Wewe ni wa thamani mno

Matanga

JF-Expert Member
Joined
Nov 13, 2019
Posts
2,281
Reaction score
3,988
ULICHONACHO KINA THAMANI KUBWA SANA

Wenye Chakula hawana appetite (hamu ya kula) na wenye appetite hawana chakula. Wenye majumba ya kifahari wanakosa usingizi, na wenye usingizi wa kutosha hawana hata pakulala. Wagonjwa mahututi wanaomba uzima, wazima wa afya wanajiua. Wagumba wanalilia watoto, wasio wagumba wanatoa mimba na kutupa watoto chooni. Wenye mialiko mingi hawana nafasi ya kwenda na wenye nafasi hawana mialiko.

Wasio na kope wamejikubali kama walivyo, wenye kope wanavaa za bandia. Anayepewa upendo hauthamini asiyependwa analilia upendo.

Wenye amani wanaomba vita na kutishia machafuko, wenye vita wanalilia amani.

Mwenye nafasi ya kusoma na ada analipiwa hataki shule wala haitilii maanani, mwenye kiu ya kusoma hana ada.

Ni kama binadamu hajui anachokitaka hivyo hata akipata alichodhani anataka bado haridhiki kwani sicho hicho anachotafuta.

CHA KUSHANGAZA

1. Hicho unachokidharau Leo ndicho kilikuwa kinakuliza jana na kukunyima usingizi.

2. Hayo unayotafuta Leo pia kesho hayatakuwa na mashiko kwako.

MAISHA NI FUMBO LILILOSHEHENI VIFUMBO
KAMA MFALME SULEIMAN ALIVYOSEMA " TUNAFUKUZA UPEPO" ambao hatutakaa tuukamate!!

SHUKURU KWA UHAI. VINGINE VYOTE VINATHAMANI USIPOKUWA NAVYO, UKIVIPATA THAMANI YAKE INAISHIA HAPO. HIVYO USIRUHUSU VIKAKUTAWALA,UKIZINGATIA HIVYO UTAISHI KWA AMANI BILA KUUTESA MOYO WAKO.
 
Bonge la uzi ,ubarikiwe mkuu mwenye ufahamu atajifunza kitu hapa .Kweli Dunia huwezi ukashindana nayo ukaiweza hicho kidogo unachopata mshukuru Allah .
 
Unajifariji tu mkuu!!!Maisha ni mateso fulani hv yaliyobuniwa na mbunifu mwenye akili sana alietuzidi upeo!ndio maana hayana maana,hayafurahishi na yana katisha tamaa sana na hayana utoshelevu!!Ndio mana motivational speakers na psychologist wanajitahidi kutulisha upepo lakini wapi!!!!???
 
Ni kweli kabisa, tatizo binadamu wa siku hizi ni wabishi sana...
 
Kweli maisha hayapo fair hii mwanangu imemtokea yeye ni inocent man na anaozea segerea
 
Hayo machache yanatosha kutuonesha au kutujuza kuwa duniani sio makazi yetu ya kudumu bali tunapita, Yote hayo yatumika kutukumbusha kuwa tuna mahali pengine panapotustahili sisi wanadamu ili turidhike kabisa mioyo yetu... Hivi vyote tuvionavyo hapa duniani ni vichache mno kulinganisha na vilivyopo mbinguni alipo Mungu wetu... Uzuri Ni kwamba roho inajua hilo ndio maana Ni ngumu mwili kuiridhisha roho, Roho zetu zinafahamu kuwa mbinguni Kuna zaidi ya hivi vya duniani ndo maana kwa hapa duniani ukitaka hichi alafu ukakipata bado utatamani kingine, Hii inaonesha kuwa roho zetu kuna kitu inachokihitaji na inajua kuwa kipo na kipo mahali fulani.... Tumgeukie Mungu wetu aliye tuumba maana yeye ndo anajua kuiondoa kiu yetu na kutufanya tufurahi milele na kuridhika.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…