Egnecious
JF-Expert Member
- Jul 8, 2015
- 879
- 969
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na watoto Bi Ummy Mwalimu amewatoa wasiwasi wazee kuhusu changamoto mbalimbali zinazowakabili ikiwemo upatikanaji wa huduma za afya
Akizungumza na baraza la wazee wa Dar es salaam Bi. Mwalim amesema serikali ya awamu ya tano imejipanga kikamilifu katika kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wazee ikiwemo kuanzisha mfuko wa wazee ambao utawasaidia kupata mikopo ili kujikwamua kimaisha na pia kutoa huduma za afya bure kwenye hospitali za serikali .
Bi Mwalim amesema wizara yake itapeleka sera ya sheria ya wazee bungeni ili iweze kujadiliwa sera ambayo itasaidia sana kutatua changamoto mbalimbali za zinazowakabili wazee.
Kwa upande wa wao baadhi ya wazee wametoa mapendekezo yao kwa waziri ambapo wameombwa kuwepo na ushirikishwaji wa karibu wa wazee pamoja na uwakilishi katika sekta mbalimbali
Akizungumza na baraza la wazee wa Dar es salaam Bi. Mwalim amesema serikali ya awamu ya tano imejipanga kikamilifu katika kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wazee ikiwemo kuanzisha mfuko wa wazee ambao utawasaidia kupata mikopo ili kujikwamua kimaisha na pia kutoa huduma za afya bure kwenye hospitali za serikali .
Bi Mwalim amesema wizara yake itapeleka sera ya sheria ya wazee bungeni ili iweze kujadiliwa sera ambayo itasaidia sana kutatua changamoto mbalimbali za zinazowakabili wazee.
Kwa upande wa wao baadhi ya wazee wametoa mapendekezo yao kwa waziri ambapo wameombwa kuwepo na ushirikishwaji wa karibu wa wazee pamoja na uwakilishi katika sekta mbalimbali