abdulahsaf
JF-Expert Member
- Aug 31, 2010
- 858
- 130
[h=1][/h]Written by zenjiboy // 12/07/2011 // Habari // 3 Comments
Na Juma Mohammed,
MAELEZO Zanzibar
Waziri wa Kilimo na Maliasili wa Zanzibar, Mh. Mansoor Yussuf Himid amesema mfumo wa muundo wa Serikali mbili kwa sasa ni butu. Amependekeza kuwepo kwa muundo wa Serikali tatu katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Akichangia makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Ardhi, Makaazi Maji na Nishati leo katika Baraza la Wawakilishi, Waziri Mansoor alisema umefika wakati kufikiria Serikali tatu kwa maslahi ya Wananchi wote.
Mheshimiwa Spika, mfumo wa Serikali mbili ni butu na haufai sasa basi twende katika Serikali tatu Alisema Waziri Mansoor.
Alisema katika dunia ya leo ni ile yenye kusikiliza maoni ya umma, hivyo tabia ya vitisho dhidi ya watu wanaotoa maoni haina nafasi kabisa, matamshi hayo yanaonekana kama kujibu maelezo yaliyotolewa na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta Bungeni aliyesema kwamba hoja ya Serikali tatu ni kutaka kuua Muungano.
Akichangia mjadala huo Sitta alisema siku ambayo Watanzania wataamua kuwa na serikali tatu za muungano, itakuwa ndiyo tiketi ya kuuvunja muungano huo.
Kuunda tena Tanganyika ni kutengeneza mbia mwingine atakayekuwa anashindana na Zanzibar, alisema Sitta.
Alifafanua kuwa hali hiyo itajenga mazingira ya mvutano kwa serikali ya Tanganyika na Zanzibar wa kila mmoja kupigania maslahi yake na Serikali ya Muungano haitakuwa na nguvu kwa sababu uwepo wake utategemea pande hizo mbili.
Mimi simtaji mtu,lakini inaonekana fikra zao ni za zamani kutisha tisha watu, yale maneno ni ya kupotosha zipo sheria za kimataifa kuhusu Territory Water na matumizi ya rasilimali, mambo ya mipaka yameelezwa sana Alisema Waziri Mansoor.
Alisema marekebisho ya Katiba ya Muungano kwa Wazanzibari maana yake ni kujadili Articles of Union na ni vyema tuwaelimishe wananchi wetu wakati ukifika waweze kuitumia vyema fursa hiyo.
Waziri huyo alisisitza msimamo wake kwamba mafuta na gesi asilia sio suala la Muungano na ni lazima yakabakia kwa maslahi ya Wazanzibari.
Makubaliano yetu ni kuyatoa mafuta na gesi asilia katika orodha ya mambo ya Muungano Alisisitiza Waziri huyo na kuongeza kwamba kuzungumzia mafuta na gesi kuwa ya Muungano ni dhambi kubwa.
Kauli ya Waziri huyo inakubaliana na hoja iliyowahi kutolewa na kundi la Wabunge 55 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania maarufu kwa jina la G 55 lilipotaka kuundwa kwa Serikali ya Tanganyika mwaka 1993.
Hoja hiyo ilizimwa na marehemu Mwalimu Julius Nyerere ambaye mbali ya kuwatuhumu Waziri Mkuu na Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi kwa wakati ule, Holice Kolimba na John Samwel Malecela kwa kumshauri vibaya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ali Hassan Mwinyi.
Kutokana na suala hilo, Rais Mwinyi alivunja Baraza la Mawaziri na aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM, Kolimba alihojiwa na Chama chake.
Hadi sasa msimamo wa CCM katika muundo wa Muungano ni kuwa na Serikali mbili ambazo mara kadhaa zimekuwa ikitetea msimamo huo katika mijadala mbalimbali.
Chanzo: Blogu ya Jamii (Issa Michuzi)
Na Juma Mohammed,
MAELEZO Zanzibar
Waziri wa Kilimo na Maliasili wa Zanzibar, Mh. Mansoor Yussuf Himid amesema mfumo wa muundo wa Serikali mbili kwa sasa ni butu. Amependekeza kuwepo kwa muundo wa Serikali tatu katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Akichangia makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Ardhi, Makaazi Maji na Nishati leo katika Baraza la Wawakilishi, Waziri Mansoor alisema umefika wakati kufikiria Serikali tatu kwa maslahi ya Wananchi wote.
Mheshimiwa Spika, mfumo wa Serikali mbili ni butu na haufai sasa basi twende katika Serikali tatu Alisema Waziri Mansoor.
Alisema katika dunia ya leo ni ile yenye kusikiliza maoni ya umma, hivyo tabia ya vitisho dhidi ya watu wanaotoa maoni haina nafasi kabisa, matamshi hayo yanaonekana kama kujibu maelezo yaliyotolewa na Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samuel Sitta Bungeni aliyesema kwamba hoja ya Serikali tatu ni kutaka kuua Muungano.
Akichangia mjadala huo Sitta alisema siku ambayo Watanzania wataamua kuwa na serikali tatu za muungano, itakuwa ndiyo tiketi ya kuuvunja muungano huo.
Kuunda tena Tanganyika ni kutengeneza mbia mwingine atakayekuwa anashindana na Zanzibar, alisema Sitta.
Alifafanua kuwa hali hiyo itajenga mazingira ya mvutano kwa serikali ya Tanganyika na Zanzibar wa kila mmoja kupigania maslahi yake na Serikali ya Muungano haitakuwa na nguvu kwa sababu uwepo wake utategemea pande hizo mbili.
Mimi simtaji mtu,lakini inaonekana fikra zao ni za zamani kutisha tisha watu, yale maneno ni ya kupotosha zipo sheria za kimataifa kuhusu Territory Water na matumizi ya rasilimali, mambo ya mipaka yameelezwa sana Alisema Waziri Mansoor.
Alisema marekebisho ya Katiba ya Muungano kwa Wazanzibari maana yake ni kujadili Articles of Union na ni vyema tuwaelimishe wananchi wetu wakati ukifika waweze kuitumia vyema fursa hiyo.
Waziri huyo alisisitza msimamo wake kwamba mafuta na gesi asilia sio suala la Muungano na ni lazima yakabakia kwa maslahi ya Wazanzibari.
Makubaliano yetu ni kuyatoa mafuta na gesi asilia katika orodha ya mambo ya Muungano Alisisitiza Waziri huyo na kuongeza kwamba kuzungumzia mafuta na gesi kuwa ya Muungano ni dhambi kubwa.
Kauli ya Waziri huyo inakubaliana na hoja iliyowahi kutolewa na kundi la Wabunge 55 wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania maarufu kwa jina la G 55 lilipotaka kuundwa kwa Serikali ya Tanganyika mwaka 1993.
Hoja hiyo ilizimwa na marehemu Mwalimu Julius Nyerere ambaye mbali ya kuwatuhumu Waziri Mkuu na Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi kwa wakati ule, Holice Kolimba na John Samwel Malecela kwa kumshauri vibaya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ali Hassan Mwinyi.
Kutokana na suala hilo, Rais Mwinyi alivunja Baraza la Mawaziri na aliyekuwa Katibu Mkuu wa CCM, Kolimba alihojiwa na Chama chake.
Hadi sasa msimamo wa CCM katika muundo wa Muungano ni kuwa na Serikali mbili ambazo mara kadhaa zimekuwa ikitetea msimamo huo katika mijadala mbalimbali.
Chanzo: Blogu ya Jamii (Issa Michuzi)