Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,789
- 218,420
Taarifa ya leo inaonyesha kwamba Waziri Mkuu Kasimu Majaliwa amepokea ripoti ya majadiliano kati ya serikali na Wafanyabiashara wa Kariakoo kutoka kwa Tume iliyoundwa ili kutatua mgogoro ulioanzishwa na TRA.
Tunamuomba Mwenyezi Mungu amsaidie Waziri Mkuu ili safari hii ripoti hiyo iwekwe hadharani angalau na sisi wananchi tujue yaliyomo.
---
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Jumatano, Juni 21, 2023, Jijini Dodoma amepokea taarifa ya Kamati Maalum aliyoiunda kwa ajili ya kupitia, kuchambua na kutoa mapendekezo ya kutatua changamoto za Wafanyabiashara nchini.
Taarifa hiyo imekabidhiwa na Mwenyekiti wa kamati, Dkt. John Jingu ambaye pia ni Katibu Mkuu, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum.
Mkutano huo umehudhuriwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenista Mhagama, Waziri Fedha na Mipango, Dkt. Mwigulu Nchemba, Waziri wa Viwanda na Uwekezaji Ashatu Kijaji, Waziri wa Nchi OR – TAMISEMI, Angellah Kairuki, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Ahmad Chande, Makatibu Wakuu, Makamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Wanakamati na Wataalamu kutoka sekta mbalimbali za masuala ya kodi, biashara na uwekezaji.
Akiongea baada ya kupokea taarifa hiyo, Majaliwa amesema Kamati hiyo imefanya kazi kubwa na imeleta majibu ambayo yatatatua changamoto za Wafanyabiashara nchini na ameahidi kuwa Serikali imepokea taarifa hiyo na itayafanyia kazi mapendekezo na ushauri uliotolewa na Kamati hiyo.
Kamati hiyo ambayo ilipewa siku 14, imefanya mapitio katika maeneo mbalimbali ya kikodi, bandari na maeneo ya Wafanyabiashara kwenye Mikoa mbalimbali nchini.
Tunamuomba Mwenyezi Mungu amsaidie Waziri Mkuu ili safari hii ripoti hiyo iwekwe hadharani angalau na sisi wananchi tujue yaliyomo.
---
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Jumatano, Juni 21, 2023, Jijini Dodoma amepokea taarifa ya Kamati Maalum aliyoiunda kwa ajili ya kupitia, kuchambua na kutoa mapendekezo ya kutatua changamoto za Wafanyabiashara nchini.
Taarifa hiyo imekabidhiwa na Mwenyekiti wa kamati, Dkt. John Jingu ambaye pia ni Katibu Mkuu, Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum.
Mkutano huo umehudhuriwa na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenista Mhagama, Waziri Fedha na Mipango, Dkt. Mwigulu Nchemba, Waziri wa Viwanda na Uwekezaji Ashatu Kijaji, Waziri wa Nchi OR – TAMISEMI, Angellah Kairuki, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Ahmad Chande, Makatibu Wakuu, Makamishna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Wanakamati na Wataalamu kutoka sekta mbalimbali za masuala ya kodi, biashara na uwekezaji.
Akiongea baada ya kupokea taarifa hiyo, Majaliwa amesema Kamati hiyo imefanya kazi kubwa na imeleta majibu ambayo yatatatua changamoto za Wafanyabiashara nchini na ameahidi kuwa Serikali imepokea taarifa hiyo na itayafanyia kazi mapendekezo na ushauri uliotolewa na Kamati hiyo.
Kamati hiyo ambayo ilipewa siku 14, imefanya mapitio katika maeneo mbalimbali ya kikodi, bandari na maeneo ya Wafanyabiashara kwenye Mikoa mbalimbali nchini.