Habari zenu wanajamvi.
Me ni kijana wa kiume,bado sijaoa. Huwa najiuliza sana,nitatumia vigezo gani ili kumjua kuwa mwenza huyu atanifaa...nini cha kuzingatia kwa umakini ili kuwa na ndoa yenye amani,upendo na furaha?
Karibuni wenye uzoefu ktk ndoa zenu mtupe siri ya mafanikio yenu!
Kunahizi herufi sita za mwanzo jatika alfabetiko oda, A, B, C, D, E na F
A = age, msitofautiane sana kwenye umri, tofauti ikiwa kubwa kuna tencency ya mmoja kujiona kama mzazi wa mwingine hivyo kumtriti mwenzie kama mwanae vile.
B = body structure. Hii ipo phisical zaidi. Jaribu kumfuta mwenye umbo unalopendelea naye awe anapenda umbo lako. Ingawa lazima ukubali kuwa maumbo huwa yanabadilika. Unaweza ukaowa kipetitit leo, lakini ukikipiga na misosi kinabongeka ghafra.
C = character zipoje? Hapa wengi huzificha. Lakini unaweza ukajuwa haiba yake kupitia mavazi, aina ya marafiki alionao, maeneo anayoyapenda, aina vyakula anavyopenda etc... Kwa mfano kila siku yeye ni kudai baga, kesho piza, keshokutwa hiki au kile cha hadhi hiyo. Mtu huyu unaweza ukapredict maisha anayoyapendelea .
D = displine. Displine ya mtu utaijua kwa namna ya maongezi au majibu yake kwenye maswali toka kwa wengine.
E = education background. Wenye elimu ndogo huwa wanatendensi ya kuamini kuwa mwenye elimu kubwa ndo anajuwa kila kitu na hivyo atakuachia kila kitu uamuwe wewe ndani ya nyumba. Huwa hawana ushauri hata kama anao atahofia elimu yake. Jitahidi muwe na elimu sawa au isiyopishana sana.
F = famili background. Wazee wa zamani walikuwa wanaangalia zaidi kama upande wa pili kuna magonjwa ya kurithi au la. Kwa mfano pumu, kifafa n.k.
Kuna familia ukiowa, juwa watahamia wote kwako. Na hasa kama una kauwezo kuliko wote katika familia uliyoowa. Jua mapema hilo na kama utakuwa tayari kwa hili we endelea, lakini usije ukabadirika baadaye kwani huwa yanaleta shida sana haya mambo ya kuowa mmoja halafu unahudumia wote.
Madewa, kazi ni kwako...