'Tartarusi'. Katika kosmogoni ya ki-'Orfeusi' husimulika juu ya yule Kronosi asiyezeeka—kuwa alifanyiza 'Aither'--Aitha pamoja na 'Mvurugiko' na basi kulifanya Yai la rangi ya fedha kwa Aitha manani—ambalo kutokana nalo kila kitu kilikuja kutokea.

Na Aristotle ndiye alikuja kupendekeza vitu vyote ni jinsi moja ya kimaada ambayo katika mchanganyiko wake na 'hali' tofauti tofauti ndiyo huja kuzaa kadiri ya Ardhi, Maji, Hewa na Moto. Kama vile kusema: 'maada msingi' + joto joto + ukavu = moto, 'maada msingi' + 'joto joto' + ubichi ubichi = Hewa, 'maada msingi' + baridi + ubichi ubichi = Maji, 'maada msingi' + baridi + ukavu = Ardhi.

Japo Aristotle alikuwa ni mwenye kuvutia sana kwa ufundi wake wa kisomo chenye mantiki na kujaribu 'kuyalaza' mashauri yote katika mizania za kimantiki, yeye alikuwa akigusia tu mashauri yale juu ya mambo yasiyo dhahiri--'kutojisumbua' kudadavua mashauri ya hayo kwa mapana ama kina ; vile basi kama alivyopata kugusia udhanifu wake wa kuwa mbingu imepata kufanywa kwa 'elementi ya Tano'. Ile elementi ambayo Plato alipata kufundisha uwepo wake na yeye Aristotle kudokeza hivyo katika kazi yake ya 'Juu ya Mbingu'--Kuhusu kuumbika kwa Mbingu.

Katika siku za akina Aristotle na Plato kuna uwezekano wa mashauri yao mengi kuwa ni yenye kufanyika kutokana na ushawishi wa chini chini toka kwa majirani zao wa Kihindi na Waajemi; kulingana na yale yaliyokuwa yakizungumzwa na kuaminika na mapokeo ya hao.

Kutoka Bara Hindi kulipata kuwepo mapokeo ya kiveda. Kumbukumbu na rejea za kileo zinakadirisha Veda, kama makusanyiko ya tungo za maelezo kwa mambo ya kiroho, ilichipuka kati ya miaka 1500 hadi 500 KK; japo asili ya veda kiukweli yaweza kuwa zamani sana hata kupita hapo. 'Veda' inatafsiri ya 'Maarifa' na hasa yaliyotokana na ma-Rishi wa zamani katika Bara Hindi. Katika nyakati za zamani palipata kutokea wimbi la watu 'waliochanua' kiroho kama mchipuo wa uyoga mwingi juu ya ardhi katika Bara Hindi; mchanuo huu ulio ni epifani ama pia kusema ufunuo mananifu--ni kitendo cha mtu kufunguka kiroho na kuzama katika raha ya kuogelea katika 'mwili' mkuu wa uzima wa maumbo na nyenendo zote. Nyakati fulani zinazoshuhudiwa kupata kuwepo, wapo watu waliopata kuwa na epifanina kutokana yale yaliyowatokea na kufanyika bayana katika akili zao walijaribu kuwasilisha picha na maelezo ya yale yaliyowezekana--kuwasilisha mfananio wake kusudi wale ambao hawajapata ule ufunuo wapate kubaki na masimulizi ya kimwongozo. Wao waliongea katika lugha fulani yenye kushahibiana maneno fulani kama vile ule msisitizo wenye kujirudia sana juu ya 'Hiki' na 'Kile' katika kueleza uhusiano wa maumbo dhahiri machoni na ile 'Kweli' ya Uzima wake isiyoonekana kwa macho wala kusikika kwa masikio; vile vile hata mioyo ya watu haijapata 'kuonja' ladha ya utamu wa hisia zake juu ya yote. Lugha yao pia ilikuwa ni mchanyiko wa utenzi na ushairi kwa kuwa wao walikuwa ni watu wenye ufunuo wenye raha sana katika kuzama ndani ya 'kweli'.

Watu hao, ndiyo kusema marishi; japo walikuwa ni mtu mmoja mmoja na tena kila mtu kivyake vyake, baadhi ya yale waliyoyashuhudia kwa kuyaeleza kuhusu ulimwengu wa kiroho ilidhahirika kwa watu wa kipindi kile kushahibiana na kuonekana kama ni wenye kuzungumza lugha moja yenye uashirifu wa jambo kuu. Basi sehemu ya yale waliyokuwa wakiyatamka ama kuwakilisha kwa watu yalikuja kutunga mwili wa veda; mapokeo yalianza kwa mdomo na mbinu za kiuhifadhi ulio ni ukaririfu kiakili; na halafu kadri yalivyokutana na mwanzo wa kisomo cha maandishi, yakaja kunakiliwa na kutajwa miongoni mwa waandishi na wanakisomo kama 'samhita'--makusanyo ya tungo na semi kutoka kwa wale waliopata kujua na kuishuhudia 'Kweli'. Pia mwongozo kwa wasiofahamu ili wapate kufahamu mambo makuu kuhusu ulimwengu na neema istawishayo watu na kuleta taratibu za kiutamaduni na zaidi ili kuwa hao wenye kupokea hayo waweze kufuatisha maarifa yenye kupelekea jamii kwenye mwangaza na kheri.

Lugha iliyotawala katika siku za Marishi ni lugha ya kisanskriti; na ndiyo lugha ambayo kisomo cha siku zile kilijisheheneza umashuhuri wake kimatumizi. Na pia ndiyo lugha iliyopata kuwa na ushawishi na tena mama hata kwa lugha nyingi za leo za Ulaya na Asia—kama ilivyo leo kwa lugha ya kiingereza kutawala visomo na matanuko yake kwa nguvu ya ushawishi; kilatini pia kimewahi pia kuwa ni lugha ya visomo miongoni mwa wanavisomo... Lakini kisanskriti kilipata kuwa na mfano kama huu hapo siku za zamani sana. Na ndiyo hivi hata kuna maneno mengi ya kiingereza, yananyoosha mkondo wake hado kwenye asili ya maneno ya kisanskriti. Vivyo hivyo kwa lugha nyingi za ulaya kiasi kwamba inaleta udhanio wa kuwa sehemu kubwa ya watu wa makabila ya ulaya huwenda wamewahi kupata kuwa sehemu ya Bara Hindi au ndiyo kusema wana asili ya kupata kuchangamana wa watu kutoka huko ama hata kutokea huko.

Kwa asili mapokeo ya kiveda yanaangukia katika namna ya makundi manne makubwa yaliyo ni mikusanyo ya 1. Rigveda, 2. Yarjuveda, 3. Samaveda na 4. Atharvaveda. Haya yote hufanya sehemu muhimu wa ustawi na ustaarabu wa Kihindu. Yalijitokesha na kushamiri tangu miaka maelfu kabla ya kuzaliwa kwa Yesu aiitwaye pia kristu kule mashariki ya kati. Hapo awali kabisa mwili wa mapokeo ya kiveda ulihifadhika kwa mafunzo ya kukariri na kughani katika mitindo maalum yenye kuweza kuhakiki uhifadhiko wa tenzi na habari zibebazwo. Na hayo makundi manne tofauti yalikuwa yakiendana na taratibu maalum za kuhusisha utumiko wa utenzi wa kiveda. Toka siku za zamani, Veda husemwa ni zao lililotokana na kazi isiyo ya mwanadamu peke yake yaani apauruseya; miongoni mwa Wahindu. Husemwa ya kuwa Veda ilikuja kwa 'kusikika' ndani ya watu walioipokea na kutamka kwa maneno kusudi na wengine wapate kufaidika; hili hutajwa kama ni sruti(kisanskriti, pia 'shruti')—'kilichosikika' miongoni mwa Wahindu. Kipindi cha baadaye kazi hizo za mapokeo zilipoanza kunakiliwa katika mtindo wa maandishi ndipo hizo kazi zikaitwa smriti--'Kilichokumbukwa'. Na hivyo jamii ya Wahindu walihusisha Veda na matendo yao makuu ya kiimani, ustawi na ustaarabu.

Rigveda, inayokubalika kutangulia makundi mengine yote ya makusanyo ya kiveda; hukadiriwa kuchipua miaka ya takribani 1500 KK. Hii ni ya kwanza kwa msingi wa 'utatu wa sayansi' iliyofanyika takatifu kwa Wahindu—trayi vidya; na hivi Rigveda ilikuwa ni mapokeo kwa makuhani wa juu wa Kihindu kwa ajili ya mwongozo wa utaratibu mzima wa ibada za Kihindu. Ndani ya tenzi zake kulikuwa na mantra zenye vina maalum vya kitenzi kwa ajili ay kughaniwa kwa sauti katika kusifu 'Brahma'--roho kuu ya uumbaji wote katika sura ya unafsi. Yarjuveda ni mkusanyiko wa tenzi zilizo/zinazoghaniwa kwa sauti ya chini chini katika shughuli za kufanya sadaka za matoleo kwa Brahma. Samaveda hubeba ndani yake tenzi zilizo ni mapambio yenye kuimbwa katika sherehe za ibada kwa Brahma.

Atharvaveda ilikuwa ni mkusanyiko wa mawaidha yenye sura ya tenzi zenye vina na mizani ama vinginevyo kawaida yenye kukazia maana kwa namna za makundi mengine ya Kiveda. Pia ndani yake kulikuwa kunamafunzo ya siri yenye kuweza kuleta uwezo wa kiganga, uwezo wa kuponya maradhi na hata kudhuru wengine walio ni maadui kiakili ama hata kusababisha madhara katika mazingira yenye kuweza kukusudiwa. Na hivi Atharvaveda hubakia ni mapokeo yenye kukanganya maana yake hasa kwa kuwa umuhimu wake kuchukua sura tofauti kwa watu tofauti. Mengine yapatikanayo katika Atharvaveda kuchukuliwa kuwa ni ya zamani labda hata kutangulia Rigveda ama tuseme yalianza sambamba na kujitokeza kwa Rigveda. Na kwa sehemu kubwa ni ujuzi wa kunuia mambo, kughani maneno yenye nguvu za kimazingara, kukinga mtu dhidi ya mapepo, kufukuza maradhi, kuapiza madhara, kufanikishia matakwa ya kimatamanio, kujitakia maisha marefu n.k.

Upande wa kiufundi wa maarifa ya kiveda, ufahamikayo kama Upaveda, ndiyo umeleta ufundi na ujuzi kwa mambo kama vile sayansi ya utabibu ifahamikayo kama Ayurveda. Hii imetokana na Rigveda japo imetanabahika kuingilia na Atharvaveda nyakati zingine. Kutokana na Yarjuveda kulikuja kuwa naDhanurveda—sanaa ya kutumia silaha za Upinde wa mshale. Kutokana na Samaveda kulikuja kuwa na uchezaji muziki uliotambulika ni mtakatifu—Gandharvaveda. Kutokana na Atharvaveda kulikuja kuwa na Shastrashastra.

Ni muhimu kutazama kisomo cha Veda ili kuelewa chimbuko la mambo kama Sthapatyaveda—ubunifu wa sura za majengo, kama ilivyotumika kwa mahekalu na nyumba za kuishi kwa wale waliomudu kuunda; Shilpa—sanaa za mikono ambavyo huwekwa katika Upaveda kwa Atharvaveda. Hayo yote hufanya Veda nne mashuhuri tokea siku za zamani na mapokeo mengine kama Mahabarata,Natyasastra na Puruna kadhaa kupewa jina la pamoja kama Veda za Tano. Na hapo hapo mapokeo kama Bhagavad Gita – 'Wimbo wa aliyebarikika' (Mkasa wa shujaa wa mapambano Arjuna na Krishna Mkuu katika kuiyaingia mapambano ya kivita ya mahala palipoitwa Kuruksetra; palipokuwa ni mahala pa kuhiji pia—Dhamaksetrah) na Vedanta—ukomofu wa veda kwa utimilifu wa kupokea mashauri kutoka kwa wale wenye kuhuisha maana yake kutokana na kutaamulika kwao--Kwa wengine miongoni mwa waumini wa Kihindu pia huchukulika ni sehemu ya Veda kwa nyakati zote.

Lakini kubwa katika kudadavua mapokeo ya veda ni kutambua umashauri wake ambao hapana shaka ulikuja kuathiri hadhi ya sifa na tabia kwa uwezekano wa mapokeo mengine yenye kuja kutokea na kuweza kuunda hata hadhi ya 'dini' ndani na nje ya mipaka ya India. Jinsi yake ya uandishi na ushairi, uhifadhi wake, maudhui na visa vyake vimedondolewa ama kujitokeza tena katika mapokeo na muundo wa dini zingine hata magharibi ya India, naam, Arabuni na mashariki ya kati. Kuna wakati veda ilikuwa ndiyo kisomo chenye umashuhuri mkuu katika nyanja za usomi na uanazuoni ambapo wale wenye kujihusisha na visomo vyake walionekana ni mastadi na watu wa upeo—watu wa vitabu. Kulikuwa na watu wengi tu waliopata kujitokeza kaandika mawaidha ya kina juu ya veda katika kudhihirisha umahiri ama upeo katika kutambua mashauri yajayo na mapokeo ya veda.

Labda ni India tu ambapo utamaduni wa mapokeo ya 'kinadharia' daima yamechuana sambamba na mapokeo ya moja kwa moja ya kutoka kwa wale walioitambua na kuiishi kweli wakati hata wakati. Ni katika hili ndio Vedanta ilikuja kujitokeza kama ukamilisho wa veda kulingana na jitihada za wale waliobaini kweli fulani na toka kwenye ile kweli kujaribu kuzungumzia veda kwa sura bora na yenye msingi imara siyo mapokeo tu ya mdomo ama maandishi. Pia ndiyo kuendeleza utamaduni waUpanishad... Yale ambayo watu walijifunza miguuni pa waliotaamulika ama kufunguka kiakili. Ndiyo hivi waliopata kutokea kwenye hata jamii za Kihindu kama Gautama Buddha aliyefahamika awali kama Siddhartha Mshakya; waliweza kufundisha mafundisho mapya yaliyotegemeana na kufunguka kwa fahamu zao na ufahamu wa yote. Tokea kwake yalikuja mapokeo ya U-Buddha yaliyojikita katika mtindo wenye kufahamika toka siku zake kama njia ya Buddha—dhammapada. Hii ni kuweka alama juu ya tofauti ya mapokeo ya kifikra yanayoridhiwa kama habari tupu; kuyatofautisha na yale mapokeo yanayolenga kumletea mtu mwongozo katika njia ya mabadiliko halisi ili kweli aishuhudiayo mtu kuwa ni moja na kweli aliyofanyikia upya mtu mwenyewe. Si Buddha pekee yake aliyefundisha mafunzo ya mabadiliko ya moja kwa moja ya kiutu; wapo wengine wengi walifanya hivyo hivyo kwa namna zao za kipekee na huku wengine wakikumbukwa na wengine kuwa kana wameshahaulika. Wapo walimu na wanasayansi wa zamani kama yule mwalimu mkuu wa Yoga Hatha, Patanjali, aliyefundisha mbinu za mikao, utulivu na ukimya wa kiakili na kimwili vinavyoweza kuleta utangamano wenye kutaamulisha akili ya mtu hata kuinukia na kufika katika ufahamu wa 'Kweli' na 'Nguvu' iliyofanyikia ulimwengu wote... Yupo Krishna aliyefundisha Yoga Bhakti—Yoga ya wanaojitoa moyo wote kwa Kweli ya Krishna iliyo ni Kweli ya ulimwengu wote mzima katika fahari yake iliyofichika mbele za macho ya watu waliokosa mwongozo ili kuona; na hivi kupitia Yoga Bhakti wanaweza kufunguka na kuwa moja na hiyo... Japo mafundisho ya Buddha ndiyo yamekuja kutawala sehemu mbali mbali za India na nje ya mipaka yake na huku yakionekana kuchepuka kutoka kwenye mapokeo ya awali ya kihindu na utamaduni mzima wa kiveda. Na haya pia kuwa mahususi kwa wale wenye kupenda na kutaka kuongoka hadi katika 'Kweli' iliyo ni muktadha wa Ufahamu mkuu wa Hekima na Huruma juu ya masumbuko ya mwanadamu katika zama zote anazoishi na ujinga wa kutotambua asili ya 'Buddha' ndani yao wenyewe...

Haya yote ni mwaliko wa kuingia katika kutambua kuwa daima kumekuwa na misimamo ya aina mbili katika kushika nia juu ya mtu kufuata mkondo wa 'mafundisho' matupu ama mafundisho yaliyo ni taa yenye kumuongoza mtu katika hata ile kweli itakayommeza yeye mzima mzima na kumwezesha yeye kuzaliwa mara ya pili katika 'Kweli'. Ni sehemu ya hili la pili ambapo Plato na baadhi ya wanafilosofia wakiyunani walikuwa wakilitambua lakini walijua hakuna 'lugha' hasa ya kueleza ufasaha wa yote yanayodhahirika. Ilikuwa ni jitihada yao kujaribu kudadavua mashauri ya watu na ustaarabu wao katika kuingiliana na lile 'lisiloelezeka'. Kwa hilo ambalo halielezeki wao walijaribu kutambua kanuni na taratibu zinazoongoza yote yafanyikayo; japo wapo ambao walianza kutotea kwa ujumla katika mashauri ya kueleza 'siri' za ulimwengu wa maumbo na 'asili' yake. Ndivyo falsafa ilivyozaliwa japo hata kwa wayunani si kuwa ndiko pekee jitihada kama hizo zimepata kufanyika... Kutoka Bara Hindi kumepata kuwa na jitihada kama za wayunani hata kipindi kirefu kabla ya siku za akina Plato na Aristotle.

Tutaendelea kuchambua mengine katika kisomo rasmi cha utatu na wawezekano ya kuupangilia upya ustawi na tamaduni za watu ili kuendana na visomo vya leo na mawezekano ya neema zaidi.
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…