Wenye continental decoder, matangazo yamerudi?

fred tarimo

Member
Joined
Oct 3, 2011
Posts
10
Reaction score
5
Kwa wadau wanaotumia continental decoder, naomba mwenye ufaham kama imerudisha urushaji wa matangazo
au kama kuna namna ya kufanya ili kurudisha..

===========


Taarifa mpya
Habari wanaJamii,

Continental kwa sasa wanarusha matangazo yao kutumia Satelaiti ya ABS 3A frequence 11150, Symbole rate 45000, Polarization vertical, direction 3 degree west.
 
Bwanae bado mpaka sasa....hawa continental nawaona kama wazushi tu maana ni zaidi ya wk 2 leo. sijui km kuna namna ya kufanya zaidi ya kusubiri km yupo anayejua atusaidie.
 
aisee. mm nilijua dish limeyumba, nmemuita fundi wao kila siku ananipiga saundi, kumbe kuna tatizo hukohuko kwao. hawa jamaa hawako serious
 
Ni majanga mkubwa, mi nawaza kuling'oa very soon..
 
Azam wako vizuri kuliko zuku, kwasababu azam wanarusha local chanel bure hata ucpolipia, tofauti na zuku kifurushi chako kikiisha hupati chanel yeyote bure labda zile za fta.
 
watarudi hewani kwa satellite nyingine na itakuwa Siyo bure tena
 
Kuna mdau jana alitutaarifu humu tayari washarudi ila wako satellite tofauti...
 
Sio continental pekee, hata TING wiki ya pili sasa hawajafanikiwa kurudisha matangazo
 
kama wako satellite nyingine kwa nn hawatoi tangazo namna ya kuwapata? hizi ndiyo adhabu za digital kwa watu analogue.

continental km mko humu semeni cha kufanya.....mwezi sasa kimya..shame on you.
 
" wapigieee....ni nzuriiiiiiii!! (katika sauti ya sharobaro wa kihaya)
 
Spacecom loses contact with Amos-5 satellite

Soma hapa ujue kwanini Continental na TING hawapo hewani, kwa kuwa kampuni ya Kiisraeli ya Spacecom imepoteza mawasiliano na Satellite ya Amos 5 ambayo ndiyo ilikuwa ikirusha matangazo ya TING na Continental. Tusubiri wahamie Satellite nyingine.
 
Hawa wapumbavu kweli mpaka sasa wamekaa kimya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…