Mtego wa Noti
JF-Expert Member
- Nov 27, 2010
- 2,591
- 1,599
Umeongea vizuri sana Kanigini, tatizo wanaume wengi tunaogopa kwenda kupima na badala yake tunawatanguliza wake zetu ndio wakapime ili watuletee majibu. Yaani akina mama huwa nawavulia kofia maana akiwa mjamzito tu apende asipende lazima apimwe HIV. Nakumbuka Morogoro sehemu moja vijijini huko kuna kijiji wana sera yao kuwa mama mjamzito lazima aende na mme wake kupima. Sasa kuna jamaa mmoja mke wake alikuwa mjamzito, mke alienda kupima ila jamaa aligoma kwenda kupima mpaka akawa anajificha maporini. Baada ya kuona vile ilibidi mtendaji wa kijiji atume mgambo wakamkamate na kumpeleka kituo cha afya kupima akiwa na mkewe! lengo likiwa ni kulinda mtoto aliyeko tumboni. Hii ni balaa kwa kweli! sasa sikuuliza kama alifanyiwa Counselling baada ya kupelekwa na mgambo kituo cha afya!
Kikawaida mwanaume unatakiwa uwe wa kwanza kwenda kupima kabla wife hajaenda, ukikuta ndivyo sivyo unafanya kumwandaa mapema.
Ila kiukweli ukimwi unatisha, inabidi upate counseling ya kueleweka si mchezo.
All in all, Ukimwi wa siku hizi hauui kama zamani, ukijikubali ziko njia za kueleweka za kuishi nao.