Waziri wa ofisi ya Rais na Utawala Bora ongea na Maafisa Utumishi na Waziri wa Elimu, HESLB inatutesa watumishi wa Umma

Retina

JF-Expert Member
Mar 6, 2015
1,038
1,154
Kumekuwa na Uzi mbalimbali humu JF zinazoonesha malalamiko mbalimbali ya jinsi bodi ya mikopo Elimu ya juu (HESLB) Kwa kushirikiana na maafisa utumishi kuingiza makato kwenye mishahara ya watumishi wa umma hata ambao hawajawahi kukopeshwa na HESLB ama wengine kumalizana na bodi miaka kadhaa iliyopita kupewa barua kama uthibitisho lakini HESLB imekuwa ikirudisha makato kimakosa na kuleta usumbufu mkubwa katika kufuatilia marekebisho yake.

Ukifika ofisini kwao kudai chako wanakuambia refund inajazwa online, ukijaza hata usitarajie kuipata kwa wakati kwangu mwezi wa pili sasa,hata online feedback haioneshi kama wanafuatilia, ukipiga simu hawapokei yaan ni kero juu ya kero.

Makato haya yanaingizwa kimakosa na maafisa utumishi Kwa kushirikiana na maafisa wa HESLB cha kujiuliza, kwanini hawa maafisa utumishi hawafanyi mawasiliano na wafanyakazi hali wana taarifa zote za watumishi, wana namba za simu, email hata Kwa kufahamiana.

Kwa kweli wiki hii nzima sijaenda kazin nafuatilia Hela yangu ya sikukuu wateja wangu watasubiri mpaka nitakapofanikisha.

Ninaomba Waziri wetu watumishi atoe maelekezo Kwa maafisa utumishi kuhusu kadhia hii tunayoipata lakini pia afanye mawasiliano na waziri wa Elimu au maafisa wa HESLB watafute namna nyingine ya kupata wadaiwa.
 
Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu ni 🚮. Aisee namuomba tu Mwenyezi Mungu anijalie uhai. Haki ya nani watoto wangu nitawalipia mwenyewe ada mpaka wamalize elimu ya chuo kikuu.

Hii Bodi ina mambo mengi sana ya kijinga. Wanakuwekea wenyewe mkopo walio kukopesha wakati unasoma chuo kikuu kwenye salary slip! Unakatwa kila mwezi kwenye mshahara wako mpaka deni linaisha! Na makato yanakoma.

Halafu baada ya miaka 5 mbele, wanaanza kukukata tena! Unaenda ofisi kwao kuwauliza, wanaleta porojo na kukukabidhi deni jipya! Eti sijui ni retention fees, sijui ulipigwa penati!!

Pumbavu sana hawa.
 
Nilijaza kuomba refund kwa maelekezo ya bodi ya mikopo tawi la Mwanza. Uki confirm data baada ya muda zinarudi kuwa un-confirmed. nimeshaenda pale ofisini kwao mara 5 bila kupewa ufumbuzi. Wanasema tu kwa ufupi tatizo ni system na watashughulikia. Liquidation letter ilitoka tangu 28/03/2022 na tangu wakati huo ni danadana tu hakuna ufumbuzi.
 
Nilijaza kuomba refund kwa maelekezo ya bodi ya mikopo tawi la Mwanza. Uki confirm data baada ya muda zinarudi kuwa un-confirmed. nimeshaenda pale ofisini kwao mara 5 bila kupewa ufumbuzi. Wanasema tu kwa ufupi tatizo ni system na watashughulikia. Liquidation letter ilitoka tangu 28/03/2022 na tangu wakati huo ni danadana tu hakuna ufumbuzi.
Kibaya zaidi wameweka utaratibu wa kwamba lazima uombe hela yako kwa kujaza online lakini kitu cha ajabu hata ukifanya hivyo hawana hata muda wa kupitia maombi hayo .Ndani ya Siku 90 zilizowekwa kisheria kwamba mdai awe amelipwa hazizingatiwi na watu wa bodi .Mdai anaweza akakaa hadi miezi sita hola na wala hakuna updates zozote kinachoendelea.Hivi watu wa bodi mna nini lakini tupeni pesa zetu kwani mnapata faida gani kushindwa kuwarefund watu ambao si wanufaika wa mikopo yenu?
 
Hivi kuna mtu amewahi kupewa deni ila hajawahi kusomea mkopo wa heslb
 
Hii bodi ibinafusishwe tuu kero kweli kweli wangejua mm sijasoma na mkopo mwaka wa kwanza na tabu nilizopata wasingezinhua hata kidogo
 
Kumekuwa na Uzi mbalimbali humu JF zinazoonesha malalamiko mbalimbali ya jinsi bodi ya mikopo Elimu ya juu (HESLB) Kwa kushirikiana na maafisa utumishi kuingiza makato kwenye mishahara ya watumishi wa umma hata ambao hawajawahi kukopeshwa na HESLB ama wengine kumalizana na bodi miaka kadhaa iliyopita kupewa barua kama uthibitisho lakini HESLB imekuwa ikirudisha makato kimakosa na kuleta usumbufu mkubwa katika kufuatilia marekebisho yake.

Ukifika ofisini kwao kudai chako wanakuambia refund inajazwa online, ukijaza hata usitarajie kuipata kwa wakati kwangu mwezi wa pili sasa,hata online feedback haioneshi kama wanafuatilia, ukipiga simu hawapokei yaan ni kero juu ya kero.

Makato haya yanaingizwa kimakosa na maafisa utumishi Kwa kushirikiana na maafisa wa HESLB cha kujiuliza, kwanini hawa maafisa utumishi hawafanyi mawasiliano na wafanyakazi hali wana taarifa zote za watumishi, wana namba za simu, email hata Kwa kufahamiana.

Kwa kweli wiki hii nzima sijaenda kazin nafuatilia Hela yangu ya sikukuu wateja wangu watasubiri mpaka nitakapofanikisha.

Ninaomba Waziri wetu watumishi atoe maelekezo Kwa maafisa utumishi kuhusu kadhia hii tunayoipata lakini pia afanye mawasiliano na waziri wa Elimu au maafisa wa HESLB watafute namna nyingine ya kupata wadaiwa.
Kkila mtumishi tu hivi sasa yuko desperate nchi haieleweki
 
Nipe utaratibu wa kujaza online wanilipe Hela yangu
Andika barua na uitume kwa njia posta EMS fasta unalipwa ila uambatanishe na vitu vifuatavyo
Cheti Cha form 4 kopi
Salary slip inayoonyesha makato ya bodi
Kopi ya kadi ya benki
Kitambulisho Cha kazi
kwenye barua ya maombi weka passport

Utalipwa haraka sana ila hizo za kujaza online utakesha Hadi yesu arudi.Mimi nilihangaika kujaza online Kuna sister mmoja HR mmoja akaniambia andika barua utalipwa chapuchapu na ikawa hivyo

Nilijaza mwezi wa nne mwanzoni watano tarehe 16 mzigo ukaingia.

Hakikisha wakati unaomba kurudishiwa pesa Yako uainishe
Check no
Kazi Yako
Mwajiri wako
Kituo Cha kazi
 
Andika barua na uitume kwa njia posta EMS fasta unalipwa ila uambatanishe na vitu vifuatavyo
Cheti Cha form 4 kopi
Salary slip inayoonyesha makato ya bodi
Kopi ya kadi ya benki
Kitambulisho Cha kazi
kwenye barua ya maombi weka passport

Utalipwa haraka sana ila hizo za kujaza online utakesha Hadi yesu arudi.Mimi nilihangaika kujaza online Kuna sister mmoja HR mmoja akaniambia andika barua utalipwa chapuchapu na ikawa hivyo

Nilijaza mwezi wa nne mwanzoni watano tarehe 16 mzigo ukaingia.

Hakikisha wakati unaomba kurudishiwa pesa Yako uainishe
Check no
Kazi Yako
Mwajiri wako
Kituo Cha kazi
Mjomba nimewahi kuandika barua Tena nikaipereka mwenyewe wakaikataa wanasema utaratibu ni kujaza online
 
Kumekuwa na Uzi mbalimbali humu JF zinazoonesha malalamiko mbalimbali ya jinsi bodi ya mikopo Elimu ya juu (HESLB) Kwa kushirikiana na maafisa utumishi kuingiza makato kwenye mishahara ya watumishi wa umma hata ambao

Ninaomba Waziri wetu watumishi atoe maelekezo Kwa maafisa utumishi kuhusu kadhia hii tunayoipata lakini pia afanye mawasiliano na waziri wa Elimu au maafisa wa HESLB watafute namna nyingine ya kupata wadaiwa.
Duh,

Hii inabidi iwekwe sawa. Safari ya mteja tangu anaomba mkopo akiwa mwanafunzi aliyemaliza sekondari, akiwa chuoni na hata akiwa mhitimu anayerejesha inapaswa kuwa rafiki kadri iwezekanavyo. Akiomba mkopo kwa shida, akawa analipwa kwa shida akiwa chuoni, na urejeshaji ukawa siyo rafiki, jina la kampını linachafuka. Jamaa waongeze nguvu kuifanya safari ya mteja kuwa rafiki.

Ila mnyonge mnyogeni, haki yake mpeni. Kuna mabadiliko makubwa sana ya kiutendaji kaika miaka mitano-sita iliyopita. Kuwa hivi sasa unaomba refund online, ni jambo la kupongeza Kuwa wamejiongeza kwenye teknolojia.

Kingine ninachokiona, ni mifumo yetu kama nchi kutokuongea (not intergrated) kama inavyotarajiwa. Ingekuwa kitambulisho cha NIDA kinabeba kila kitu, ikiwemo mamba ya Form IV (ambayo hao HESLB ndiyo wanaitumia kama unique identifier) nadhani haya madudu yangepungua sana. Unaunganisha mfumo wa HESLB na wa NIDA penye namba za form IV then huwezi kukosea. Lile dude la e-GA la GovESB linaweza kusaidia kama taasisi zote zitaingia mule, bonge la move.

Alamsiki
 

Attachments

  • 1687067768976.png
    1687067768976.png
    9.5 KB · Views: 3
Duh,

Hii inabidi iwekwe sawa. Safari ya mteja tangu anaomba mkopo akiwa mwanafunzi aliyemaliza sekondari, akiwa chuoni na hata akiwa mhitimu anayerejesha inapaswa kuwa rafiki kadri iwezekanavyo. Akiomba mkopo kwa shida, akawa analipwa kwa shida akiwa chuoni, na urejeshaji ukawa siyo rafiki, jina la kampını linachafuka. Jamaa waongeze nguvu kuifanya safari ya mteja kuwa rafiki.

Ila mnyonge mnyogeni, haki yake mpeni. Kuna mabadiliko makubwa sana ya kiutendaji kaika miaka mitano-sita iliyopita. Kuwa hivi sasa unaomba refund online, ni jambo la kupongeza Kuwa wamejiongeza kwenye teknolojia.

Kingine ninachokiona, ni mifumo yetu kama nchi kutokuongea (not intergrated) kama inavyotarajiwa. Ingekuwa kitambulisho cha NIDA kinabeba kila kitu, ikiwemo mamba ya Form IV (ambayo hao HESLB ndiyo wanaitumia kama unique identifier) nadhani haya madudu yangepungua sana. Unaunganisha mfumo wa HESLB na wa NIDA penye namba za form IV then huwezi kukosea. Lile dude la e-GA la GovESB linaweza kusaidia kama taasisi zote zitaingia mule, bonge la move.

Alamsiki
Umeshauri vema sana ila system Zetu Tz ni hovyo sana,operators wengi huwa wazito kuifanyia mifumo frequently check up Ili kuondoa errors
 
Nilijaza kuomba refund kwa maelekezo ya bodi ya mikopo tawi la Mwanza. Uki confirm data baada ya muda zinarudi kuwa un-confirmed. nimeshaenda pale ofisini kwao mara 5 bila kupewa ufumbuzi. Wanasema tu kwa ufupi tatizo ni system na watashughulikia. Liquidation letter ilitoka tangu 28/03/2022 na tangu wakati huo ni danadana tu hakuna ufumbuzi.
Vp mkuu ulishalipwa na bodi?
 
Back
Top Bottom